· Nacte yafuta leseni ya vyuo vya ufundi 26 · 20 vyasimamishiwa programu zisizosajiliwa na baraza hilo · ...
·
Nacte yafuta leseni ya vyuo vya ufundi
26
·
20 vyasimamishiwa programu zisizosajiliwa na baraza hilo
·
2 vyasimamishwa kwa kutokuwa na usajili
Baraza
la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) limevifungia vyuo vya ufundi 26
kutokana na makosa mbalimbali, ikiwamo kushindwa kuzingatia masharti
yaliyowekwa na kutoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Kaimu Katibu mtendaji wa
NACTE, Dkt.Adolf Rutayuga, alisema kuwa wamekuwa
wakifuatilia
vyuo vya ufundi ili kutathmini kama vinafuata viwango vya ubora wa
kitaaluma vilivyowekwa na NACTE katika kutoa mafunzo.
“Kama
ilivyoelezwa katika sheria za Usajili na Kanuni za leseni, kutozingatia
matakwa yoyoye yaliyowekwa na NACTE ni kosa kisheria. Kanuni zinasema
kuwa hatua kali zinawezakuchukuliwa kwa kila kosa. Kulingana na matokeo
ya ufuatiliaji uliofanywa na timu maalumu, Baraza lina uwezo wa
kuchukua hatua dhidi ya taasisi au vyuo vinavyoshindwa kutekeleza kanuni
zilizowekwa,” alisema.
Alisema
kuwa baada ya kufanya utafiti wao, wamebaini vyuo 26 vilishindwa
kuzingatia masharti yaliyowekwa na NACTE katika
cheti cha usajili, huku vyuo 20 vikitoa mafunzo ambayo
hayajathibitishwa chini ya idara isiyotambulika,wakati vyuo viwili
vikiwa na vituo vya satellite/Kampasi ambavyo navyo havijathibitishwa na
chombo husika.
“Baraza
linaufahamisha umma kwamba limechukua hatua mbalimbali kwa vyuo vya
ufundi 48 kutokana na makosa mbalimbali, yaliyofanywa na vyuo hivyo
ambapo limesitisha vyeti vilivyotolewa kwa vyuo 20 ambavyo vimeshindwa
kuzingatia masharti yaliyowekwa kwenye Cheti cha Usajili.
“Uamuzi huu umefanywa kwa mujibu wa Kanuni ya 20 ya Usajili wa Vyuo vya Ufundi ya mwaka 2001,” alisema.
Rutayuga
alisema kwamba vyuo vilivyofutiwa usajili kutokana na kosa la kutoa
mafunzo ambayo hayajathibitishwa chini ya idara
isiyotambulika ni 26.“Vyuo vya ufundi vinatakiwa kupata kwa idhini ya
Baraza kabla ya kuanza kutoa mafunzo yoyote. Idhini hiyo inahusu
uthibitisho
wa mtaala kwa ajili mafunzo yaliyokusudiwa na utambuzi wa idara
iliyopangwa kutoa mafunzo hayo,” alisema.
Juu ya vyuo vyenye vituo vya setelite, kampasi, Dkt.Adolf Rutayuga
alisema kuwa Baraza linahitaji mafunzo kutolewa katika vituo
vilivyosajiliwa/kampasi za vyuo vikuu baada ya kuthibitishwa kwamba
vinastahili kutoa mafunzo.
“Hata hivyo, taasisi mbili zimebainika kutoa mafunzo katika vituo vya satellite/vyuo vikuu ambavyo havijasajiliwa na Baraza
na hivyo kuadhibiwa. Vyuo hivyo navyo vimefutiwa leseni,” alisema Rutayuga.
NACTE
ni bodi iliyoanzishwa kisheria chini ya Sheria ya Baraza la Taifa la
Elimu ya Ufundi, kifungu cha 129, kusimamia na kuratibu utoaji wa elimu
ya ufundi na mafunzo nchini Tanzania. Chini ya sheria hiyo, ili
kufikia na kudumisha hali ya mtoa mafunzo, vyuo vyote vinatakiwa viwe
vimesajiliwa, vibali na kuwa mitaala iliyopitishwa na baraza. Vyuo
haviruhusiwi kuanza kutoa kuanza kutoa huduma yoyote ya
mafunzo bila idhini ya baraza.
Jedwali 1: Vyuo vya Ufundi vilivyofutiwa usajili
S/N
|
CHUO
|
1
|
Institute of Management and Development Studies – Iringa
|
2
|
Green Hill Institute – Mbeya
|
3
|
Institute of Business and Social Studies – Mbeya
|
4
|
Loyal College of Africa – Mbeya
|
5
|
Mbeya Training College – Mbeya
|
6
|
Mbengwenya College of Business and Information Technology –Mbinga
|
7
|
New Focus College – Mbeya
|
8
|
Shukrani International College of Business and Administration – Mbeya
|
9
|
Majority Teachers College – Mbeya
|
10
|
Rukwa College of Health Sciences – Sumbawanga
|
11
|
MAM Institute of Education – Mbeya
|
12
|
Belvedere Business and Technology College – Mwanza
|
13
|
Geita Medical Laboratory Sciences and Nursing Training College – Geita
|
14
|
Global Community College – Geita
|
15
|
Muleba Academy Institute – Muleba
|
16
|
St. Bernard Health Training Institute – Katoro, Geita
|
17
|
Victoria Institute of Tourism and Hotel Management – Mwanza
|
18
|
Gisan Institute of Health Sciences – Mwanza
|
19
|
Dar es Salaam Institute of Business Management – Dar es Salaam
|
20
|
SAMFELIS College of Business Studies – Dar es Salaam
|
21
|
Ellys Institute of Technology – Bunda, Mara
|
22
|
Tanzania Institute of Chartered Secretaries and Administrators – Arusha
|
23
|
Emmanuel Community College – Kibaha
|
24
|
Modern Commercial Institute – Dar es Salaam
|
25
|
Marian College of Law – Dar es Salaam
|
Jedwali 2: Vyuo vya Ufundi vinavyotoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa
S/N
|
CHUO
|
MAFUNZO
|
1
|
MISO Teachers College – Mafinga
|
Competence Building Network (CBN) - a Certificate in Early Childhood Education
|
2
|
Tusaale Teachers College - Mafinga
|
Competence Building Network (CBN) - a Certificate in Early Childhood Education
|
3
|
The St. Joseph’s College Institute of Business and Management (SJCIBM) – Morogoro
|
|
4
|
The Golden Training Institute – Dar es Salaam
|
|
|
||
|
||
|
||
|
||
|
||
5
|
Nkrumah Mkoka Teachers College – Kongwa, Dodoma
|
|
6
|
National Institute of Agriculture (Chuo cha Kilimo cha Taifa) – Arusha
|
|
7
|
Musoma Utalii Training College – Musoma
|
|
8
|
Mwanza Polytechnic Institute – Mwanza
|
|
9
|
Mwanza Polytechnic Institute – Maswa
|
|
10
|
Ruter Institute of Financial Management – Mwanza
|
|
11
|
Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Mwanza
|
|
12
|
Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Geita
|
|
13
|
Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Bukoba
|
|
14
|
Singni International Training Institute – Bukoba
|
|
15
|
Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Kahama
|
|
16
|
Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Simiyu
|
|
17
|
Richrise Teachers College – Geita
|
|
18
|
Twiga Training Institute – Musoma
|
|
19
|
Zoom Polytechnic Institute – Bukoba
|
|
20
|
St. Thomas Training College – Shinyanga
|
|
Jedwali 3: Vyuo vya Ufundi vyenye Vituo vya Satellite / Kampasi
S/N
|
CHUO
|
1
|
MISO Teachers College – Mafinga
|
2
|
Rungemba Teachers College – Mafinga
|
COMMENTS