Mwanariadha Alphonce Simbu aliyeshika nafasi ya tano katika mashindano ya London Marathon anatarajia kutembelea bunge la Jamhuri ya Muung...
Mwanariadha Alphonce Simbu aliyeshika nafasi ya tano katika mashindano ya London Marathon anatarajia kutembelea bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhamisi April 27 akiwa ni mgeni maalum wa Waziri wa Habari, Sanaa, Michezo na Utamaduni Harisson Mwakyembe. Baada ya kutembelea bumge hilo Simbu pia atakuwa na mazungumzo na Waziri Mwakyembe.
Simbu ataambatana na muwakilishi wa wadhamini wake DStv pamoja na maafisa waandamizi wa Jeshi la Kujenga Taifa JKT.
Akizungumzia
mualiko huo, mwanariadha huyo amesema kuwa amefurahi sana kupata
mualiko wa Waziri anayehusika na sekta ya michezo kwenda bungeni kama
mgeni wake maalum. Amesema hii inaonyesha kuwa serikali inatambua
jitihada zake anazozifanya
katika kuiwakilisha vyema nchi katika mashindano ya kimataifa.
“Nimefurahi sana kualikwa na muheshimiwa Waziri kumtembelea bungeni,
bila shaka hii itakuwa fursa nzuri ya hata wabunge kutambua jitihada
tunazofanya vijana wao katika kuliletea taifa sifa. Natumaini
pia nitapata fursa ya kuongea ana kwa ana na Waziri” alisema Simbu na
kuongeza kuwa atatumia fursa hiyo kumueleza Waziri changamoto nyingi
wanazokabiliana nazo wanamichezo hapa nchini.
Amesema
kuna mengi ya kuongea na Waziri na kwamba anaamini mazungumzo yao
yatakuwa na tija na manufaa si kwake tu, bali kwa wanamichezo wote kwa
ujumla.
Kwa upande wake, Meneja Uhusiano wa
Multichoice Tanzania Johnson Mshana, ambaye anaandamana na Simbu,
amesema kuwa anaamini kuwa ziara hiyo na mkutano na Waziri utakuwa na
manufaa makubwa kwani pia itakuwa ni fursa nzuri ya kujadili namna
bora zaidi ya Serikali kushirikiana na wadau katika kuimarisha na
kuendeleza michezo hapa nchini. “sisi kama wadhamini wa mwanariadha huyu
tunaamini kuwa kitendo cha Waziri kutualika ni ishara tosha kuwa kweli
anadhamiria kushirikiana na sisi wadau wa michezo
ili kuongeza nguvu za pamoja za kuimarisha michezo hapa nchini” alisema
Mshana
Multichoice Tanzania kupitia DStv
imekuwa ikimdhamini Simbu tangu mwaka jana na udhamini huo pia
umewanufaisha wanariadha wengine ambao wamekuwa kambini kwa muda sasa
pamoja na simbu. “Kambi ya mazoezi ya Simbu ambayo ilidhaminiwa na DStv
pia ilikuwa na wanariadha wengine ambao wote walinufaika moja kwa moja
na udhamini huo. Tunaamini kuwa pia kati ya hao tutapata wanariadha
watakaofanya vizuri siku zijazo”.
Alphonce
Simbu, ambaye pia ni mshindi wa medali ya dhahabu katika mashindano ya
Mumbai Marathon ni miongoni mwa wanariadha wa timu ya Taifa
itakayoshiriki katik mashindano ya Dunia yatakayofanika jijini London
mwezi Agosti mwaka huu
COMMENTS