Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 21 Juni, 2017 amefuturisha wananchi wa mkoa wa Pwani ...
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 21 Juni, 2017 amefuturisha wananchi wa mkoa wa Pwani na kuwataka
waumini wa dini ya Kiislam na madhehebu mengine kuendeleza umoja na
mshikano uliopo kwa muda mrefu kwa lengo la kudumisha amani nchini.
Mhe.
Rais Magufuli amesema anaungana na waumini wa dini ya Kiislamu nchini
katika kumi la mwisho la Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa kuwaombea
kumaliza kwa amani ibada ya Funga ya Ramadhani ikiwa ni kutekeleza nguzo
ya nne kati ya nguzo tano ya dini ya kiislam.
Amesema
kwa mujibu wa dini ya Kiislamu ibada ya Funga ya Mwezi Mtukufu wa
Ramadhani ni muhimu kwani ni njia sahihi ya kujirekebisha kuachana na
matendo maovu yanayoweza kusababisha kutenda dhambi.
‘’Ramadhani
ni ibada muhimu kwa Waislaam kwani ndio mwezi ambao huchoma dhambi zao
na kutenda matendo mema hivyo ni muhimu kwa ndugu Waislaam kuendeleza
yote mema ambayo wanafanya katika kipindi hiki cha mwezi wa Ramadhani
ikiwa ni pamoja na kuliombea Taifa.’’
Kwa
upande wake Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti Aboubakar Zubeir Ali ametaka
wananchi wa Tanzania bila kujali itikadi za kidini kuendelea kuliombea
Taifa ili lizidi kuendelea kuwa na amani.
Nae
Kaimu Sheikh wa mkoa wa Pwani Sheikh Hamisi Mtupa amemshukuru Rais
Magufuli kwa ukarimu wake wa kuwaaandalia futari wananchi wa mkoa wa
Pwani ikiwa ni pamoja na makundi maalum ya watoto yatima wa kituo cha
Bulome Foundation cha mjini Kibaha mkoani Pwani.
Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Kibaha, Pwani
Rais
wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa katika
foleni ya kunawa na kisha kuchukua chakula leo Jumatano Juni 21, 2017
katika futari aliyowaandalia wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu
ndogo ya Kibaha ambayo ilihudhuriwa pia na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh
Aboubakar Zubeir Ali pamoja na viongozi wengine wa dini, serikali,
vyama na watoto wanaolelewa kwenye vituo mbalimbali vya yatima mkoani
humo.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuli (wa pili
kulia) akichukua chakula leo Jumatano Juni 21, 2017 katika futali
aliyowaandalia wananchi wa mkoa wa Pwani futari katika Ikulu ndogo ya
Kibaha ambayo ilihudhuriwa pia na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh
Aboubakar Zubeir Ali pamoja na viongozi wengine wa dini, serikali, vyama
na watoto wanaolelewa kwenye vituo mbalimbali vya yatima mkoani humo.
Kina
mama wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kibaya Mhe. Asumpta Mshama
wakichukua chakula wakati wa futari iliyoandaliwa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa wananchi wa mkoa wa
Pwani katika Ikulu ndogo ya Kibaha
Rais
wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitoa neno
la shukrani leo Jumatano Juni 21, 2017 wa waliohudhuria futari
aliyowaandalia wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu ndogo ya Kibaha.
Mufti
Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Ali akizungumza machache na
kuomba dua baada ya futari iliyoandaliwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli
kwa wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu ndogo ya Kibaha.
Sehemu
ya waalikwa wakiitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh
Aboubakar Zubeir Ali baada ya futari iliyoandaliwa na Rais Dkt John
Pombe Magufuli kwa wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu ndogo ya
Kibaha.
COMMENTS