MAELFU YA AKINA MAMA WAENDELEA KUNUFAIKA NA HUDUMA YA WAZAZI NIPENDENI

Maelfu ya akina mama wanaendelea kunufaika na huduma ya ujumbe mfupi wa maandishi unaotolewa bure na Vodacom Tanzania Foundation wa ...



Maelfu ya akina mama wanaendelea kunufaika na huduma ya ujumbe mfupi wa maandishi unaotolewa bure na Vodacom Tanzania Foundation wa ‘Wazazi Nipendeni’, unazidi kuendelea kuwanufaisha maelfu ya akina mama wajawazito kupitia dondoo mbali mbali za kiafya.

 
Akiongea na mtandao huu Faidha Abdallah pichani ambaye ni mkazi wa Buguruni jijini Dar es Salaam anasema amekuwa akitumia huduma hiyo ambayo imekuwa msaada mkubwa kwake.

“Kupitia huduma hii ninaweza kujifunza namna ya uzazi salama kupitia simu yangu ya kiganjani bila malipo yoyote. Nimekuwa nikipokea ujumbe kila wiki na ninaishukuru  Vodacom Tanzania Foundation pamoja na wadau wengine waliofanikisha huduma hii nzuri,” anasema.

 “Pamoja na kuwa nimezaa na kukuza watoto wawili, sikufahamu kuwa kumbe ni muhimu sana kumnyonyesha mtoto kwa miezi sita bila kumkatisha kabla ya kuanza kumlisha aina nyingine ya chakula,” anaelezea

Naye Meneja Ruzuku na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Foundation, Sandra Oswald alisema jijini Dar es Salaam kuwa, zaidi ya wateja milioni moja wamejiunga na huduma hiyo tangu izinduliwe mwaka 2012.

“Wateja waliojiunga na huduma hii wamepokea jumla ya ujumbe mfupi unaofikia milioni 55 wenye maelekezo mbali mbali  juu ya afya bila malipo. Ujumbe wanaopokea ni pamoja na kubaini dalili hatari kwa uja uzito mapema, maendeleo ya mtoto, namna ya kuepuka maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa  mtoto, vyakula muhimu kwa mama mja mzito, uhuhimu wa  mama kuhudhuria kliniki mapema,” anaeleza
Oswald  anasema, kupitia ujumbe mfupi akina mama wajawazito wanaelimishwa namna ya kuishi wakiwa na afya ili waweze kujifungua watoto wenye afya bora pia watu wengine kama vijana, akina mama na wazee wanaweza kujifunza namna ya kujikinga na magonjwa mbali mbali kama Malaria na mengineyo.
Wateja wetu  wanaweza kupata   huduma hii ya bure kwa kutuma ujumbe kwenye namba 15001 au 15012 na wataweza kupokea ujumbe mfupi kupitia simu zao za viganjani.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAELFU YA AKINA MAMA WAENDELEA KUNUFAIKA NA HUDUMA YA WAZAZI NIPENDENI
MAELFU YA AKINA MAMA WAENDELEA KUNUFAIKA NA HUDUMA YA WAZAZI NIPENDENI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi8YEdP0l3u3gFUsg_CImFDEWuQ-ZHyRzP-RcUc-HgLgu1yA9Y0Ahtxw3phAgpzN2HZei9v3R__l4zqGmK1gITgoYzjyqM0v0Xdq_d4g9-Iybco-qDWFqUZ4CHQn4b4jUwqHC5g7ieN9sU/s640/IMG_4064.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi8YEdP0l3u3gFUsg_CImFDEWuQ-ZHyRzP-RcUc-HgLgu1yA9Y0Ahtxw3phAgpzN2HZei9v3R__l4zqGmK1gITgoYzjyqM0v0Xdq_d4g9-Iybco-qDWFqUZ4CHQn4b4jUwqHC5g7ieN9sU/s72-c/IMG_4064.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/maelfu-ya-akina-mama-waendelea.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/maelfu-ya-akina-mama-waendelea.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy