Ijumaa hii na kila Ijumaa ni siku ya raha na starehe kwa wakazi wa Tabata na vitongoji vyake, maana mara tu baada ya jua kuzama kiota ma...
Ijumaa
hii na kila Ijumaa ni siku ya raha na starehe kwa wakazi wa Tabata na
vitongoji vyake, maana mara tu baada ya jua kuzama kiota maarufu cha
NEXT DOOR kilichopo katika kitongoji hicho cha wastaarabu huwaka moto wa
midundo ya aina mbalimbali inayoporomoshwa na IVORY BAND iliyosheheni
vipaji visivyo vya kawaida.
Ripota
wa Globu ya Jamii alipotembelea hapo katika ukumbi wa NEXT DOOR Ijumaa
hakuweza kuamini macho na masikio yake kukuta ukumbi umefurika mashabiki
wakipata burudani toka kwa vijana hao. Akaamua kuhoji wahusika.
“Bendi
hii tulianzisha mwaka jana (2016) mwezi wa tano na wamiliki wake ni
sisi wanamuziki wenyewe tukishirikiama na wenzetu kadhaa ambao
tumewaajiri”, alisema mmoja wa wamiliki wa IVORY BAND, Rama Pentagone,
wakati wa mapumziko mafupi. Alisema waliamua kujiita IVORY BAND sababu
ya kuangalia jina fupi litalokuwa rahisi kushikika na pia hakuna
asiyefahamu thamani ya "IVORY" (Pembe ya ndovu).
Pentagone,
anayepiga kinanda, gitaa na kuimba alisema wamiliki wa bendi hiyo ni
yeye, mwanamuziki mkongwe mwenye sauti tamu Saleh Kupaza, Omari Kisila
na Amina Juma. “IVORY BAND bado hatujatoa mtindo wa kutumia kwa sababu
sisi tunapiga muziki tofauti na wengie wengine, hasa ukizingatia kwamba
hatupigi “Sebene”, alisema Pentagone.
Saleh
Kupaza aliyekuwa pembeni akipoza koo na maji alisema hatua ya kwanza ya
kuanzisha bendi na kujiajiri wao wenyewe imefanikiwa kwa asilimia 100,
na kwamba sasa wako katika hatua ya pili ambayo ni kuazalisha nyimbo
kibao zenye mtazamo wa kitaiafa na kimataifa.
“Malengo
yetu ya mbeleni ni kuwa kundi la muziki la Kimataifa na endapo Mungu
atatujalia kutimiza malengo yetu ni kufanya maonesho makubwa ndani na
nje ya nchi”, alisema Kupaza.
Omari
Kisila akaongezea kwamba kwa kuwa inakaribia watimize mwaka mmoja toka
waanze rasmi, IVORY BAND imepanga kufanya bonge la onesho
litakaloandamana na sherehe za bendi hiyo kutimiza mwaka mmoja mnamo
mwezi wa Julai.
“Tumeamua
kufanya onesho hilo kabambe mwezi wa Saba kwa sababu mwezi Mei na Juni
utakuwa ni Mwezi Mtukufu wa Ramadhani unaotarajiwa kuanza mwishoni mwa
mwezi Mei na kumalizikia mwezi Juni”, alisema Kisila.
Amesema
ukumbi pamoja na tarehe rasmi ya kufanyika tukio hilo vitatangazwa muda
utapokaribia, na kwamba kwa sasa wako katika hatua za mwisho za kuanza
kupasua anga za redio na TV kwa kutoa kibao chao cha utambulisho
kiitwacho SHIKA MOYO unachokisikia hapo chini. Hicho ni moja ya vibao
takriban kumi ambavyo husisimua mashabiki kila wapigapo.
COMMENTS