JUMIA TRAVEL YAZINDUA RIPOTI YA UTALII BARANI AFRIKA

Dar es Salaam, Mei 26, 2017. Kuzidi kuongezeka kwa watumiaji wa intaneti barani Afrika na kufikia zaidi ya milioni 300 ambayo kiuw...




Dar es Salaam, Mei 26, 2017. Kuzidi kuongezeka kwa watumiaji wa intaneti barani Afrika na kufikia zaidi ya milioni 300 ambayo kiuwiano kwa ueneaji wake ni sawa na 27.7% ni ishara nzuri kwa uchocheaji wa ukuaji wa shughuli za utalii kwa njia ya mtandao.



Hayo yalibainishwa kupitia ‘Ripoti ya Utalii Afrika kwa mwaka 2017’ iliyowasilishwa na Jumia Travel inayojihusisha na huduma za hoteli kwa njia ya mtandao, ambapo inaelezea kuwa teknolojia na huduma za simu zimeliingizia bara la Afrika mapato ya ndani kwa 6.7% kwa mwaka 2015 (ambazo ni sawa na dola za kimarekani bilioni 150 kwa thamani ya kiuchumi), na yanatarajiwa kuongezeka kwa zaidi ya dola za kimarekani bilioni 210 (7.6% ya jumla ya pato la ndani la taifa) kufikia mwaka 2020. 
Kaimu Meneja Mkuu wa Hoteli Hong Kong inayotumia huduma ya Jumia Travel akiongea na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati wa uzinduzi wa ripoti ya utalii Barani Afrika, ambapo idadi ya watumiaji wa huduma ya intaneti kwa Bara hili imefikia milioni 300 ambayo ya kiuwiano kwa ueneji wake ni sawa na asilimia 27.7 ikiashiria uchocheaji wa ukuaji wa shughuli za utalii kwa njia ya mtandao. Kulia ni Meneja Mkazi wa Jumia Travel Fatema Dharsee na Meneja Uhusiano wa Umma wa Kampuni hiyo Geofrey Kijanga.

Meneja Mkazi wa Jumia Travel Fatema Dharsee akifanya uwasilishaji wa ripoti ya utalii Barani Afrika, kwa wana habari Dar es Salaam leo, ambapo idadi ya watumiaji wa huduma ya intaneti kwa Bara hili imefikia milioni 300 ambayo ya kiuwiano kwa ueneji wake ni sawa na asilimia 27.7 ikiashiria uchocheaji wa ukuaji wa shughuli za utalii kwa njia ya mtandao. Kushoto ni  Meneja Uhusiano wa Umma wa Kampuni hiyo Geofrey Kijanga, Geofrey Kijanga.




Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kuiwasilisha ripoti hiyo, Meneja Mkaazi wa Jumia Travel nchini Tanzania, Bi. Fatema Dharsee amesisitiza kuwa takwimu hizo zinaifanya kampuni kuamini kuwa bara la Afrika lina fursa kubwa katika ukuaji wa sekta ya utalii kwa njia ya mtandao.



“Jumia Travel inaona kuwa ujio wa intaneti na kupokelewa vizuri na waafrika, ni ishara nzuri kwamba sekta ya utalii itakua ukizingatia ina mchango mkubwa kwenye kuchangia pato la taifa. Kwa mfano mpaka kufikia mwishoni wa mwaka 2015, 46% ya idadi ya waafrika (zaidi ya nusu bilioni ukilinganisha na idadi ya waafrika wanaofikia takribani bilioni 1.2) walijiunga na huduma za simu. Hii idadi ni ya kipekee kwani inatarajiwa kufikia milioni 725 mnamo mwaka 2020,” alisema Bi. Dharsee.



“Hayo yote kwa kiasi kikubwa yamechochewa na uapatikanaji wa mtandao wa intaneti wa 4G kwa zaidi ya nusu ya nchi za kiafrika, ambapo mpaka kufikia katikati ya mwaka 2016 takribani nchi 32 zilikuwa zimekwishaunganishwa na mitandao 72 ya LTE (Long-Term Evolution). Hata hivyo, bado tunajikongoja kwa namna tulivyopokea mabadiliko hayo ukilinganisha na sehemu zingine duniani ambapo ueneaji wake kwetu ni sawa na 20% ya idadi ya watu waliofikiwa na mtandao wa 4G,” aliongezea Menaja Mkaazi huyo wa Jumia Travel hapa Tanzania.



Aliendelea kwa kufafanua zaidi kuwa changamoto kubwa inayolikabili bara la Afrika kwa sasa hususani kusini mwa jangwa la Sahara ni ukosefu wa ujuzi kwenye masuala ya kigiditali. Hivyo basi wao wanaona kwamba kuunga mkono jitihada za utoaji elimu ya kidigitali kwa wadau wa utalii kuna umuhimu mkubwa katika kukuza sekta hiyo mtandaoni ndani ya bara la Afrika.



