MAFUNZO YA UKAKAMAVU KIDATO CHA KWANZA JITEGEMEE JKT SEKONDARY YAFUNGWA RASMI JIJINI DAR ES SALAAM
HomeJamii

MAFUNZO YA UKAKAMAVU KIDATO CHA KWANZA JITEGEMEE JKT SEKONDARY YAFUNGWA RASMI JIJINI DAR ES SALAAM

  Mgeni rasmi wa kufunga mafunzo ya ukakamavu kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza wa Shule ya Jitegemee Sekondari Mgulani JKT, Meja Hau...

MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI(WCF) UMEKUWA MSHINDI WA PILI KATIKA MASUALA YA USALAMA NA AFYA MAHALA PA KAZI
DK. KIGWANGALLA ATOA OFA YA MAPUMZIKO YA FUNGATE YA ALI KIBA KATIKA HIFADHI ZA WANYAMAPORI
RAIS MAGUFULI AFUNGUA BARABARA YA IRINGA-DODOMA KM 189



 Mgeni rasmi wa kufunga mafunzo ya ukakamavu kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza wa Shule ya Jitegemee Sekondari Mgulani JKT, Meja Haule (katikati), akiwa na viongozi wengine wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo Dar es Salaam leo asubuhi. Kutoka kulia ni Ofisa Tawala wa Kombania wa shule hiyo, Kepteni Zaujia Shemahonga, Msanifu wa Shule, Meja Rehema Wanjara, , Makamu Mkuu wa Shule Utawala, Kepteni Benitho Lubila na Makamu Mkuu wa Shule Taaluma, Ema Mosha.

 Paredi la ukakamavu na uzalendo likifanyika.


 Gwaride likitoa heshima mbele ya mgeni rasmi.


 Ndugu, wazazi na jamaa wa wanafunzi hao wakifuatilia kwa karibu shughuli hiyo.
 wanafunzi wa shule hiyo wakifuatilia gwaride hilo.


 Gwaride likiendelea.
 wazazi wakiwa kwenye hafla hiyo.
 Wimbo maalumu ukiimbwa.
 Kiongozi wa gwaride hilo, Pelegia Nyunga akikabidhiwa zawadi na mgeni rasmi.
 Francis Christopher akipewa zawadi.
 Mwanahawa Shabani akikabidhiwa zawadi.
 Salehe Hemedi akipata zawadi yake.
 Nuhu Sajilo akipata zawadi.
 Furaha na utamu wa gwaride hilo.
 James David akikabidhiwa zawadi.



 Miriam Simon akipata zawadi


 Ofisa Tawala wa Kombania wa shule hiyo, Kepteni Zaujia Shemahonga akizungumza katika hafla hiyo.
 Makamu Mkuu wa Shule Utawala, Kepteni Benitho Lubila, akitoa hutuba fupi kaba ya kumkaribisha mgeni rasmi.



Wimbo wa taifa ukiimbwa.


 Wimbo wa Taifa ukiimbwa.


Brass Band ya JKT ikiongoza gwaride hilo.

Na Dotto Mwaibale

WANAFUNZI nchini wametakiwa kuacha kujiingiza katika makundi yasiofaa ili kujiepusha na kujihusisha na dawa la kulevya.

Mwito huo umetolewa na Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Mgulani, Meja Haule wakati akifunga mafunzo ya ukakamavu kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza wa Shule ya Sekondari ya Jitegemee Dar es Salaam leo.

"Wanafunzi acheni kujihusisha na makundi yasiofaa ili kujiepusha kuingia katika vishawishi vya matumizi ya dawa za kulevya" alisema Meja Haule.

Aliwataka wanafunzi hao kutumia muda wao wote kwa kusoma ili kutimiza ndoto za maisha yao kwa kupata elimu bora.

Meja Haule aliwataka wanafunzi wa kike kujiepusha na tamaa mbalimbali kwani wao wapo katika hatari ya kupata vishawishi na aliwataka kujifunza kwa wanawake waliofanikiwa na kufanya vizuri kwa kuwa viongozi katika taifa.

Haule aliziomba shule zilizopo chini ya jeshi kuiga mfano wa shule ya Jitegemee ya kutoa mafunzo hayo ya ukakamavu kwani yanawafanya wanafunzi hao kuwa wazalendo wa nchi yao.

Makamu Mkuu wa Shule Utawala Kepteni Benitho Lubida alisema wanafunzi waliopata mafunzo hayo ni 604 na walitumia wiki tatu kufuzu.

Alisema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wanafunzi hao wa kujitegemea, kuwafanya wawe na nidhamu, kujiamini, kuwa wavumilivu na kujiamini.

Aliwaomba wazazi wa wanafunzi hao kuwa wa kwanza kutoa mafunzo mbalimbali kwa watoto wao ili kuwajenga katika misingi mizuri kuanzia ngazi ya familia.

(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAFUNZO YA UKAKAMAVU KIDATO CHA KWANZA JITEGEMEE JKT SEKONDARY YAFUNGWA RASMI JIJINI DAR ES SALAAM
MAFUNZO YA UKAKAMAVU KIDATO CHA KWANZA JITEGEMEE JKT SEKONDARY YAFUNGWA RASMI JIJINI DAR ES SALAAM
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj0qZrNOR3ppItBLS4hmLoy03otO6-sd3g4LH9eqqcbrRA0sjjFuh8DEM_-3JyCY_XBi6rpPY9Bra8nK_w-Cehnj02fUVRwWCeyoBe3vlkzT8k4PMTWMubx7BbeaivMJMyCRhL1k4KGYZcw/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj0qZrNOR3ppItBLS4hmLoy03otO6-sd3g4LH9eqqcbrRA0sjjFuh8DEM_-3JyCY_XBi6rpPY9Bra8nK_w-Cehnj02fUVRwWCeyoBe3vlkzT8k4PMTWMubx7BbeaivMJMyCRhL1k4KGYZcw/s72-c/1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/02/mafunzo-ya-ukakamavu-kidato-cha-kwanza.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/02/mafunzo-ya-ukakamavu-kidato-cha-kwanza.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy