Umma unaarifiwa kuwa Serikali imefanya jitihada za kuwatafuta na hatimaye kuwapata ndugu wa marehemu Mzee Francis Maige Kanyasu ...
Umma
unaarifiwa kuwa Serikali imefanya jitihada za kuwatafuta na hatimaye
kuwapata ndugu wa marehemu Mzee Francis Maige Kanyasu (86) anayetajwa
kuwa mmoja wa wachoraji wa nembo ya Taifa. Mzee Kanyasu alifariki dunia
usiku wa tarehe 29 Mei, 2017 saa mbili na nusu katika Hospitali ya Taifa
Muhimbili.
Mwili
wa marehemu utaagwa rasmi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kuanzia
saa mbili na nusu asubuhi Jumamosi ya tarehe 3 Juni, 2017 na mara baada
ya kuagwa mwili marehemu atasafirishwa na Serikali kwenda kijijini kwao
Igokero, Wilaya ya Misungwi kwa ajili ya mazishi.
Taarifa zaidi kuhusu mazishi ya Mzee Kanyasu zitaendelea kutolewa kwa umma kadiri inapobidi.
Imetolewa na:
Bi. Sihaba S. Nkinga
KATIBU MKUU
Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
(MAENDELEO YA JAMII)
COMMENTS