Mbali na uwasilishaji wa ripoti hiyo ya utalii barani Afrika pia kampuni hiyo imesema kuwa kwa sasa inaendesha kampeni inayolenga kuwakomboa waafrika kusafiri ndani na nje ya mipaka yao kwa gharama nafuu.



“Kampeni hii iliyopewa jina la ‘Democratize Travel’ dhumuni letu kubwa ni kuondoa mawazo yaliyojengeka miongoni mwetu haswa linapokuja suala la mchakato mzima kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Hii inamaanisha kupunguza gharama hususani za malazi, upatikanaji wa taarifa pamoja na kutoa huduma bora kwa kila mtu. Pia kupitia kampeni hii tunataka kuwaonyesha wateja wetu uzuri uliofichika kuhusu bara la Afrika kwa kuwapatia suluhu ya mahitaji yao yote pindi wanapotaka kusafiri kama vile; hatua au mambo ya kuzingatia, malazi, chakula na shughuli za kufanya mahali waendapo,” alisema Bi. Dharsee.



“Hatutoishia hapo bali tunataka pia kuondoa mitazamo tofauti ya kwamba sehemu za kutembelea zilizopo nchi za Magharibi kama vile Ulaya na Marekani au Dubai ni bora zaidi ya Afrika. Mbali na kuwarahisishia waafrika kusafiri kwenye maeneo waliyopo lakini pia tunawawezesha kuvuka mipaka kwenda sehemu nyingine duniani. Hapa msafiri ataweza kulipia gharama za kusafiri, kwa mfano kwenda jijini London nchini Uingereza, kwa fedha ya nchi yake anayotokea. Hayo yote yanawezekana na yamerahishwa kwani kupitia mtandao wetu mteja ataweza kukata tiketi ya ndege na kufanya huduma ya malazi kwa sehemu anayokwenda kwa wakati mmoja,” alihitimisha  Bi. Dharsee.



Kampuni hiyo imesema mbali na kuelekeza kampeni hiyo kwa wateja wake lakini pia itawashirikisha hoteli washirika katika kuhakikisha wanawafikia wateja na kukua kwa haraka zaidi. Hayo wanayahakikisha kupitia kuwatangaza mtandaoni ili kukuza muonekana na biashara zao, kuwapatia mifumo ya teknolojia inayoendana na soko la Afrika ili kuwarahishia uendeshaji wa biashara zao kama vile Extranet, SMS au barua pepe pamoja na kuchochea utoaji na uboreshaji wa huduma bora ili kuwavutia wateja wengi zaidi.



Akizungumzia namna Jumia Travel inavyorahisisha ufanyikaji wa shughuli za kila siku za hoteli, Kaimu Meneja Mkuu wa Hong Kong Hotel ya jijini Dar es Salaam, Bw. Mganja Suleiman amesema kuwa, “Kujiunga kufanya kazi na mtandao wa Jumia Travel kumetunufaisha kwa kiasi kikubwa sana ukilinganisha na hapo awali. Kwanza kabisa kujulikana na kutangazwa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania hivyo kutuongezea soko, kama mjuavyo shughuli za matangazo na kutafuta masoko zinahitaji mfanyabiashara au kampuni iwe na fedha ya kutosha. Lakini kupitia mtandao huu wateja wanaweza kujua huduma tulizonazo bila ya hata kuwasiliana nasi moja kwa moja kwani kila kitu kipo mtandaoni na pia kuacha maoni yao pale wanapovutiwa na namna walivyohudumiwa au kitu gani cha kuboresha.”



“Kwa kiasi kikubwa mtandao huu umekuwa ni chachu kwa hoteli yetu kufanya vizuri na kuendelea kuboresha huduma zetu kwa ubunifu zaidi ili kuweza kumudu suhindani wa kwenye soko. Pia ningependa kutoa pongezi kwa kutuletea teknolojia mpya na za kisasa kabisa ambazo zinarahisisha kazi zetu. Kwa mfano mfumo wao wa Extranet ambao umelenga kuwarahisishia mameneja au wa hoteli au wapokeaji wa maombi ya huduma kutoka kwa wateja kwa njia ya mtandao popote walipo. Mfumo huu unapatikana kwenye kompyuta, tabiti na simu pia, hivyo kupunguza lile adha ya kumlazimu meneja kutoa huduma mpaka awe hotelini. Lakini pia mfumo huu unatupatia sisi fursa ya kujua aina, idadi na hadhi ya wateja wanaotumia huduma zetu hivyo kurahisisha kuwafikia na kuwapatia kile wanachokitaka,” alihitimisha Bw. Suleiman.


Jumia Travel unveils 2017 Hospitality Report for Africa



Dar es Salaam, May 26, 2017. Increasing number of internet users across the African continent which reaches over 300 million, representing a penetration rate of 27%, shows a good sign regarding the growth of e-tourism.



That has been revealed through the 2017 Hospitality Report for Africa presented by Jumia Travel, Africa's No.1 hotel booking website. The report claims that mobile technologies and services generated 6.7% of GDP in Africa in 2015 (around USD 150 billion of economic value), and is expected to increase to more than USD 210 billion (7.6% of GDP) by 2020.



Speaking to the press while presenting the report, Jumia Travel Country Manager for Tanzania, Ms. Fatema Dharsee emphasized the company’s confidence in Africa’s potential for growth in terms of e-tourism.



“Jumia Travel sees the invasion of internet among Africans as an opportunity to the growth of various sectors including tourism, which plays a great role in the contribution of national GDP to most countries. For instance, by end of 2015, 46% of the African population (more than half a billion people) subscribed to mobile services. The number of unique subscribers is estimated to reach 725 million by 2020,“ said Ms. Dharsee.



“All those have been a result of the extension of the 4G network to more than half of the African countries, with 72 live LTE (Long-Term Evolution) networks in 32 countries by mid-2016. However, its adoption still lags behind the rest of the world with only 20% 4G population coverage,” added the Tanzania Country Manager .



She went further to explain that currently, the only challenge facing Africans especially in Sub-Saharan Africa is the low level of digital skills which slows the process to mobile internet adoption. As online travel agents, supporting digital literacy among tourism stakeholders in the continent is therefore an essential element in promoting e-tourism in Africa.   



Currently, apart from revealing the 2017 Hospitality Report for Africa to Tanzanians, Jumia Travel is running a campaign dubbed ‘Democratize Travel’ aimed to provide Africans freedom of travelling within and out of their destinations at affordable rates.        



“Our main focus is to break travel barriers including lowering costs especially for accommodation, access to information and better quality services to everyone. Also, through this campaign we want to showcase and expose the hidden beauty of the African continent as well as provide solutions to all needs for our customers such as the procedures, accommodation, food and activities to go where they want to go,” said Ms. Dharsee.



“The campaign also wants to change the attitude that destinations in Western world (Europe and America) and Dubai are better than Africa. Apart from facilitating Africans with easy accommodation and travel services within their boundaries, we are going also to open-up the outbound destinations to them. In this case a traveler will be able to book and pay for his/her flight ticket, for example from Dar es Salaam to London, via local currency. All those are possible with our website whereby a travel can book a hotel and flight ticket at the same time without a hustle of searching from one company’s website to another,” added the company’s Country Manager.



However, the campaign will not only benefit customers but also hoteliers as well through the visibility of their hotels which they are going to receive to enhance business growth. Hoteliers will be benefited from the massive visibility through the company’s website and social media platforms, provide them with technology to simplify operation of their businesses such as Extranet, SMS/Emails as well as encouraging provision and improvement of quality services to obtain better review scores.



Explaining on how Jumia Travel facilitates easy operations of hotels, a Deputy General Manager of Hong Kong Hotel of Dar es Salaam city center, Mr. Mganja Suleiman said that, “Joining Jumia Travel has benefited our hotel a lot. First of all, the marketing and visibility activities of our property has increased within and outside the boundaries of Tanzania. Hence, increased coverage of our services as you all know, marketing and advertising need a substantial capital in terms of execution which I am quite sure a few hotels can manage that. Apart from that, through their website our customers can visit, browse and book rooms without contacting us directly as well as leaving comments and reviews on our services.”



“To a greater extent this online platform has been a pushing force for us to keep on providing quality services and keep on doing regular improvements so as to stay competitive. All in all, I would like to also commend on the good job they are doing especially by introducing to us technologies which help in facilitating easy operations of our hotel. For instance, Jumia Travel’s Extranet plays a great role in simplifying hotel or reservation managers to receive bookings wherever and whenever they are. This system is not only accessed through our computers but also on tablets and smartphones. Now I don’t need to be at the front desk at the hotel to receive customers’ bookings, I can do that right here via my phone. Lastly but not least, this system provides us an opportunity to review the number and type of customers who regularly use our services, hence to know what and where to improve our services so as to meet their expectations,” concluded the Deputy General Manager of Hong Kong Hotel.

Below is the link for 2017 HOSPITALITY REPORT

https://travel.jumia.com/en-gb/hospitality-report-africa

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: JUMIA TRAVEL YAZINDUA RIPOTI YA UTALII BARANI AFRIKA
JUMIA TRAVEL YAZINDUA RIPOTI YA UTALII BARANI AFRIKA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgg_qduH73ngVjZizpOICOULe_nSGSpZMrpGTQgccbtxabeHqZxqvW5vHk891FMgGwAe0YhXu19fGJVaybwuPCOa0kco8l108DBlcZl4uRxgnkBdWc6QdEVOC-Zbz1plw5BO1hXceQoU0Y/s640/K3.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgg_qduH73ngVjZizpOICOULe_nSGSpZMrpGTQgccbtxabeHqZxqvW5vHk891FMgGwAe0YhXu19fGJVaybwuPCOa0kco8l108DBlcZl4uRxgnkBdWc6QdEVOC-Zbz1plw5BO1hXceQoU0Y/s72-c/K3.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/jumia-travel-yazindua-ripoti-ya-utalii.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/jumia-travel-yazindua-ripoti-ya-utalii.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy