KIWANDA KIKUBWA CHA MBOLEA KUJENGWA MTWARA
HomeMikoaniSlide

KIWANDA KIKUBWA CHA MBOLEA KUJENGWA MTWARA

Kiwanda kikubwa cha mbolea kujengwa Mtwara. Eneo la hekta 400 latengwa Na Greyson Mwase, Mtwara. Serikali kwa kushirikiana na kamp...


Kiwanda kikubwa cha mbolea kujengwa Mtwara.
Eneo la hekta 400 latengwa
Na Greyson Mwase, Mtwara.
Serikali kwa kushirikiana na kampuni ya Helm  kutoka Ujerumani inatarajia kujenga kiwanda kikubwa cha mbolea katika eneo la  Msanga Mkuu mkoani Mtwara.
Hayo yalielezwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa katika nyakati  tofauti katika ziara ya siku  tatu mkoani Mtwara ya kutembelea maeneo ambayo gesi inazalishwa na kujiridhisha iwapo itatosha katika uendeshaji wa kiwanda kikubwa cha mbolea kinachotarajiwa kujengwa.
Profesa Ntalikwa alisema kuwa kutokana na ugunduzi wa gesi nyingi mkoani Mtwara  wawekezaji wengi wameanza kuonesha nia ya kuwekeza katika mkoa  huo hususan katika uanzishwaji wa viwanda vya mbolea na saruji.
Alisema kiwanda cha mbolea kinachotarajiwa kujengwa, kitahitaji gesi kiasi cha futi za ujazo trilioni 0.8 kwa kipindi cha miaka 20 na kusisitiza kuwa serikali  imejipanga katika kuhakikisha  kuwa gesi ya kutosha inazalishwa ili kuendana na mahitaji ya kiwanda hicho pamoja na matumizi mengine ya majumbani.
Akielezea uwezo wa kampuni zilizopo Mtwara katika uzalishaji wa gesi ya kutosha, Profesa Ntwalikwa alifafanua kuwa, kampuni ya Ndovu Resources Limited iliyopo katika eneo la  Ntorya ipo katika programu ya kuchimba visima ambapo imeshachimba kisima kimoja ambacho kimeweza kutoa kiasi cha futi za ujazo trilioni  0.15
Aliongeza kuwa kampuni hiyo ina mpango wa kuchimba kisima cha pili ambacho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha gesi kiasi cha futi za ujazo trilioni 0.9 na kisima cha tatu kitakachokuwa na uwezo wa kuzalisha gesi kiasi cha futi za ujazo trilioni 1.5 na kuongeza kuwa kisima cha pili kinatarajiwa kukamilika mapema Machi, 2017 na cha tatu mwezi Juni, 2017.
Aliongeza kuwa kampuni nyingine ya Maurel & Prom yenye visima vitano imesema kuwa ipo tayari wakati wowote kuchimba visima vya ziada vya kuzalisha gesi ili kuongeza wingi wa gesi itakayohitajika katika viwanda mbalimbali ambapo kwa sasa wanazalisha gesi nyingi hali inayopelekea nyingine kukosa soko.
Akielezea maandalizi ya ujenzi wa kiwanda hicho,  Profesa Ntalikwa alisema kuwa Serikali  imetenga eneo la Msanga Mkuu lililopo Mtwara lenye ukubwa wa hekta 400 kwa ajili ya  ujenzi wa kiwanda hicho.
Aliongeza kuwa eneo hili limeshalipiwa fidia pamoja na halmashauri ya Mtwara kuboresha miundombinu  ya barabara kwa kuweka lami kutoka Mtwara Mjini hadi eneo la kiwanda tayari kwa kukabidhiwa kwa mwekezaji kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda.




KATIBU MKUU WA WIZARA YA NISHATI NA MADINI PROFESA  JUSTIN NTALIKWA AANZA ZIARA MTWARA
Picha Na 1
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa  (kulia) akisalimiana na Afisa Rasilimaliwatu kutoka Shirika la  Umeme Nchini (TANESCO)- Tanga, Samia Suleman (kushoto) mara baada ya kuwasili kwenye ofisi zake mkoani Mtwara. Profesa Ntalikwa  yupo  katika ziara ya siku  tatu katika  mkoa  wa Mtwara  yenye lengo la kukagua  shughuli za sekta za nishati na madini.
Picha Na 2
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa akisaini kitabu cha wageni mara baada ya  kuwasili katika kituo cha kuzalisha  umeme cha Mtwara.
Picha Na 3
Kituo cha  kuzalisha umeme mkoani Mtwara kama kinavyoonekana pichani.

Picha Na 4
Meneja wa kituo cha kuzalisha umeme cha Mtwara, Mhandisi Mkulungwa Chinumba (kulia) akitoa maelezo juu ya uendeshaji wa kituo hicho kwa Katibu Mkuu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa (kushoto)

Picha Na 5
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa  (katikati mbele) pamoja na  wataalam kutoka  Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Shirika la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC) akiendelea na  ziara katika kituo cha kuzalisha umeme cha Mtwara.
Picha Na 6
Meneja wa kituo cha kuzalisha umeme cha Mtwara, Mhandisi Mkulungwa Chinumba (kushoto) akielezea mitambo ya kuzalisha  umeme inavyofanya kazi katika kituo hicho.
Picha Na 7
Msimamizi wa mradi wa ujenzi wa kituo cha kupooza  umeme cha Mtwara, Mhandisi Amon Gamba (kushoto) akielezea maendeleo ya  ujenzi wa kituo hicho kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa ( wa pili kushoto)
Picha Na 8
Kamishna Msaidizi wa Madini- Kanda ya Kusini, Mhandisi Benjamin Mchwampaka (kushoto) akiwasilisha  taarifa ya maendeleo ya sekta ya madini katika kanda hivyo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa (kulia) mara Profesa Ntalikwa alipofanya ziara katika kituo hicho.
Picha Na 9
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa (kushoto) akisalimiana na Meneja Uendeshaji wa Mnazi Bay,  David Chaudronnier (kulia) mara baada ya kuwasili katika kituo hicho.
Picha Na 10
Msimamizi wa shughuli za uzalishaji kutoka Mnazi Bay, Kilemo Nyomwa akielezea mikakati ya uzalishaji wa gesi ya kutosha katika kituo hicho ili kuendana na kasi ya  ukuaji wa viwanda katika mkoa wa Mtwara.
Picha Na 11
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa (mwenye suti nyeusi) pamoja na wageni wengine,  akiendelea na ziara katika kituo cha Mnazi Bay mkoani Mtwara.

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: KIWANDA KIKUBWA CHA MBOLEA KUJENGWA MTWARA
KIWANDA KIKUBWA CHA MBOLEA KUJENGWA MTWARA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh4LFnYdkp4xdMHJrZSioWYYMD9HhvPSNI6QXiYu38zwXg1O4eO5iizCMKbUPC_vu6RRbJakmR_SMZxTpHjsOsSSWxUmk3m-PPE4d2pmBiTgaP91p9QfQ4fi__BXzAjG5WOctqL53jkVt8/s640/mtwara_supply_base.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh4LFnYdkp4xdMHJrZSioWYYMD9HhvPSNI6QXiYu38zwXg1O4eO5iizCMKbUPC_vu6RRbJakmR_SMZxTpHjsOsSSWxUmk3m-PPE4d2pmBiTgaP91p9QfQ4fi__BXzAjG5WOctqL53jkVt8/s72-c/mtwara_supply_base.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/10/kiwanda-kikubwa-cha-mbolea-kujengwa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/10/kiwanda-kikubwa-cha-mbolea-kujengwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy