Mshindi wa mwezi wa Disemba, 2015 ni Ibrahim Ajib ambapo amepata kura nyingi zaidi zilizopigwa na mashabiki na wapenzi wa Simba na sok...
Mshindi wa mwezi wa Disemba, 2015 ni Ibrahim Ajib ambapo amepata kura nyingi zaidi zilizopigwa na mashabiki na wapenzi wa Simba na soka wa Tanzania kwa ujumla kupitia simu za mkononi ambao pia wamejiunga na huduma ya Simba News.
Katika
kuongeza morali na kuwazawadia wachezaji wanaofanya vizuri, Klabu ya Simba
ilianzisha Tunzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi kuanzia mwezi wa Septemba 2015.
|
Akimakabidhi
tunzo hiyo Mkuu wa kitengo cha biashara na mipango kutoka EAG Group Richard
Mvula alisema “kama mtakumbuka utaratibu huu ulianzishwa kwa ajili ya kuwapa
motisha wachezaji wetu na sasa umekuwa ni utamaduni wetu katika kuwapongeza na
kuonesha kuthamini jitihada zinazofanywa na wachezaji wetu katika kuutafuta
ushindi wa msimu huu”
Napenda
kuwakumbusha wanachama na wapenzi wa Simba kuendelea kuwapa sapoti wachezaji
wetu kwani kwa sapoti yao ndio mafanikio ya timu yetu yanapopatikana, aliongeza
Mkuu wa kitengo cha biashara na mipango kutoka EAG Group Richard Mvula
Akizungumza
jinsi tunzo ya mchezaji bora itakavyoendeshwa, Mkurugenzi Mkuu wa EAG Group,
Imani Kajula alisema “Wanachama na wapenzi wa Simba na wapenda michezo ndio
watakao kuwa wanachagua mchezaji bora wa mwezi kwa kutuma jina la mchezaji wanayempendekeza
kwenda kwenye namba 15460, Ni wale tu ambao wamejiunga na Simba News kupitia
mtandao wa Voda na Tigo wataweza kupiga kura kuchagua mchezaji bora wa mwezi wa
Simba”.
Tukumbuke
kuwa unaweza kumchagua mchezaji bora wa mwezi ukiwa umejiunganisha na huduma ya
Simba News kwa kutuma jina la mchezaji kwenda namba 15460. Zoezi la kumchagua
mchezaji bora wa mwezi wa Januari, 2016 litaanza February 29
2016. Piga kura mara nyingi zaidi kuweza kumpata mchezaji wako bora wa
Mwezi Januari, 2016.
Simba News
ni huduma iliyoanzishwa na Simba ili kuwapa wapenzi wa Simba habari mbalimbali
za Simba popote pale walipo ikiwemo matokeo, majina ya wachezaji wanaocheza
mechi, usajili na habari nyingine za klabu ya Simba. Kujiunga na Simba News
tuma neno Simba kwenda namba 15460 ni maalum kwa Tigo na Vodacom.
COMMENTS