MAJALIWA ATEMBELEA CHANZO CHA MAJI CHA MZAKWE DODOMA, ATAKA ORODHA YA WADAIWA SUGU DUWASA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mitambo ya maji ya DUWASA inayotoa maji yanayosambazwa katika Manispaa ya Dodo...









Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mitambo ya maji ya DUWASA inayotoa maji yanayosambazwa katika Manispaa ya Dodoma wakati alipotembelea chanzo cha maji cha Mzakwe Dodoma Oktoba 2, 2016.
 
 
 
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mitambo ya maji ya DUWASA inayotoa maji yanayosambazwa katika Manispaa ya Dodoma wakati alipotembelea chanzo cha maji cha Mzakwe Dodoma Oktoba 2, 2016.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 


*Ni wa taasisi za umma, wanadaiwa sh. bilioni 1.4

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza apatiwe orodha ya wadaiwa sugu wa taasisi zote za Serikali mkoani Dodoma ambao wamelimbikiza deni la sh. bilioni 1.4 zikiwa ni bili zao za maji.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumapili, Oktoba 2, 2016) wakati akizungumza na watumishi na viongozi wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dodoma (DUWASA) mara baada ya kukagua utendaji kazi wa chanzo cha maji cha Mzakwe nje kidogo ya mji wa Dodoma.

“Niletee haraka orodha ya wadaiwa wote wa Ofisi za Serikali na taasisi za umma ambao hawajalipa bili zao. Madeni yote ni lazima yalipwe,” amesema Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu ambaye yuko katika ziara ya siku mbili ya kukagua maandalizi ya Serikali kuhamia Dodoma, anatembelea sehemu mbalimbali za kutolea huduma za jamii pamoja na kukagua miundombinu ya mkoa huo.

Aliutaka uongozi wa DUWASA na watumishi wote wahakakishe wanaboresha huduma za upatikanaji wa maji hasa kwenye maeneo yanayopimwa viwanja ili wananchi au wawekezaji wanaponunua viwanja wakute huduma hiyo ipo na waanze ujenzi mara moja.

“Tumealika wawekezaji, nataka wajenge viwanda na mahoteli hapa Dodoma, sasa wakikuta maji na umeme kwenye maeneo yao, itakuwa ni kichocheo cha kuharakisha kazi za ujenzi,” amesema.

Pia amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Bi. Christina Mndeme ahakikishe eneo lililo jirani na chanzo hicho cha maji halikaliwi na mtu yeyote na linalindwa dhidi ya uchomaji mioto.

“Uchomaji moto uoto wa asili umeharibu vyanzo vingi vya maji. Ni tatizo kubwa hapa nchini na halina budi kusimamiwa hadi liishe,” amesisistiza.

Amefikia uamuzi huo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa DUWASA, Mhandisi David Pallangyo kwamba kuna wananchi wameanza kujenga na kufanya shughuli za kijamii jirani na chanzo hicho licha ya kuwa walikwishaondolewa zamani.

Kuhusu wadaiwa sugu, Mhandisi Pallangyo alisema mashirika ya umma na taasisi za Serikali ndiyo wanaongoza kwa kulimbikiza madeni. “Wananchi wa kawaida wapo wanaodaiwa lakini deni lao siyo kubwa na hao tunawamudu,” alisema wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi.

Alisema changamoto nyingine inayowakabili ni uchomaji moto ambapo hivi karibuni uliwashwa moto na kuunguza baadhi ya nguzo za umeme ambazo zinapeleka umeme kwenye chanzo hicho.

Alisema askari wa JKT Makutupora walisaidia kuzima moto huo ili usifike kwenye mitambo mingine ya chanzo hicho cha maji.

Waziri Mkuu pia alikagua maabara ya upimaji maji kwenye chanzo hicho kabla hayajasambazwa kwa wateja na mara yanapokuwa yamefika kwa wateja na kuelezwa kuwa maji hayo yanakidhi viwango vya kitaifa na vya kimataifa vilivyowekwa na Shirika la Afya Duniani (WHO).

Waziri Mkuu anaendelea na ziara yake kwa kutembelea kiwanda cha magodoro Dodoma na kituo cha kuzalisha umeme cha Zuzu.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
S. L. P. 980,
DODOMA.
JUMAPILI, OKTOBA 2, 2016

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAJALIWA ATEMBELEA CHANZO CHA MAJI CHA MZAKWE DODOMA, ATAKA ORODHA YA WADAIWA SUGU DUWASA
MAJALIWA ATEMBELEA CHANZO CHA MAJI CHA MZAKWE DODOMA, ATAKA ORODHA YA WADAIWA SUGU DUWASA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEirL0Lbwg53ZyxfIH5uL24nfNL9idThVjv9uL3HOt14Td_seXQS8PQTOGFWeqVRoMJCXmZByXTtfy5s2GWVTgIRo6ghD0rRdHoK0LOpIpI2M5XgTBwh-Jt0xeLN6Qs9ylP63UXjf1_ySvPF/s640/ADEN+1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEirL0Lbwg53ZyxfIH5uL24nfNL9idThVjv9uL3HOt14Td_seXQS8PQTOGFWeqVRoMJCXmZByXTtfy5s2GWVTgIRo6ghD0rRdHoK0LOpIpI2M5XgTBwh-Jt0xeLN6Qs9ylP63UXjf1_ySvPF/s72-c/ADEN+1.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/10/majaliwa-atembelea-chanzo-cha-maji-cha.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/10/majaliwa-atembelea-chanzo-cha-maji-cha.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy