MKE WA RAIS MAMA JANETH  ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI  ALIPOKUWA AMELAZWA
HomeJamii

MKE WA RAIS MAMA JANETH ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI ALIPOKUWA AMELAZWA

 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa anatoka kwenye    Wodi ya Sewahaji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kureje...



 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa anatoka kwenye  Wodi ya Sewahaji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kurejea nyumbani  mara baada ya kuruhusiwa baada ya kupata nafuu. Mama Janeth Magufuli alikuwa amelazwa hospitalini hapo tangu tarehe 9 Novemba 2016. 
 
 
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimshukuru Dkt. Raymond Mwenesano, Mkuu wa Idara ya Wagonjwa wa nje na Daktari Bingwa wa magonjwa ya ndani katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili mara baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini hapo na kurejea nyumbani baada ya kupata nafuu.
 
 
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimshukuru Dkt. Edward Ngwalle, mara baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini hapo na kurejea nyumbani baada ya kupata nafuu.
 
 
 
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimshukuru Dkt. Benard Kepha ambaye Daktari Bingwa wa Magonjwa ya dharura na ajali katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili mara baada ya kuruhusiwa kutoka na kurejea nyumbani mara baada ya kupata nafuu. (Picha na IKULU)
 
 

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli aliyekuwa amelazwa katika wodi ya Sewahaji ya Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam ameruhusiwa na kurejea nyumbani leo tarehe 11 Novemba, 2016 baada ya afya yake kuimarika.
Kabla ya kuondoka katika wodi ya Sewahaji alikokuwa amelazwa Mama Janeth Magufuli amewashukuru Madaktari na Wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu mazuri aliyoyapata na pia amewashukuru Watanzania wote kwa kumuombea afya njema.
"Namshukuru sana Mungu kwamba afya yangu imeimarika, pia napenda kuwashukuru Madaktari na Wauguzi, nimepata huduma nzuri sana maana siku nilipoletwa hapa nilikuwa sina fahamu na hali yangu ilikuwa mbaya lakini mmenipigania na leo narudi nyumbani nikiwa na afya imara.
"Naomba pia niwashukuru Watanzania wote kwa kuniombea, nawahakikishie kuwa sasa nipo vizuri na madaktari wameniruhusu nirudi nyumbani ambako nitamalizia matibabu yangu" amesema Mama Janeth Magufuli. 
Mama Janeth Magufuli alilazwa hospitalini hapo tangu Juzi tarehe 09 Novemba, 2016 baada ya kuugua ghafla na kupoteza fahamu.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
11 Novemba, 2016
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MKE WA RAIS MAMA JANETH ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI ALIPOKUWA AMELAZWA
MKE WA RAIS MAMA JANETH ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI ALIPOKUWA AMELAZWA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg9fUQ_S4X6PtVFGRzT5IGLmE0ETR-XpQwPE_CGT3LHucGGxdiqGOGF-SDi7foTHhTQKW0AHgsGLE2LmNmvC4xciLoabqrKCkQS-GowtAj25z20at_5dxmhYHM5bLsJMqzEIqMPuK9buxg/s640/2.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg9fUQ_S4X6PtVFGRzT5IGLmE0ETR-XpQwPE_CGT3LHucGGxdiqGOGF-SDi7foTHhTQKW0AHgsGLE2LmNmvC4xciLoabqrKCkQS-GowtAj25z20at_5dxmhYHM5bLsJMqzEIqMPuK9buxg/s72-c/2.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/11/mke-wa-rais-mama-janeth-aruhusiwa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/11/mke-wa-rais-mama-janeth-aruhusiwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy