WAZIRI wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Tizeba amewataka viongozi wa miradi ya kilimo inayofadhiliwa na serikalipamoja na ...
WAZIRI
wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Tizeba amewataka viongozi wa
miradi ya kilimo inayofadhiliwa na serikalipamoja na mashirika ya
misaada kuzingatia malengo ya kuanzishwa miradi hiyo ili kuongeza
uzalishaji wa chakula nchini.
Akizungumza
katika skimu ya umwagiliaji ya Dakawa mkoani Morogoro hivi karibuni
Dkt. Tizeba alisema wakulima hawana sababu ya kuwa na hiyari kwani fedha
zinazotolewa ni nyingi na wahisani pamoja na serikali wanataka kuona
matokeo ya misaada hiyo.
“Naomba
unisikilize ndugu mwenyekiti, waliopewa pesa kwa ajili ya kilimo wasiwe
na hiyari ya kulima, hatuwezi kuendelea kusikia tu wenzetu wanavuna
tani nyingi katika mataifa mengine ikiwa sisi bado tunaendelea hivi
hivi,” alisema Dkt. Tizeba na kusisitiza:“Anayetaka kukaa hapa kwenye skimu akae kwa kufuata masharti na asiyetaka aondoke apishe wengine.
USAID
(Shirika la misaada la watu wa Marekani) kiasi walichotoa kinafikia Sh
bilioni 29, tukizigawa kila mmoja anapata Sh milioni 60. Naombeni make
halafu mkubaliane kuwa suala la kufanya kilimo cha hiyari katika maeneo
tuliyofadhili hatutaki kusikia. Msimu ujao tunataka tuvune tani 12
katika skimu hii.”
Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Mbegu za Kilimo, Dkt. Filimini Mizambwa amesema ili
taasisi zinazosaidia wakulima ziendelee kuwepo lazima wakulima hasa
wadogo waonyeshe tija katika shughuli wanazofanya ikiwemo kuonyesha
matokeo mazuri wakati wa mavuno.
“Ili
sisi tuendelee kuwepo lazima wakulima hasa mkulima mdogo fanikiwe, wito
wangu wakulima wajifunze kilimo chenye tija na kufanya kazi kwa juhudi
ili kuwaonyesha wafadhili fedha zao hazipotei bure kwa uzembe.
“Kazi
yetu ni kuhakikisha wakulima wanapata mbegu bora na kuongeza tija katika
uzalishaji mazao, tunafanya kazi na sekta binafsi na sekta za umma,
majukumu yetu ni kuongeza uzalishaji mbegu bora,” alisema Dkt. Mizambwa.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Kuendeleza Kilimo Kusini
mwa Tanzania (SAGCOT), Bwana Geoffrey Kirenga alisema malengo ya ziara
hiyo katika skimu ya umwagiliaji ya wakulima wadogo Mkondo na skimukubwa
ya Dakawa yenye ukubwa wa Hekta 2000 inalenga kuangalia shughuli
zinazofanyika na kuangalia changamoto zilizopo.
“Huu
ni mfano mzuri wa utekelezaji wa dhana ya SAGCOT, ambayo ni ubia kati ya
sekta binafsi na sekta ya umma. Katika ziara hii kuna watu wa serikali
na sekta binafsi, wakulima ni sehemu ya sekta binafsi,” alisema na
kuongeza:
“Nawashauri
wakulima wadogo wafuate kanuni bora za kilimo ili kuonyesha tija,
zamani suala hili ilikuwa ni utashi wa mkulima lakini kwa sasa si suala
la hiyari tena. Kama alivyosema Mheshimiwa Waziri wa Kilimo asiyetaka
atupishe ili tulete watu wengine.
Tumwekeza
fedha nyingi za walipa kodi na fedha za wahisani lengo ni kuona mkulima
anapata faida, ikiwa kinyume chake haitakuwa na maana hiki
tunachokifanya.”Ziara
hiyo ni sehemu ya maandalizi ya uzinduzi wa skimu hizo za umwagiliaji
mkoani Morogoro utakaofanywa hivi karibuni na Rais Dkt. John Magufuli.
Miongoni
mwa wafadhili wa shughuli za SAGCOT ni Serikali ya Tanzania, Ubalozi wa
Norway, USAID, UKAID, Benki ya Dunia, UNDP na AGRA.
COMMENTS