DKT. TIZEBA;WALIOSHINDWA KUTIMIZA MALENGO MIRADI YA KILIMO WATUPISHE

WAZIRI wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Tizeba amewataka viongozi wa miradi ya kilimo inayofadhiliwa na serikalipamoja na ...


WAZIRI wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Tizeba amewataka viongozi wa miradi ya kilimo inayofadhiliwa na serikalipamoja na mashirika ya misaada kuzingatia malengo ya kuanzishwa miradi hiyo ili kuongeza uzalishaji wa chakula nchini.
Akizungumza katika skimu ya umwagiliaji ya Dakawa mkoani Morogoro hivi karibuni Dkt. Tizeba alisema wakulima hawana sababu ya kuwa na hiyari kwani fedha zinazotolewa ni nyingi na wahisani pamoja na serikali wanataka kuona matokeo ya misaada hiyo.
“Naomba unisikilize ndugu mwenyekiti, waliopewa pesa kwa ajili ya kilimo wasiwe na hiyari ya kulima, hatuwezi kuendelea kusikia tu wenzetu wanavuna tani nyingi katika mataifa mengine ikiwa sisi bado tunaendelea hivi hivi,” alisema Dkt. Tizeba na kusisitiza:“Anayetaka kukaa hapa kwenye skimu akae kwa kufuata masharti na asiyetaka aondoke apishe wengine. 
USAID (Shirika la misaada la watu wa Marekani) kiasi walichotoa kinafikia Sh bilioni 29, tukizigawa kila mmoja anapata Sh milioni 60. Naombeni make halafu mkubaliane kuwa suala la kufanya kilimo cha hiyari katika maeneo tuliyofadhili hatutaki kusikia. Msimu ujao tunataka tuvune tani 12 katika skimu hii.”
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mbegu za Kilimo, Dkt. Filimini Mizambwa amesema ili taasisi zinazosaidia wakulima ziendelee kuwepo lazima wakulima hasa wadogo waonyeshe tija katika shughuli wanazofanya ikiwemo kuonyesha matokeo mazuri wakati wa mavuno.

“Ili sisi tuendelee kuwepo lazima wakulima hasa mkulima mdogo fanikiwe, wito wangu wakulima wajifunze kilimo chenye tija na kufanya kazi kwa juhudi ili kuwaonyesha wafadhili fedha zao hazipotei bure kwa uzembe.
“Kazi yetu ni kuhakikisha wakulima wanapata mbegu bora na kuongeza tija katika uzalishaji mazao, tunafanya kazi na sekta binafsi na sekta za umma, majukumu yetu ni kuongeza uzalishaji mbegu bora,” alisema Dkt. Mizambwa.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Kuendeleza Kilimo Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), Bwana Geoffrey Kirenga alisema malengo ya ziara hiyo katika skimu ya umwagiliaji ya wakulima wadogo Mkondo na skimukubwa ya Dakawa yenye ukubwa wa Hekta 2000 inalenga kuangalia shughuli zinazofanyika na kuangalia changamoto zilizopo.

“Huu ni mfano mzuri wa utekelezaji wa dhana ya SAGCOT, ambayo ni ubia kati ya sekta binafsi na sekta ya umma. Katika ziara hii kuna watu wa serikali na sekta binafsi, wakulima ni sehemu ya sekta binafsi,” alisema na kuongeza:
“Nawashauri wakulima wadogo wafuate kanuni bora za kilimo ili kuonyesha tija, zamani suala hili ilikuwa ni utashi wa mkulima lakini kwa sasa si suala la hiyari tena. Kama alivyosema Mheshimiwa Waziri wa Kilimo asiyetaka atupishe ili tulete watu wengine.

Tumwekeza fedha nyingi za walipa kodi na fedha za wahisani lengo ni kuona mkulima anapata faida, ikiwa kinyume chake haitakuwa na maana hiki tunachokifanya.”Ziara hiyo ni sehemu ya maandalizi ya uzinduzi wa skimu hizo za umwagiliaji mkoani Morogoro utakaofanywa hivi karibuni na Rais Dkt. John Magufuli.
Miongoni mwa wafadhili wa shughuli za SAGCOT ni Serikali ya Tanzania, Ubalozi wa Norway, USAID, UKAID, Benki ya Dunia, UNDP na AGRA.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: DKT. TIZEBA;WALIOSHINDWA KUTIMIZA MALENGO MIRADI YA KILIMO WATUPISHE
DKT. TIZEBA;WALIOSHINDWA KUTIMIZA MALENGO MIRADI YA KILIMO WATUPISHE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi3jQMy6PmclpmPG95f33GHqKTZn5Lw7tILiLKHAtBX5zeCeGCBpT-0x1kRQcPyBYmW5pa0YSrJOQIAJqXY8IMVlffhNPLVGkBXrd8ovE0zDy7nHJSSrippe0BlAwLzsbJjUAGsiWwnOXE/s400/Waziri-wa-Kilimo-Dr-Charles-Tizeba.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi3jQMy6PmclpmPG95f33GHqKTZn5Lw7tILiLKHAtBX5zeCeGCBpT-0x1kRQcPyBYmW5pa0YSrJOQIAJqXY8IMVlffhNPLVGkBXrd8ovE0zDy7nHJSSrippe0BlAwLzsbJjUAGsiWwnOXE/s72-c/Waziri-wa-Kilimo-Dr-Charles-Tizeba.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/dkt-tizebawalioshindwa-kutimiza-malengo.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/dkt-tizebawalioshindwa-kutimiza-malengo.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy