KAMANDA KOVA AMUANIKA KINARA WA WIZI WA MABENKI, PAMOJA NA SILAHA, MENO YA TEMBO NA TUKIO ZIMA LA WIZI BENKI YA BARCLAYS TAWI LA KINONDONI DAR

KAMANDA KOVA AMUANIKA KINARA WA WIZI WA MABENKI, SILAHA, MEN O YA TEMBO NA WIZI BENKI YA BARCLAYS TAWI LA KINONDONI DSM. Kamanda wa ...

KAMANDA KOVA AMUANIKA KINARA WA WIZI WA MABENKI, SILAHA, MENO YA TEMBO NA WIZI BENKI YA BARCLAYS TAWI LA KINONDONI DSM.


Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Suleiman Kova akionesha picha ya kinara anayetuhumiwa kufanya wizi katika mabenki anajulikana kwa jina la RONALD S/O MOLLEL umri miaka 37, mfanyabishara na mkazi wa Kimara Bonyokwa Jijini Dar es Salaam.

 

Baadhi ya mali za wizi zaanikwa.

Baadhi ya mali za wizi zaanikwa.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Suleiman Kova akiongea na waandishi wa habari.


Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Suleiman Kova akionesha meno ya tembo yaliyokamatwa.

Kamanda Suleiman Kova akionesha moja ya magari yalikamtwa kwa makosa ya uhalifu. 





JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA



PRESS RELEASE
14/05/2014

POLISI WAMGUNDUA KINARA WA MTANDAO WA WIZI  KATIKA MABENKI JIJINI D’SALAAM (PICHA YAKE YATOLEWA HADHARANI) ANATAFUTWA NA JESHI LA POLISI
Jeshi la Polisi Kanda Maalum D’Salaam limefanikiwa kumbaini mtuhumiwa mhimu ambaye ni kinara wa mtandao wa wizi katika mabenki ambaye anajulikana kwa jina la RONALD S/O MOLLEL umri miaka 37, mfanyabishara na mkazi wa Kimara Bonyokwa Jijini D’salaam.

Mtuhumiwa huyu amekimbilia mafichoni mara baada ya tukio la ujambazi katika Tawi la Benki ya Barclays  Kinondoni lililotokea tarehe 15/4/2014 ambapo majambazi walifanikiwa kupora kiasi kikubwa cha fedha T.Shs.390,220,000/= , USD 55,000/= na EURO 2150/=.  Aidha sasa imefahamika kwamba mtuhumiwa huyu ni mume wa mtuhumiwa wa kwanza katika tukio la Barclays Benki aitwaye ALUNE D/O KASILILIKA @ ALUNE D/O MOLLEL , miaka 28,  Mkazi wa Kimara Bonyokwa ambaye ni Meneja wa Benki Tawi la Barclays Kinondoni.  Mtuhumiwa Mollel anatafutwa kwa kila hali kwa vile yeye ndiye alikuwa kinara wa kupanga tukio hilo la Barclays na mara baada ya tukio ametoroka na kiasi kikubwa cha fedha hizo zilizoibiwa.

Zipo taarifa za kuaminika kuwa mtuhumiwa huyu amekuwa akipanga na kushiriki kikamilifu katika matukio mbali mbali ya uhalifu mkubwa ikiwa ni pamoja na kuongoza vikundi vya majambazi vilivyowahi kupora katika mabenki mbali mbali katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.  Mtuhumiwa huyo ni hatari kwani ana mtandao na watumishi muhimu katika matawi mbali mbali ya mabenki kwa lengo la kufanikisha uhalifu katika mabenki hayo.

Jeshi la Polisi limelazimika kutoa picha yake hadharani kwa kutumia dhana ya ulinzi shirikishi ili mtuhumiwa huyu akionekana akamatwe na taarifa zitolewe katika kituo chochote cha Polisi ikiwa ni lengo la polisi kupambana na uhalifu katika dhamira ya kuzuia uhalifu, kulinda maisha na mali za wananchi.  Zawadi nono ya fedha taslim itatolewa kwa siri kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa zitakazosaidia kukamatwa kwa mtuhumiwa huyu.  Pamoja na maelezo hayo mtuhumiwa mwenyewe sasa anapewa fulsa ya kujisalimisha katika kituo chochote cha polisi kabla ya kukamatwa kwa njia nyingine.



 
Kinara anayetuhumiwa kufanya wizi katika mabenki anajulikana kwa jina la RONALD S/O MOLLEL umri miaka 37, mfanyabishara na mkazi wa Kimara Bonyokwa.
MAJAMBAZI WATATU WAKAMATWA NA SILAHA 2 NA SARE ZA JESHI.  

Jeshi la Polisi Kanda Maalum D’Salaam mnamo tarehe 13/05/2014 limefanikiwa kuwakamata majambazi watatu wakiwa na silaha mbili aina ya Shot gun na risasi 12, Redio Call 1 na sare za Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ). Mafanikio haya yametokana na msako mkali unaoendelea jijini D’Salaam.  Majina ya majambazi hayo ni kama ifuatavyo:-

1.    Isi-Hakka s/o Salehe

2.    Alex s/o Andrew

3.    Odinga s/o Swalehe

Majambazi hao walikamatwa maeneo ya Chamazi katika Mkoa wa Kipolisi Temeke baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi.  Jambazi mmoja alikamatwa ndani ya gari aina ya Hiace (daladala) na wengine wawili ndani ya nyumba baada ya jambazi wa kwanza kuelekeza wenzake walipo.  Polisi walifanya upekuzi katika nyumba hiyo na kufanikiwa kupata vitu hivyo.  Uchunguzi bado unaendelea na watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.



POLISI JIJINI DAR ES SALAAM WAFUMUA MTANDAO WA MAKOSA YA UVUNJAJI KWA KUKAMATA MAJAMBAZI SUGU 15 NA VITU MBALIMBALI.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum kwa kutumia kikosi maalum cha Kiintelijensia (special intelligence task force) limefanikiwa kuufumua mtandao unaojihusisha na ujambazi jijini Dar es Salaam ikiwemo kuhusika na uvunjaji na kisha kupora mali mbalimbali zikiwemo nyumba za ibada.

Katika oparesheni hiyo iliyoanza tarehe 29/04/2014, wamekamatwa majambazi sugu wawili ambao baada ya kuhojiwa waliwataja wenzao wengine kumi na tatu (13) wanaoshirikiana nao katika matukio ya ujambazi na kufanya idadi yao kufikia kumi na tano.

Watuhumiwa waliokamatwa na kutaja mtandao mzima ni SHABAN S/O MAFURU, Miaka 36, Mkazi wa Magomeni na ABDALLAH S/O HUSSEIN, Miaka 52, Mkazi wa Tabata Mawenzi, ambao wote walikutwa kwenye gari namba T259 ADB, T/RAV rangi ya Silver wakiwa wamepakia vitu mbalimbali vya wizi kama ifuatavyo:

·         Moving Camera - 4.

·         Stand mbili za Moving Camera.

·         Desk-top computer – 2

·         Deki mbili za DVD.

Inasemekana mali hizi walizokutwa nazo watuhumiwa hawa ziliibwa katika ofisi za ISLAM INTERNATIONA LTD zilizopo maeneo ya mabibo jijini Dar es Salaam.

Baada ya kukamatwa kwa watuhumiwa hao kumi na tano walihojiwa na kukiri kuhusika katika matukio kadhaa ya uvunjaji na uporaji kama ifuatavyo:

·         Tukio la tarehe 01/05/2014 maeneo ya REGENT ESTATE katika ofisi za NAIRO ambapo walivunja na kuiba viyoyozi (Air Condition) 120 na vitu vingine.



·         Tarehe 22/04/2014 huko maeneo ya Mwenge katika duka SAMSUNG, walivunja na kuiba TV Set zipatazo nane (8) na simu za mkononi mbalimbali.



·         Tarehe 17/04/2014 maeneo ya MASAKI walivunja Supermarket iitwayo SHIREJEES na kupora fedha TSh. 19,000,000/= (Millioni kumi na tisa), Monitor mbili za Computer, LCD TV Set mbili, na pombe kali za aina mbalimbali.



·         Pia wamekiri kuvunja Makanisa mawili moja ni lile la K.K.K.T Usharika wa Magomeni na kupora pesa taslim Tsh. 8,000,000/=. Kanisa lingine walilokiri kuvunja ni lile la AICT ambapo walipora Tsh 500,000/=, Desk-top Computer mbili aina ya DELL, Laptop mbili aina ya DELL, na Projctor moja aina ya Sony.



·         Wamekiri kuhusika katika uvunjaji kwenye ofisi za Shule ya Sekondari ya LOYOLA iliyoko Mabibo na kuiba DOLLA ZA KIMAREKANI zipatazo 8000 na Shillingi za Kitanzania 9,000,000/=

Watuhumiwa wengine waliokamatwa wanaounda mtandao huu ni kama ifuatavyo:
·         FLORIAN S/O PHILOMON @ K.K, Miaka 35, Mkazi wa Manzese.
·         MATOKE S/O MAGERE, Miaka 30, Mkazi wa Kigogo Kintinku.
·         RASHID S/O MUSSA @ GAIDI, Miaka 42, Mkazi wa Kariakoo Mchikichini.
·         ATHUMAN S/O SALEHE @ KIDINYU, Miaka 30, Mkazi wa Magomeni Makuti.
·         AZIZI  S/O SAID FADARI, Miaka 38, Mkazi wa Kiwalani Minazi Mirefu
·         IBRAHIMU S/O KINGU, Miaka 50, Mkazi wa Temeke Mikoroshini.
·         THOMAS S/O KIMAMBI, Miaka 33, Mkazi wa Ubungo External.
·         JOSEPH S/O JOSEPH THOMAS, Miaka 32, Mkazi wa Kimara Stop Over.
·         STEPHANO S/O SAMWEL @ LIKONGO, Miaka 37, Mkazi wa Mburahati Mianzini.
·         NICKO S/O NUSULUPIA HAULE @ NICK BUTY, Miaka 31, Mkazi wa Mburahati Mianzini.
·         KUDRA S/O MOHAMED, Miaka 30, Mkazi wa Ubungo.
·         HAMISI S/O SALUM SALEHE, Miaka 31, Mkazi wa Kimara Rombo.
·         MOHAMED S/O RASHID, Miaka 30, Mkazi wa Kimara Rombo.

WATUHUMIWA 2 WAKAMATWA NA MENO 25 YA KIBOKO NA  1 AKAMATWWA NA VIPANDE 8 VYA MENO YA TEMBO AMBAVYO NI NYARA ZA SERIKALI
Jeshi la Polisi Kanda Maalum limefanikiwa kukamata vipande zaidi ya ishirini (20) vinavyodhaniwa kuwa ni meno ya Tembo vilivyokuwa vimehifadhiwa nadni ya mfuko maarufu kwa jina la kiroba. Tukio hili lilitokea tarehe 30/04/2014 katika kiwanda cha Nondo Steel Master kilichopo eneo la Mbozi Road (W) kipolisi Chang’ombe (M) kipolisi Temeke baada ya Polisi kupokea taarifa kuwa katika kiwanda hicho kuna mfuko wa kiroba wenye bidhaa hiyo umefichwa.
Baada ya taarifa hizo askari kikosi cha Upelelezi walifika kiwandani hapo na kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Kiwanda hicho aitwaye HITESH S/O PATEL walifanya upekuzi. Katika upekuzi huo polisi walifanikiwa kukamata vipande 25 vya meno yadhaniwayo kuwa ni ya KIBOKO vikiwa vimehifadhiwa ndani ya mfuko wa kiroba ukiwa umefichwa kwenye Roll ambayo ni Malighafi maalum ya kutengenezea nondo. Kwa mujibu wa taarifa ya maafisa wa wanyamapori ni kwamba kwa idadi ya vipande hivyo 25 ni sawa na VIBOKO 6 waliouawa ambapo meno ya Kiboko mmoja yana thamani ya Dolla za Kimarekani 1500 sawa na Shilingi za Kitanzania zaidi ya (Millioni Mbili Laki Nne na Sabini na Tano) Tshs.2,475,000. Hivyo kwa idadi ya VOBOKO sita thamani yake ni sawa na shilingi za kitanzania THS; 14,850,000/= (million kumi na nne, mia nane na hamsini elfu tu).
Katika tukio hilo, polisi inawashikilia watu wawili ambao ni RASHID S/O ABDALLAH, Miaka 19, mwingine ni HEMED S/O JUMA @ KASIMU, Miaka 25.   Washitakiwa hao watafikishwa mahakamani kujibu shitaka linalowakabili pindi upelelezi utakapokamilika.
Aidha katika tukio lingine mnamo tarehe 5/5/2014 huko maeneo ya Tabata Kisiwani karibu na uwanja wa Twiga Mkoa wa Kipolisi Ilala, Polisi wamefanikiwa kumkamata MUSA S/O LUCAS KIFARU akiwa naa vipande 8 vya meno ya tembo vyenye uzito wa kilogram 13.5 ambavyo thamani yake T.Shs.49,500,000/= vikiwa vimehifadhiwa kwenye begi lenye rangi ya blue na nyeusi.  Mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa .
TAARIFA ZA UKAMATAJI WA MAKOSA KITENGO CHA USALAMA BARABARANI KANDA MAALUM KUANZIA 01/05/2014 HADI SASA.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani liliendesha oparesheni kamambe kukamata makosa yanayohusisha uvunjaji wa sheria mbalimbali za usalama barabarani ili kuhakikisha watumiaji wote wa barabara wanazingatia sheria hizo. Makosa hayo ni pamoja na haya yafuatayo:
·         Ubovu wa Magari,
·         Obstraction,
·         Kuzidisha Abiria,
·         T.L.A,
·         Kukatisha Route,
·         Uendeshaji wa hatari,
·         Kutotii Amri,
·         Matumizi mabaya ya barabara,
·         Kutokuwa na Leseni, nk.
Aidha katika oparesheni hiyo vyombo mbalimbali vya usafiri yakiwemo Magari, Pikipiki, Bajaji na vingine vilikamatwa na kutozwa tozo kulingana na makosa kwa kila chombo kama ifuatavyo:
MGAWANYO WA MAKOSA NGAZI YA KI-MIKOA
JUMLA YA MAKOSA - ILALA
JUMLA YA MAKOSA  TEMEKE
JUMLA YA MAKOSA  KINONDONI
JUMLA KUU
3066
2399
4630
10095

MGAWANYO WA TOZO NGAZI YA KI-MIKOA
JUMLA YA TOZO
ILALA
JUMLA YA TOZO  TEMEKE
JUMLA YA TOZO KINONDONI
JUMLA KUU
Tshs 82,200,000/=
65,850,000/=
125,580,000/=
273,630,000/=

Aidha, taarifa ya Kikosi cha Usalama barabarani Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam ya ukamataji wa makosa ya Usalama Barabarani kwa kipindi cha kuanzia Mwezi Januari 2014 ni kama ifuatavyo:
1.    Idadi ya magari yaliyokamatwa -          64,785
2.    Idadi ya pikipiki zilizokamatwa   -          17,082
3.    Jumla ya Makosa yaliyokamatwa  -      84,474
4.    Fedha za TOZO zilizopatikana     Tsh: 2,534,220,000/=

S.H. KOVA
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAAM

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: KAMANDA KOVA AMUANIKA KINARA WA WIZI WA MABENKI, PAMOJA NA SILAHA, MENO YA TEMBO NA TUKIO ZIMA LA WIZI BENKI YA BARCLAYS TAWI LA KINONDONI DAR
KAMANDA KOVA AMUANIKA KINARA WA WIZI WA MABENKI, PAMOJA NA SILAHA, MENO YA TEMBO NA TUKIO ZIMA LA WIZI BENKI YA BARCLAYS TAWI LA KINONDONI DAR
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhnNr5v5Jns5C2Dr20VUu7y5QPfcszmIjNTUiccqF9gTLo_-wbPSAqIN08W7g0yo986Wbw2ptK5s8ymz9YistnVIPhtvMbjG5n-9cNE-hpGJPl9EmXRSLvNZbDsrTI9Bjchy2Ypy5Uj0RI/s1600/IMG_0966.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhnNr5v5Jns5C2Dr20VUu7y5QPfcszmIjNTUiccqF9gTLo_-wbPSAqIN08W7g0yo986Wbw2ptK5s8ymz9YistnVIPhtvMbjG5n-9cNE-hpGJPl9EmXRSLvNZbDsrTI9Bjchy2Ypy5Uj0RI/s72-c/IMG_0966.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2014/05/kamanda-kova-amuanika-kinara-wa-wizi-wa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2014/05/kamanda-kova-amuanika-kinara-wa-wizi-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy