WARIDE: ASISITIZA UBUNIFU KWA WATENDAJI WA CCM NA SERIKALI.

NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR. KATIBU wa NEC,   Idara ya Itikadi na Uenezi   CCM Zanzibar,   Waride Bakari Jabu amewataka viongozi na wat...

NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

KATIBU wa NEC,  Idara ya Itikadi na Uenezi  CCM Zanzibar,  Waride Bakari Jabu amewataka viongozi na watumishi wa Chama na Serikali kubuni miradi na fursa zitakazosaidia kukuza kipato cha wananchi.

Alisema Viongozi Wakuu wa Kitaifa wamekuwa wakisisitiza suala la ubunifu kwa watumishi wa umma ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya watumishi hao kwa lengo la kukuza uchumi wa Taifa.

Kauli hiyo ameitoa  ofisini kwake Kisiwandui Mjini  Unguja, alieleza kwamba ajenda ya maendeleo ya nchi inamgusa kila mtu hasa watumishi waliopewa dhamana ndio wanaotakiwa kupanga mikakati ya kiuchumi kwa kuwahasisha wananchi watumie fursa zilizowazunguka zikiwemo ujasiriamali, kilimo, uvuvi na  ufugaji kujipatia kipato cha halali.

“Nchi yetu inapita katika kipindi kigumu cha kutoka katika uchumi wa Kati kwenda uchumi wa juu unaotegemea viwanda na masoko ya kimataifa ya ndani ya nchi, yote hayo yanahitaji ushirikiano wa kiutendaji miongoni mwetu.”, alisema Waride.

Pia alieleza kwamba wananchi wataendelea kuwa na imani na Chama cha Mapinduzi endapo serikali zote mbili zitaendelea kuwa  karibu na wananchi kwa kutatua kwa wakati kero na matatizo yanayowakabili.

Aidha alisema lengo la CCM ni kuendeleza utamaduni wa kuenzi demokrasia ndani na nje ya taasisi hiyo, sambamba na kuzishauri serikali zitekeleze sera za maendeleo kwa wananchi wote bila ubaguzi wa kisiasa na kidini.

Akizungumzia mipango ya chama hicho kwa sasa kuwa ni kufanikisha Uchaguzi wa ndani ya taasisi hiyo ambao kwa sasa unafanyika kwa ngazi za jumuiya na matawi yake ili kupata  viongozi na watendaji watakaotekeleza majukumu ya CCM kwa ufanisi ndani ya miaka mitano ijayo.

Katibu huyo alisema mpango mwingine ni kusimamia kwa nguvu zote utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama hicho, sambamba na kuandaa mazingira bora ya kisiasa yatakayosaidia wananchi kuichagua CCM kwa kura nyingi katika uchaguzi mkuu wa 2020.

Hata hivyo alimpongeza Mwenyekiti wa CCM Taifa, ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli kwa juhudi zake za kupambana na vitendo vya ubadhirifu wa rasilimali za Taifa.

Ni Katibu wa NEC,  Idara ya Itikadi na Uenezi  CCM Zanzibar,  Waride Bakari Jabu.   (PICHA YA MAKTABA YA AFISI KUU CCM-ZANZIBAR)


COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WARIDE: ASISITIZA UBUNIFU KWA WATENDAJI WA CCM NA SERIKALI.
WARIDE: ASISITIZA UBUNIFU KWA WATENDAJI WA CCM NA SERIKALI.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYI9VRTx70dqBKvlbMkH7rZ4qJBxgF0kZH429f8u4b_VBn8XOCNHeyT2m8IPgHMt7QmTN0J1kM2W4hUs6AkKzj43YtUuNrWWgagw0I69XHQl-k765mfZ_vzml9FKCJboOGRkjyC4fZwSo/s640/001%25283%2529.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYI9VRTx70dqBKvlbMkH7rZ4qJBxgF0kZH429f8u4b_VBn8XOCNHeyT2m8IPgHMt7QmTN0J1kM2W4hUs6AkKzj43YtUuNrWWgagw0I69XHQl-k765mfZ_vzml9FKCJboOGRkjyC4fZwSo/s72-c/001%25283%2529.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/waride-asisitiza-ubunifu-kwa-watendaji.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/waride-asisitiza-ubunifu-kwa-watendaji.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy