VODACOM YASOGEZA HUDUMA ZAKE KWA WATEJA WAKE

Ofisa Mkuu  wa Idara ya Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh, akiteta jambo na mmliki wa duka la Vodacom, Ricky Renson,...

Ofisa Mkuu  wa Idara ya Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh, akiteta jambo na mmliki wa duka la Vodacom, Ricky Renson,  lililoko Mzambarauni ,Gongo la Mboto, Jijini Dar es Salaam, Baada ya uzinduzi wa Duka hilo ambalo litatoa huduma kwa wakazi wa eneo hilo na maeneo ya jirani. Katikati ni Mke wa Mmiliki wa duka hilo, Beatrice Renson.
Ofisa Mkuu  wa Idara ya Mauzo na Usambazaji wa Vodacom, Hassan Saleh, akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani, wakati wa uzinduzi wa duka jipya la Vodacom lililoko Mzambarauni , Gongolamboto, jijini Dar es Salaam, Duka hilo litatoa huduma kwa wakazi wa eneo hilo na maeneo ya jirani.
Mmiliki wa duka jipya la Vodacom lililopo Mzambarauni , Gongolamboto Dar es Salaam, Ricky Renson, akizungumza na waandishi wa habari, hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa duka hilo. Duka hilo litatoa huduma kwa wakazi wa eneo hilo na maeneo ya jirani. Katika ni mke wa mmiliki wa duka hilo, Beatrice Renson na Mkuu wa kitengo cha Mauzo wa Vodacom Tanzania, Upendo Richard.

Ofisa mkuu  wa Idara ya Mauzo na usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh (wa kwanza kushoto) pamoja na Mkuu wa kitengo cha Mauzo wa kampuni hiyo  Upendo Richard na Mmiliki wa duka jipya la Vodacom lililoko Mzambarauni , Gongolamboto Dar es Salaam, Beatrice Renson  , wakifurahia mara baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi wa duka hilo.
Ofisa mkuu  wa Idara ya Mauzo na usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh, akimkabidhi funguo Mmiliki wa duka jipya la Vodacom lililopo Mzambarauni, Gongolamboto, Ricky Renson, mara baada ya uzinduzi rasmi wa duka hilo linalofikisha idadi ya maduka 67 yanayotoa huduma kwa wateja  nchini. Katika ni Mkuu wa kitengo cha Mauzo wa kampuni hiyo  Upendo Richard na Mke wa Mmiliki wa duka hilo, Beatrice Renson.
Mmiliki wa duka jipya la Vodacom liliko Mzambarauni, Gongolamboto jijini Dar es Salaam Bi. Beatrice Renson akifungua mlango kuashiria kuanza kwa huduma katika duka hilo mara baada ya uzinduzi huo. Katika ni Ofisa mkuu  wa Idara ya Mauzo na usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh, na Mkuu wa kitengo cha Mauzo wa kampuni hiyo  Upendo Richard.
Mfanyakazi wa duka jipya la Vodacom lililoko Mzambarauni, Gongolamboto Dar es Salaam, John Kimwaga (Wa kwanza kushoto), akimuunganishia intaneti mmoja wa wateja aliyefika kupata huduma katika duka hilo, Venant Mlokozi. Anayeshuhudia ni  Ofisa mkuu  wa Idara ya Mauzo na usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh.
Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania, Elihuruma Ngowi na Upendo Happiness Macha wakifungua shampeni kuashiria uzinduzi wa duka jipya la Vodacom lililoko Mzambarauni, Gongolamboto.



Vodacom continues to bring services closer to customers
·        Opens 67th shop at Gongo la Mboto
Dar es Salaam, 23rd August, 2013 … Vodacom Tanzania continued to bring customer care services to its customers in a move aimed at giving efficient and effective services across the country.
Today, the Vodacom has opened its 67th customer care shop at Gongo la Mboto, Dar es Salaam, and this makes it the telecommunications company with the highest number of shops in the market.
Speaking during the launch of the shop, Vodacom Tanzania Chief Officer Sales and Distribution, Hassan Saleh, said that the company will continue opening as many shops as possible in order to reduce congestion in the already existing shops. Some of the company's shops in Dar es Salaam are situated at, among others, Mlimani City Mall, Ohio Street, RDK Victoria, Samora Avenue, and Ali Hassan Mwinyi Road.
The services to be offered in the new shop, Saleh, include Internet activation, device sales and configuration, M-Pesa and after sales support.
"Our customer base has experience a tremendous growth, and we are therefore looking for ways of bringing services closer to the people so as to avoid congestion and wastage of time," said Saleh, adding that, "The opening of this outlet will not only help in main services available, but it is also an employment opportunity for Tanzanians."
So far, according to Saleh, Vodacom has given direct employment to over 500 individuals and over 30,000 Tanzanians indirectly. Plans are also underway to open shops at Kimara, Msimbazi, and Kigogo.





Vodacom yasogeza zaidi huduma kwa wateja
Agosti 23, 2013 …KATIKA kukidhi haja ya utoaji wa huduma kwa wateja nchini, Kampuni ya Vodacom Tanzania imeendelea kupanua wigo wa huduma zake kwa kufungua duka jipya (Vodashop) katika eneo la Gongo lamboto jijini Dar es Salaam.
Ufunguzi wa duka hilo ni katika harakati za kuendelea kusogeza huduma za mawasiliano karibu na wateja na kufanya mauzo ya bidhaa mbalimbali za mtandao huo kuwa karibu zaidi ikiwemo huduma za kutuma na kupokea fedha (M-PESA), Intaneti, sambamba na vifurushi mbalimbali.

Akizungumzia wakati wa uzinduzi wa maduka hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Rene Meza, alisema Vodacom ni kampuni pekee ambayo imeendelea kuongoza kwa kuwa na maduka mengi ya mauzo na huduma kwa wateja kwa kufikisha maduka 67 kwa jijini Dar es Salaam huku ikitarajia kufungua maduka mengine zaidi.
Aliongeza kuwa ili kufanikisha azma ya kukidhi mahitaji ya huduma kwa wateja wa kampuni hiyo --Vodacom Tanzania imeamua kuongeza idadi ya maduka yake jijini Dar es Salaam kufikia 24 kutokana na mahitaji makubwa zaidi.
"Ukuaji wa huduma kwa kampuni ya Vodacom umekuwa mkubwa sana, huduma kama ya M – Pesa sasa imepanuka kwa kasi ambapo kwa sasa kampuni yetu inatoa huduma kwa watanzania zaidi ya milioni 20. Hivyo, kufuatia mafanikio haya tunalazimika kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya uhakika kwa wateja wetu," alisema Bw. Meza, na kuongeza kuwa, "Kuongoza katika sekta ya mawasilaino kuna changamoto zake,hivyo ni lazima tuhakikishe tunaendana na kasi ya ukuaji wa huduma zetu ili kuendana na ongezeko la watu wa aina mbalimbali."

Aidha Bw. Meza alisema kuwa kufunguliwa kwa duka hilo hivi sasa si tu kunaboresha upatikanaji wa huduma bali ni fursa pekee ya kuendelea kupanua wigo wa ajira kwa watanzania.
"Ufunguzi wa duka hili unatoa fursa ya ajira kwa Watanzania. Halikadhalika ufunguzi huu umejumuisha  ajira kwa wafanyakazi zaidi ya 10 ambao watatoa huduma kwa wateja wetu hivyo ni hatua kubwa tumetengeneza ajira kwa wafanyakazi wapya. Hadi kufikia sasa, Vodacom imetoa ajira za moja kwa moja kwa wafanyakazi 500 na wengine zaidi ya 30,000 wenye ajira zisizo za moja kwa moja," alisema.
Kufuatia uzinduzi wa duka hilo la huduma za mawasiliano ya simu maeneo ya Gongolamboto, Kampuni ya Vodacom iko mbioni kufungua maduka mengine katika maeneo ya Kimara, Kigogo, na Msimbazi hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
Upanuzi huu wa wigo wa huduma za mawasiliano ya simu wa Kampuni ya Vodacom Tanzania unafuatia uwekezaji kwenye mfumo wa mawasiliano wa 3G na 4G mfumo ambao unaotumia teknolojia mpya ya mawasiliano kazi iliyofanywa na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania.


COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: VODACOM YASOGEZA HUDUMA ZAKE KWA WATEJA WAKE
VODACOM YASOGEZA HUDUMA ZAKE KWA WATEJA WAKE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjmBbRlZEbu_4fg0T1ipKSnYJzdD2M2gPRX6n4CWVD4hV_Ay5XJ-Rc4zKQW128Zk5cBP6Pn6l4b6CkJIvks1k4ZIgAY0b6KKh6wfdBaQy6cvb_PVaUrKxvtl0RhTZPYhFJqf8509yhMs_ju/s640/001+GONGOLAMBOTO-742306.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjmBbRlZEbu_4fg0T1ipKSnYJzdD2M2gPRX6n4CWVD4hV_Ay5XJ-Rc4zKQW128Zk5cBP6Pn6l4b6CkJIvks1k4ZIgAY0b6KKh6wfdBaQy6cvb_PVaUrKxvtl0RhTZPYhFJqf8509yhMs_ju/s72-c/001+GONGOLAMBOTO-742306.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2013/08/vodacom-yasogeza-huduma-zake-kwa-wateja.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2013/08/vodacom-yasogeza-huduma-zake-kwa-wateja.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy