RAIS wa Jamhuriya Muungano wa Tanzania, Dkt. John PombeMagufuli, “ametembea’ kwenye maneno yake, aliyoyatoa mapema ...
RAIS wa Jamhuriya
Muungano wa Tanzania, Dkt. John PombeMagufuli, “ametembea’ kwenye
maneno yake, aliyoyatoa mapema wakati akizindua Bunge la Tanzania kwamba
ifikapo mwisho wa Septemba 2016, Serikali itaingiza nchini ndege mbilimpya, na
leo ndege ya ya pili aina ya Bombadier Q400 imewasili nchini leo mchanaikitokea
nchini Canada ilikoundwa.
Ndege ya kwanza iliwasili
mapema wiki iliyopita na taarifa zinasema Jumatano Septemba 28, 2016, Rais
Magufuli atazindua ndege hizo ili zianze kutoa huduma. Pichani ndege hizo zikiwa
zimeegeshwa kwenye hanga la ndege za Kjeshi (Air Wings) Ukonga jijini Dar es
Salaam. (PICHA NA IKULU)
Ndege ya pili ya
Bombadier Q400 iliyonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Taifa
(ATCL) ikipata Saluti ya maji (Water Canon Salutation) mara tu baada ya kutua
katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo
Septemba 27, 2017 ikitokea Canada ilikotengenezwa. Sherehe za uzinduzi rasmi wa
ndege hizo umepangwa kuganyika kesho Jumatano Septemba 28, 2016 hapo hapo
uwanjani.
Ndege hiyo ikitua kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dares Salaam, Septemba 27, 2016
Katibu Mkuu Uchukuzi Dkt
Leonard, Chamriho akisalimiana na rubani John Kuipers
aliyeeendesha Ndege ya pili ya Bombadier Q400 iliyonunuliwa na serikali kwa
ajili ya Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) na kuiwasilisha salama katika uwanja
wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 27,
2017 ikitokea Canada ilikotengenezwa. Sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege hizo
umepangwa kuganyika kesho Jumatano Septemba 28, 2016 hapo hapo uwanjani.
Katibu Mkuu Uchukuzi, Dkt
Leonard Chamriho na viongozi wengine wakielekea kwenye Ndege ya pili ya
Bombadier Q400 iliyonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Taifa
(ATCL) ilipowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini
Dar es salaam leo Septemba 27, 2017 ikitokea Canada ilikotengenezwa. Sherehe za
uzinduzi rasmi wa ndege hizo umepangwa kuganyika kesho Jumatano Septemba 28,
2016 hapo hapo uwanjani.
Katibu Mkuu Uchukuzi Dkt
Leonard Chamriho, akiikagua ndege hiyo kwa ndani
COMMENTS