WAZIRI NDALICHAKO AITUNUKU NISHANI GLOBAL EDUCATION LINK
HomeJamii

WAZIRI NDALICHAKO AITUNUKU NISHANI GLOBAL EDUCATION LINK

WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako ameitunuku nishani ya uzalendo kampuni ya Globa...


WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako ameitunuku nishani ya uzalendo kampuni ya Global Education Link (GEL) kutokana na mchango inaotoa katika maendeleo ya elimu nchini.

Nishani hiyo aliitoa leo wakati akizindua mkutano mkuu wa 11 wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari nchini (TAHOSSA) mkoani Dodoma. 
 
Mkurugenzi wa Global Education Link (kulia) akipokea tuzo kutoka kwa Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya ufundi, Profesa Joyce Ndalichako.

Rais wa Wakuu wa Sekondari Tanzania (TAHOSSA), Bonus Ndimbo alisema GEL imekuwa ni mdau mkubwa wa maendeleo katika elimu, sio tu kwa TAHOSSA hata kwa nchi kwa ujumla.
“Tunaipongeza sana Global Education Link, kwani imekuwa karibu na jamii, imekuwa karibu na sekta ya Elimu na maendeleo ya nchi kwa ujumla,” alisema Katibu Mkuu wa TAHOSSA Diana Matemu.Global Education Link ni kampuni iliyoanzishwa Mwaka 2006 kwa lengo la kuwaunganisha wanafunzi wa Tanzania wanaotaka kusoma vyuo vikuu vya nje.
Tangu imeanza shughuli zake kwa miaka 10 sasa, zaidi ya wanafunzi 5400 wamefaidika kwa kuunganishwa na vyuo mbalimbali vilivyoko Marekani, Canada, Uingereza, Afrika Kusini, Ukraine, India, Urusi, Malaysia, China na nyinginezo. 
Mkurugenzi Mkuu wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel akizungumza na Wakuu wa Sekondari Tanzania baada ya kupewa nafasi ya kipekee ya kuwawakilisha wadau mbalimbali wa elimu waliokaribishwa katika mkutano huo mbele ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Ufundi stadi Prof Joyce Ndalichako.
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA) wakimsikiliza Mkurugenzi wa Global Education Link, Abdulmalik Mollel (hayuko pichani).
Akizungumza baada ya kukabidhiwa nishani hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel alishukuru na kusema anafanya hivyo kwa lengo la kusaidia Serikali na Watanzania kwa ujumla katika kuharakisha maendeleo nchini.
Kikubwa ambacho Mkurugenzi wa GEL alisema ni kuwa mpango wa mafunzo kwa wanafunzi utasaidia kuwafanya wanafunzi kuchagua kozi ambazo zitakuwa na tija kwao na taifa kwa ujumla.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI NDALICHAKO AITUNUKU NISHANI GLOBAL EDUCATION LINK
WAZIRI NDALICHAKO AITUNUKU NISHANI GLOBAL EDUCATION LINK
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgFqKCDMdmXnFwAEYl9ji3KvJ7Dmf9OArmE_J_L9g_m4YPOcRyS9ye86RARN5nAmM1gjx2fweE9_Cn6dVNy74qTNxudq8iIbMRBXobv1L41n5kg650zQibDtWabGudPwzhrQ_AZCuqkO3J7/s640/New+Picture.png
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgFqKCDMdmXnFwAEYl9ji3KvJ7Dmf9OArmE_J_L9g_m4YPOcRyS9ye86RARN5nAmM1gjx2fweE9_Cn6dVNy74qTNxudq8iIbMRBXobv1L41n5kg650zQibDtWabGudPwzhrQ_AZCuqkO3J7/s72-c/New+Picture.png
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/12/waziri-ndalichako-aitunuku-nishani.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/12/waziri-ndalichako-aitunuku-nishani.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy