Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amewasili mkoani Kilimanjaro na kupokelewa na Mkuu wa Mk...
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amewasili mkoani Kilimanjaro na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira pamoja na Viongozi wengine wa Chama na Serikali.
Makamu wa Rais anatazamiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani ambayo Kitaifa yanafanyika mkoani Kilimanjaro kesho Oktoba 16, 2017.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni " Zuia Ajali-Tii Sheria Okoa Maisha"
Ufunguzi huo utafanyika katika Uwanja wa Mashujaa uliopo katika Manispaa ya mji wa Moshi.
COMMENTS