MISRI KUWEKEZA VIWANDA VYA KUTENGENEZA DAWA ZA BINADAMU NCHINI TANZANIA

Na. Catherine Sungura, WAMJW                   Ujumbe wa wawekezaji toka nchini Misri wamewasili nchini hapa na kufanya mazung...





Na. Catherine Sungura, WAMJW               
  
Ujumbe wa wawekezaji toka nchini Misri wamewasili nchini hapa na kufanya mazungumzo na serikali ya Tanzania kwa nia ya kujenga  viwanda vya dawa za binadamu zikiwemo za majimaji pamoja na zile za antibiotic.
Ujumbe huo ulikutana jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu  pamoja na wawakilishi toka wizara Viwanda,Biashara na Uwekezaji na Kituo cha Uwekezaji cha Taifa (TIC) kwenye ofisi ndogo ya wizara ya afya,maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto iliyopo jijini Dar es Salaam
Ujumbe huo ulisema kuwa kiwanda walichokusudia kujenga nchini hapa kitazalisha  dawa za majimaji yaani “IV Fluids” pamoja na “antiobiotics” za aina mbalimbali  ikiwemo "Paracetamol IV” na dawa za kutibu Malaria
Aidha, walisema lengo lao ni kujenga kiwanda kikubwa ambacho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha dawa ambazo zitawahudumia watanzania pamoja na nchi za Afrika Mashariki na ya kati.
Katika mazungumzo hayo,wawekezaji hao pia wanatarajia kusaidia Tanzania katika uzalishaji wa chanjo ya ugonjwa wa homa ya Ini (Hepatics B na C)
Kwa upande wake Waziri Ummy amewaahidi wawekezaji hao kuwasaidia katika mipango ya ujenzi huo na kutoa ushirikiano wa dhati katika kufanikisha viwanda hivyo vinajenga nchini kwa muda uliopangwa.
“Naelekeza kwa taasisi zote zitakazoguswa na uanzishwaji wa viwanda hivi watoe ushirikiano wa hali ya juu ili lengo hili lifikiwe, soko la dawa hapa nchini lipo naomba niwahakikishie hili”alisema waziri Ummy.
Waziri Ummy aliwaomba wawekezaji hao kuharakisha ujenzi wa viwanda huo na kujengwa ndani ya miezi kumi na nane kama walivyoahidi ili watanzania waanze kunufaika mapema. 
         

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MISRI KUWEKEZA VIWANDA VYA KUTENGENEZA DAWA ZA BINADAMU NCHINI TANZANIA
MISRI KUWEKEZA VIWANDA VYA KUTENGENEZA DAWA ZA BINADAMU NCHINI TANZANIA
https://mail.google.com/mail/u/0/?ui=2&ik=28245c01cb&view=fimg&th=15b9a6c83187092b&attid=0.0.1&disp=emb&realattid=8db4c88643462b75_0.2&attbid=ANGjdJ-7Hg_8xSJGkA6Ixjdd7bjm4mZ0Vq-JfWjQFzdx-nV6M4bal8AEuSGl4bDLPNGhBown2qkKkQvpBTzhvBCxvN-f-snGfRd4D5r0hHVoMEn7HposTJ9OK_Y-TOI&sz=s0-l75-ft&ats=1492959219185&rm=15b9a6c83187092b&zw&atsh=1
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/04/misri-kuwekeza-viwanda-vya-kutengeneza.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/04/misri-kuwekeza-viwanda-vya-kutengeneza.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy