RC RUGIMBANA: VYUO VITOE USHIRIKIANO WA KUTOSHA KWA HESLB
Afisa Tawala Msaidizi (Elimu) wa Mkoa wa Dodoma Bw. Gosbert Damazo akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa kazi wa siku ya mbili kati ya HESLB na maafisa wasimamizi wa madawati ya mikopo ya elimu ya juu kutoka taasisi za elimu ya juu mjini Dodoma leo (Alhamisi, Machi 16, 2017).
HomeJamii

RC RUGIMBANA: VYUO VITOE USHIRIKIANO WA KUTOSHA KWA HESLB

N a Mwandishi Wetu Mkuu wa Mkoa (RC) wa Dodoma, Jordan Rugimbana amezikumbusha taasisi za elimu ya juu nchini kuhakikisha zinaongeza ...

SAA 144 ZA MAXENCE MELO NDANI YA MAHABUSU!
MRADI MKUBWA WA UMEME WA BACKBONE UMEKAMILIKA, KUZINDUALIWA JANUARI
MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA VIONGOZI WA CHAMA CHA WAFANYABIASHARA WA CHINA JIJINI DAR E SALAAM

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Mkoa (RC) wa Dodoma, Jordan Rugimbana amezikumbusha taasisi za elimu ya juu nchini kuhakikisha zinaongeza uwezo wa madawati ya mikopo yaliyopo katika taasisi zao ili yaweze kutoa ushirikiano unaotakiwa katika kutatua changamoto za utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.

Mkuu wa Mkoa huyo ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Machi 17, 2017) wakati akifungua mkutano wa kazi wa siku mbili kati ya watendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) na maafisa mikopo zaidi ya 100 kutoka taasisi za elimu ya juu nchini wanaokutana katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

“Majukumu ya Bodi ni mazito na hivyo Bodi inahitaji ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wadau mbalimbali mkiwemo nyie maafisa mikopo mliopo vyuoni na mnaokutana na wanafunzi kila siku,” amesema Rugimbana katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Katibu Tawala Msaidizi (Elimu) wa Mkoa wa Dodoma, Bw. Gosbert Damazo.

Akizungumza katika mkutano huo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru amesema Bodi yake inatambua mchango mkubwa unaotolewa na maafisa mikopo hao katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu waliopo katika taasisi mbalimbali.

“Maafisa hawa ndio wanaotuunganisha na wanafunzi katika utendaji kazi wetu wa kila siku, hivyo ni watu muhimu sana kwetu na tunathamini sana mchango wao na wa taasisi zao kwa ujumla,” amesema Bw. Badru.

Kwa mujibu wa Bw. Badru, Bodi yake itatumia mkutano huo wa siku mbili kuwakumbusha maafisa hao wajibu wao katika kutunza kumbukumbu muhimu za wanufaika wa mikopo na majukumu yao muhimu ili kuongeza ufanisi na hivyo kupunguza malalamiko ya wadau wakiwemo wanafunzi wanaoufaika wa mikopo ya elimu ya juu.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji huyo alikumbusha kuwa mwaka 2011, Serikali ilivielekeza vyuo vyote vya elimu ya juu nchini kuanzisha madawati ya mikopo ya elimu ya juu ili kuongeza ufanisi katika usimamizi wa mikopo ya elimu ya juu inayotolewa na Serikali.

“Tangu wakati huo (2011), kumekuwa na mafanikio makubwa katika utendaji wetu kutokana na kuongezeka kwa ufanisi. Hivi sasa, malalamiko kutoka kwa wanafunzi yamepungua sana kwa kuwa wana sehemu ya kuwasilisha hoja zao palepale chuoni …wito wangu kwao ni kuwa wayatumie madawati haya vizuri,” amesema Bw. Badru.

Naye Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Taaluma) Prof. Lawrence Msoffe, ambaye alihudhuria hafla ya ufunguzi, amesema mkutano huo ni muhimu kwa kuwa utaisaidia Bodi kupata mrejesho kutoka kwa maafisa hao ambao ndio wanaosimamia masuala ya utoaji mikopo katika vyuo kila siku.

HESLB ilianzishwa kwa mujibu wa sheria mwaka 2004 na kuanza kazi rasmi mwezi Julai 2005 ili, pamoja na mambo mengine, kutoa mikopo ya elimu ya juu kwa wanafunzi watanzania wasio na uwezo na pia kukusanya mikopo iliyoiva iliyotolewa na Serikali tangu mwaka 1994/1995.


 Baadhi washiriki wa mkutano wa kazi kati ya HESLB na maafisa wasimamizi wa madawati ya mikopo ya elimu ya juu kutoka taasisi za elimu ya juu wakiwa katika picha ya pamoja mjini Dodoma leo (Alhamisi, Machi 16, 2017).

HESLB Dodoma 3: Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru akiongea katika mkutano kazi wa siku ya mbili kati ya HESLB na maafisa wasimamizi wa madawati ya mikopo ya elimu ya juu kutoka taasisi za elimu ya juu mjini Dodoma leo (Alhamisi, Machi 16, 2017). (Picha na Veneranda Malima – HESLB).
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: RC RUGIMBANA: VYUO VITOE USHIRIKIANO WA KUTOSHA KWA HESLB
RC RUGIMBANA: VYUO VITOE USHIRIKIANO WA KUTOSHA KWA HESLB
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEia2RX2G9yOCblFOsBcZaNwH6uc0IzQORbKACW5AHWd8CWISJtvRuQt77TevSZlhL8K9vkSHlFX1axZXnRPFnBhHdeF13AAa8Q0JIMAsN84p8EzagU3aJLN8X4bXqKIxh32jYPqvqmnae4/s640/HESLB+Dodoma+1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEia2RX2G9yOCblFOsBcZaNwH6uc0IzQORbKACW5AHWd8CWISJtvRuQt77TevSZlhL8K9vkSHlFX1axZXnRPFnBhHdeF13AAa8Q0JIMAsN84p8EzagU3aJLN8X4bXqKIxh32jYPqvqmnae4/s72-c/HESLB+Dodoma+1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/03/rc-rugimbana-vyuo-vitoe-ushirikiano-wa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/rc-rugimbana-vyuo-vitoe-ushirikiano-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy