Mbunge wa Kawe (CHADEMA), Mhe. Halima Mdee na Mbunge wa Bunda mjini (CHADEMA), Mhe. Esther Bulaya wameadhibiwa kutohudhu...
Mbunge
wa Kawe (CHADEMA), Mhe. Halima Mdee na Mbunge wa Bunda mjini (CHADEMA),
Mhe. Esther Bulaya wameadhibiwa kutohudhuria vikao vyote vya bunge
linaloendelea mpaka
mkutano ujao wa Bunge la Bajeti 2018/19.
Hukumu hiyo imeungwa mkono na wabunge wengi waliopitisha azimio hilo mapema
leo Jumatatu Juni 5, 2017 Kamati ya Maadili ilisema Bulaya na Mdee
wamemaliza adhabu za kawaida zilizopo kwenye kanuni za bunge. Hata hivyo, Bunge liliendelea kujadili makosa ya wabunge hao wa Bunda na Kawe.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, George Mkuchika aliliomba Bunge kujadili adhabu inayostahili kulingana na makosa yao.
Kanuni inasema, mbunge anayefanya kosa la kwanza anaweza
akazuiwa kuhudhuria vikao visivyozidi 10 na atayakosea kwa mara ya pili
anaweza kuzuiwa kuhudhuria vikao visivyozidi 20.
COMMENTS