HomeJamii

RC RUKWA AKUTANA NA WADHIBITI UBORA WA SHULE KUJUA CHANZO CHA KUSHUKA KWA ELIMU RUKWAB

  Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amekutana na wadhibiti ubora wa shule wa halmashauri nne za Mkoa wa Rukwa k...

GAZETI LA MWANAHALISI LATAKIWA KUOMBA RADHI TUME YA UCHAGUZI (NEC)
EU INJECTS TZS. 1.4 BILLION TO COUNTER CHILD MARRIAGE AND FGM
DAWASCO YASHAURIWA KUTOA HUDUMA KWA UWAZI



 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amekutana na wadhibiti ubora wa shule wa halmashauri nne za Mkoa wa Rukwa kujua changamoto wanazokumbana nazo na mambo yanayopelekea kushuka kwa elimu katika mkoa wa Rukwa.




Zelote Stephen alifikia uamuzi wa kuwaita wadhibiti hao baada ya Mkoa wa Rukwa kushuka kielimu kutoka nafasi ya 6 mwaka 2015 hadi nafasi ya 12 kati ya Mikoa 31 kwa mwaka 2016 kwa mitihani ya kidato cha 4, na pia kuteremka katika mitihani ya kidato cha pili kutoka nafasi ya 20 kwa mwaka 2015 hadi nafasi ya 21 kwa mwaka 2016.




Wadhibiti hao walielezea sababu kede kede zilizopelekea kushuka kwa kiwango cha elimu katika Mkoa wa Rukwa na miongoni mwao ni kutopewa mrejesho wa taarifa za kila wiki wanazoziandika na kukabidhi kwa wakurugenzi wa halmashauri na wakuu wa wilaya.




“Toka Mwezi July mwaka jana tumeshaandika ripoti nyingi tu zinazoelezea mapungufu kama vile, upungufu wa waalimu kwa baadhi ya masomo, matundu cha vyoo, vitabu vya kusomea, nakadhalika lakini hakuna hata mrejesho tunaoupata kutoka kwa Mkurugenzi,” Goreth Ntulo alieleza.




Kwa upande mwingine sababu zinazokwamisha ufanisi wa kazi za wadhibiti hao wanadai kutopewa motisha na mwajiri wao na kuwasababisha kuishi katika maisha magumu.




“Mimi sijawahi kwenda likizo kwa fedha ya serikali tangu nianze kufanya kazi na madarasha hatupandishwi n ahata ukipandishwa inabaki jina tu lakini mshahara upo pale pale na kuapata hiyo fedha ya daraja ulilopandishwa ni kazi kubwa ya kukatisha tamaa,” Mmoja wa wadhibiti hao Mama Jairo alifafanua.




Nae Mkuu wa Mkoa baada ya kusikiliza malalamiko hayo aliwaagiza wakurugenzi wote kuhakikisha kwamba wadhibiti hao wanapatiwa mrejesho juu ya kasoro walizozibaini baada ya kufanya ukaguzi katika mashule hayo.




“Kwani hizi shule ni za nani?, Si ni za wakurugenzi, sasa naagiza wakurugenzi wote wawe wanatoa mrejesho kwenu ili muweze kujua ni lipi linawezekana kurekebishika na kwa kipindi gani na nili lipi haliwezekani ili Mkae mkijua, bila ya hivyo itakuwa haina maana nyinyi kufanya ukaguzi halafu ripoti zikarundikwa kwenye madroo,” Zelote Stephen alikazia.




Pia Mkuu wa Mkoa aliwasisitiza wakati wakaguzi hao wanawapa wakurugenzi ripoti hizo wahakikishe kuwa wanawapa na “dead line” na wakurugeni wazingatie na wawaheshimu na kuwathamini ili kila mmoja afanye kazi yake ambayo ameajiriwa nayo.




“Kama Mlikuwa na uwoga muondoe ofisi hii itawapa sapote, na make mkijua kuwa tunawathamini sana maana kupitia nyinyi tunajifunza mengi sana ambayo ndio yanatupa mpango mkakati wa kuhakikisha tunapeleka elimu mbele,” Zelote Stephen aliwahakikishia.




Mmoja wa wadhibiti hao Pracida Rwegasira alitoa shukrani zake za dhati kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kwa kuchukua uamuzi wa kuwaita ili kutoa mchango wao katika kupeleka sekta ya elimu mbele na kuongeza kuwa tokea aanze kazi hiyo hawajawahi kuitwa na Mkuu wa Mkoa.




Nae Katibu Tawala wa Mkoa Tixon Nzunda aliahidi kutetea haki zao za kiutumishi na kuwa sauti ya kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elmu.




Imeandikwa na


Abdulrahman Salim


Kaimu Afisa habari Mkoa wa Rukwa
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: RC RUKWA AKUTANA NA WADHIBITI UBORA WA SHULE KUJUA CHANZO CHA KUSHUKA KWA ELIMU RUKWAB
RC RUKWA AKUTANA NA WADHIBITI UBORA WA SHULE KUJUA CHANZO CHA KUSHUKA KWA ELIMU RUKWAB
https://i.ytimg.com/vi/XBJJJXA5KXc/hqdefault.jpg
https://i.ytimg.com/vi/XBJJJXA5KXc/default.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/02/rc-rukwa-akutana-na-wadhibiti-ubora-wa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/02/rc-rukwa-akutana-na-wadhibiti-ubora-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy