WAZIRI PROF. MBARAWA AFANYA MAZUNGUMZO NA UJUMBE KUTOKA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA CONGO

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizungumza na Gavana wa Lubumbashi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia y...

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizungumza na Gavana wa Lubumbashi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Jean Claude Kazembe kuhusu mipango endelevu ya matumizi mazuri ya Bandari ya Dar es Salaam ofisini kwake jijini Dar es Salaam.(Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano)


Stori na Biseko Ibrahim.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amewataka watumishi wa Wizara hiyo Sekta ya Uchukuzi kutumia vizuri fursa ya kuhamia Dodoma kwa kuwatumikia watanzania kwa uadilifu na weledi.
Amesema hayo jijini Dar es Salaam wakati akiwaaga watumishi wa Sekta ya uchukuzi wa awamu ya kwanza ambao wameondoka leo kuelekea mjini Dodoma.
“Nawapongeza kwa kupata fursa ya kuwa katika awamu ya kwanza katika Wizara hii kuhamia Dodoma fahamuni hii ni fursa na si changamoto kwani hatua hii inasogeza huduma karibu na wananchi hivyo watumikieni kwa moyo”, amesema Prof. Mbarawa.
Prof. Mbarawa amesema kuwa nia ya Serikali ni kuhakikisha watumishi wake wanahamia Dodoma na kuendelea na utekelezaji wa majukumu yake kwa wananchi.
Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa Sekta ya Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho amesema awamu ya kwanza ya watumishi zaidi ya 45 inahamia Dodoma mwezi huu na Awamu ya pili itaanza mwezi wa Machi na watumishi wote wa sekta ya uchukuzi watakuwa Dodoma ifikapo Agosti mwaka huu.
“Watumishi wa Sekta ya Uchukuzi wanaohamia Dodoma katika awamu ya kwanza ni pamoja na Katibu Mkuu Sekta ya Uchukuzi, Wakurugenzi na Wakurugenzi wasaidizi, wakuu wa vitengo na maafisa waandamizi”, amesisitiza Dkt. Chamuriho.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Sekta ya Uchukuzi), Dkt. Leornard Chamuriho kabla ya kuwaaga watumishi wa Wizara hiyo  wanaohamia Dodoma leo, jijini Dar es salaam. (Picha na Biseko Ibrahim).

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI PROF. MBARAWA AFANYA MAZUNGUMZO NA UJUMBE KUTOKA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA CONGO
WAZIRI PROF. MBARAWA AFANYA MAZUNGUMZO NA UJUMBE KUTOKA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA CONGO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjdZpvMnubMg6FHAHghQ43RpKfnMnVLjPZ6qsZx_zKmz1Grd07qWQ7ri8pFj6lx9k5E-c-UiaK1izLdMjdhIaoccnYz9q3w8MQnwx-79Jgswbyj9jDL74xcaz5iXnhqs5jDEZUtNtw53MM/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjdZpvMnubMg6FHAHghQ43RpKfnMnVLjPZ6qsZx_zKmz1Grd07qWQ7ri8pFj6lx9k5E-c-UiaK1izLdMjdhIaoccnYz9q3w8MQnwx-79Jgswbyj9jDL74xcaz5iXnhqs5jDEZUtNtw53MM/s72-c/1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/02/waziri-prof-mbarawa-afanya-mazungumzo.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/02/waziri-prof-mbarawa-afanya-mazungumzo.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy