K atibu wa Kamati Maalum ya NEC Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Zanzibar , Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza n...
Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Zanzibar , Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza
na vyombo vya habari katika eneo la Mwanyanya Mikoroshini lililopo mkoa
wa Mjini Magharibi ambalo matendo ya uhalifu ikiwepo utumiaji wa dawa
za kulevya na uporaji hufanyika
hapo ambapo ameuagiza uongozi wa Jeshi la Polisi kushirikiana na
wananchi kuhakikisha wahalifu hao wanakamatwa na kupelekwa kwenye vyombo
vya sheria.
Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Zanzibar,
Mhandisi Hamad Masauni, akiangalia jeraha la mmoja wa wananchi wa eneo
la Mwanyanya Mikoroshini lililopo mkoa wa Mjini Magharibi, ambaye wiki
chache zilizopita alijeruhiwa na mapanga na watu wanaofanya matendo ya
uhalifu katika eneo hilo.
Mkuu
wa Upelelezi Mkoa wa Mjini Magharibi, ASP Suleiman Khamis Juma,
akizungumza na vyombo vya habari juu ya hatua zilizochukuliwa na Jeshi
la Polisi kudhibiti matukio ya uhalifu katikaeneo la Mwanyanya
Mikoroshini lililopo mkoa huo, wakati wa ziara ya Katibu wa Kamati
Maalum ya NEC Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Zanzibar, Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani) kutembelea maeneo sugu ya uhalifu.
Katibu wa Kamati Maalumya NEC Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Zanzibar,
Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mjini
Magharibi, ASP Suleiman Khamis Juma(kushoto), baada ya kutembelea eneo
la Mwanyanya Mikoroshini lililopo mkoa huo ambalo matendo ya uhalifu ikiwepo utumiaji wa dawa za kulevya na uporaji hufanyika ambapo Katibu huyo wa NEC ameuagiza uongozi wa Jeshi la Polisi kushirikiana na wananchi kuhakikisha wahalifu hao wanakamatwa.
Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kaskazini A, Mkoa wa Kaskazini Unguja, Ally Kitole, akimuelezaKatibu wa Kamati Maalumya NEC Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Zanzibar,
Mhandisi Hamad Masauni baadhi ya hatua walizochukua katika kupambana na
uhalifu unaoatokea eneo la Mwanyanya Mikoroshini.Picha na Abubakari Akida
COMMENTS