NEC KUZIALIKA ASASI ZA KIRAIA KUTOA ELIMU YA MPIGA KURA KWA KILA MTANZANIA
Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Emmanuel Kawishe
HomeSiasa

NEC KUZIALIKA ASASI ZA KIRAIA KUTOA ELIMU YA MPIGA KURA KWA KILA MTANZANIA

Hussein Makame, NEC 2/11/2016. Dar es Salaam.   Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa itazialika Asasi za Kiraia zina...




Hussein Makame, NEC
2/11/2016. Dar es Salaam.
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa itazialika Asasi za Kiraia zinazotaka kutoa Elimu ya Mpiga Kura kutuma maombi ya kupata kibali cha kutoa Elimu hiyo ili kuhakikisha kila Mtanzania anapata Elimu ya Mpiga Kura. 
 
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Emmanuel Kawishe wakati akitoa Elimu ya Mpiga Kura kwenye kipindi cha Kumekucha cha Televisheni ya ITV jijini Dar es Salaam leo.
 
Alisema kwa kuanzia asasi hizo zitapewa muda wa miezi sita kupima mafanikio ya kutoa Elimu hiyo na kwamba NEC itatoa kibali kwa asasi ambayo imetimiza vigezo vya kutoa Elimu ya Mpiga Kura nchini.
 
Bw. Kawishe alitaja vigezo hivyo kuwa ni asasi iwe imesajiliwa Tanzania, imefanya kazi ya kutoa Elimu si chini ya miezi sita, iwasilishe majina ya viongozi wake, iwe inaweza kujigharamia na iwasilishe anuani yake.
 
Aliongeza vigezo vingine kuwa ni kama ni asasi ya nje inayofanya kazi pamoja na Tanzania, kati ya viongozi wake wakuu watatu wawili wawe ni Watanzania na isiwe na historia ya kuchochea machafuko ama ndani ya Tanzania au nje ya Tanzania.
 
“Katika kupata uhakika wa taarifa hizi, sisi Tume ya Taifa ya Uchaguzi hatuna taarifa za kutosha kuhusiana na hizo asasi, kwa hiyo tunashirikiana na Jeshi la Polisi na Msajili wa Asasi tutawaomba taarifa za asasi hizo ili kujiridhisha” alisema Bw. Kawishe.
 
Alifafanua kuwa NEC inahitaji kuzifahamu asasi zinazotoa Elimu ya Mpiga Kura ili kujihakikishia zinatekeleze lengo ambalo tume hiyo inataka litekelezwe ambalo ni kutoa Elimu ya Mpiga Kura  kwa wananchi katika maeneo wanayotaka kuitoa.
 
“Kwa hiyo hizi asasi tutazialika, tutatoa tangazo kuanza na kumalizika kwa kipindi na kuna watendaji ambao wameandaliwa rasmi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi watakaokuwa wanaratibu asasi hizo, watakapoleta maombi yao watayapitia na kuona je yanakidhi vigezo” alifafanua Bw. Kawishe.
 
Alisema katika maombi yao asasi za kiraia zitaombwa kuainisha maeneo ambayo wanataka kwenda kutoa Elimu hiyo lakini NEC itazisii kwenda kutoa Elimu hiyo maeneo ya pembezoni ili kuifikisha Elimu ya Mpiga Kura katika maeneo hayo.
 
Bw. Kawishe alisema NEC imeamua kutoa Elimu hiyo endelevu kwa kuwa tathmini imeonesha kuwa Elimu hiyo haitolewi kama inavyotakiwa kiasi cha kuwafanya wananchi wengi kutofahamu majukumu ya Tume na kutumia kadi ya kupigia kura kama utambulisho kwenye taasisi za mikopo badala ya kupigia kura.
 
Mkurugenzi huyo wa Huduma za Sheria wa NEC aliwataka Watanzania kuifuatilia Tume kwenye mikutano ambayo itashiriki kutoa Elimu hiyo, kupitia kwenye vyombo vya Habari au kuingia kwenye Tovuti ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ili kupata Elimu ya Mpiga Kura.
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi inatekeleza mkakati wa kutoa Elimu ya Mpga Kura nchini ambapo imeshiriki kwenye Maonesho ya Sabasaba na Nanenane, ilishiriki Mkutano wa Mwaka wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT), Wiki ya Vijana kitaifa mkoani Simiyu na kutoa Elimu kwenye shule za Sekondari nchini.



 
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: NEC KUZIALIKA ASASI ZA KIRAIA KUTOA ELIMU YA MPIGA KURA KWA KILA MTANZANIA
NEC KUZIALIKA ASASI ZA KIRAIA KUTOA ELIMU YA MPIGA KURA KWA KILA MTANZANIA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJJJuZgYC9GMUKmMf8DpDvXODY-Rr16UdNMbTZlCPSSIEQ9j8yrSeBdtqcOQmvXpjzI-nA4nLlSjJUCYAKt0ga2g9whbEmRz_rirP5U143TwGGcHU8qzljoO6nwYHT3MC1_MAtZF3mEzA/s640/13BE9073-7F6E-452E-AD3D-90A998626E7D_cx0_cy4_cw0_mw1024_s_n_r1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJJJuZgYC9GMUKmMf8DpDvXODY-Rr16UdNMbTZlCPSSIEQ9j8yrSeBdtqcOQmvXpjzI-nA4nLlSjJUCYAKt0ga2g9whbEmRz_rirP5U143TwGGcHU8qzljoO6nwYHT3MC1_MAtZF3mEzA/s72-c/13BE9073-7F6E-452E-AD3D-90A998626E7D_cx0_cy4_cw0_mw1024_s_n_r1.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/11/nec-kuzialika-asasi-za-kiraia-kutoa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/11/nec-kuzialika-asasi-za-kiraia-kutoa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy