WAZIRI MKUU ATAKA MASHIRIKA YA UMMA YAISHAURI SERIKALI

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Wakuu wa Mashirika ya Umma ulioandaliwa kwa ushirikiano baina ya Taasisi ya Uongozi na Msajili wa Hazina leo Jijini Dar es Salaam. Lengo la mkutano huo ni kujadili nafasi ya Mashirika ya Umma katika utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016/17 -2020/21. Kutoka kulia ni Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja na Kaimu Msajili wa Hazina, Elias Mwakibinga.
HomeJamii

WAZIRI MKUU ATAKA MASHIRIKA YA UMMA YAISHAURI SERIKALI

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameyataka mashirika na taasisi za umma yaangalie utendaji wa Serikali ya awamu ya tano katika kipind...

JKCI KUANZA UPASUAJI WA KUPANDIKIZA MOYO
MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA ALAANI NA KUKEMEA VIKALI VITENDO VYA UKEKETAJI WA WANAWAKE NA UBAKAJI VINAVYOENDELEA KATIKA JAMII
WAFANYAKAZI WANAWAKE WA PPF WAUNGANA NA WENZAO KUSHEREHEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI







WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameyataka mashirika na taasisi za umma yaangalie utendaji wa Serikali ya awamu ya tano katika kipindi cha mwaka mmoja na yatoe ushauri wa namna bora ya kuboresha maendeleo nchini.

Ametoa kauli hiyo leo asubuhi (Jumanne, Februari 28, 2017) wakati akifungua Mkutano wa kujadili Nafasi ya Mashirika ya Umma katika Utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano Ikulu jijini Dar es Salaam.

Akifungua mkutano huo wa siku moja kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Waziri Mkuu amesema ana imani kuwa washiriki wa mkutano huo wataangalia uzoefu ambao Serikali imeupata katika mwaka mmoja tangu iingie madarakani na kushauri namna bora ya kukabiliana ba vikwazo ambavyo vimejitokeza.

“Ninaamini mtaangalia uzoefu tulioupata kwa mwaka mmoja uliopita ambao Serikali hii imekuwa madarakani, mtaangalia ni mpango upi tuliopanga na upi umefanikiwa ama upi umekwama na nini kilisababisha vikwazo hivyo vitokee,” amesema.

Alisema matarajio ya Serikali kutokana na mkutano huo ni kwamba washiriki wa wataainisha namna mashirika ya umma yatakavyoweza kuchangia katika utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo hususan katika kujenga uchumi wa viwanda.

“Ninaamini mtaweka wazi hatua za haraka za kisheria na za kimuundo zinazotakiwa kuchukuliwa na Serikali ili ushiriki wa mashirika yetu usikumbane na mikingamo ya kisheria na vikwazo vya mazoea ya watumishi na watendaji,” amesema.

Amesema anatarajia kuwa washiriki wa mkutano huo watapendekeza namna mashirika yanavyoweza kuunganisha nguvu katika kutekeleza aina fulani ya mradi na ushirika huo ukawa na tija.

“Kutokana na majadiliano yenu, naamini mtaainisha vihatarishi (risks) vilivyopo kwa mashirika ya Serikali  kushiriki moja kwa moja kwenye utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo na kupendekeza mbinu za kukabiliana na vihatarishi hivyo; na pia mtashauri namna bora ya kutekeleza mapendekezo yenu bila kuathiri majukumu mahsusi ya uanzishwaji wa mashirika,” amesema.

Amesema yaya binafsi anasubiri kwa shauku kubwa, muhtasari wa mkutano huo ambao anataraji utakuwa na mapendekezo yanayotekelezeka ya namna gani mashirika yaliyopo nchini kwa umoja wake au moja moja yanavyoweza kushiriki kikamilifu kwenye ajenda hiyo ya maendeleo.



IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, FEBRUARI 28, 2017.












Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Wakuu wa Mashirika ya Umma ulioandaliwa kwa ushirikiano baina ya Taasisi ya Uongozi na Msajili wa Hazina leo Jijini Dar es Salaam. Lengo la mkutano huo ni kujadili nafasi ya Mashirika ya Umma katika utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016/17 -2020/21. Kutoka kulia ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja na Kaimu Msajili wa Hazina, Elias Mwakibinga.


Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja akielezea jambo wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Wakuu wa Mashirika ya Umma ulioandaliwa kwa ushirikiano baina ya Taasisi ya Uongozi na Msajili wa Hazina leo Jijini Dar es Salaam. Lengo la mkutano huo ni kujadili nafasi ya Mashirika ya Umma katika utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016/17 -2020/21. Kutoka kulia ni Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Maduka Kessy, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa na Kaimu Msajili wa Hazina, Elias Mwakibinga.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (katikati) pamoja na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (kulia) na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja wakifuatilia matukio katika mkutano huo.


Mhariri Mtendaji wa  Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) inayozalisha magazeti ya na DailyNews HabariLeo, SundayNews na SpotLeo. Dkt. Jim Yonaz akiteta jambo na Mkuu wa Kitengo cha Utafiti na Ubunifu wa kampuni hiyo Ichikael Maro waliposhiriki katika mkutano huo, ulioandaliwa kwa ushirikiano baina ya Taasisi ya Uongozi na Msajili wa Hazina leo Jijini Dar es Salaam.




Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa Wakuu wa Mashirika ya Umma ulioandaliwa kwa ushirikiano baina ya Taasisi ya Uongozi na Msajili wa Hazina wakifuatilia mkutano huo  leo Jijini Dar es Salaam. Lengo la mkutano huo ni kujadili nafasi ya Mashirika ya Umma katika utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016/17 -2020/21.



Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa  akiagana na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja mara baada ya kufungua Mkutano wa Wakuu wa Mashirika ya Umma ulioandaliwa kwa ushirikiano baina ya Taasisi ya Uongozi na Msajili wa Hazina wakifuatilia mkutano huo  leo Jijini Dar es Salaam. Lengo la mkutano huo ni kujadili nafasi ya Mashirika ya Umma katika utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016/17 -2020/21.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa  akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Mkutano wa Wakuu wa Mashirika ya Umma ulioandaliwa kwa ushirikiano baina ya Taasisi ya Uongozi na Msajili wa Hazina wakifuatilia mkutano huo  leo Jijini Dar es Salaam. Lengo la mkutano huo ni kujadili nafasi ya Mashirika ya Umma katika utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016/17 -2020/21. (Picha na Frank Shija – MAELEZO).
https://ssl.gstatic.com/ui/v1/icons/mail/images/cleardot.gif

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI MKUU ATAKA MASHIRIKA YA UMMA YAISHAURI SERIKALI
WAZIRI MKUU ATAKA MASHIRIKA YA UMMA YAISHAURI SERIKALI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjdQ4S6wLGKtneY-Tx1zv4XW9vQdm7uqWQe5p452g3VdPDdmwrgVsO070D67Fl6udj5yq8lWr4Dt-5sg0X6FSG3SLMT73L3YMZa3xa_UkFUbpkSG-qnw9ZNtV3mvqOmSO0VCCVzBt27uC4/s640/PIX1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjdQ4S6wLGKtneY-Tx1zv4XW9vQdm7uqWQe5p452g3VdPDdmwrgVsO070D67Fl6udj5yq8lWr4Dt-5sg0X6FSG3SLMT73L3YMZa3xa_UkFUbpkSG-qnw9ZNtV3mvqOmSO0VCCVzBt27uC4/s72-c/PIX1.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/02/waziri-mkuu-ataka-mashirika-ya-umma.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/02/waziri-mkuu-ataka-mashirika-ya-umma.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy