Na Mwandishi Wetu Benki ya TIB Corporate leo imetoa msaada wa mabati mia moja kwa mkoa wa Songwe ili kusaidia kukabiliana na u...
Na Mwandishi Wetu
Benki ya TIB Corporate leo
imetoa msaada wa mabati mia moja kwa
mkoa wa Songwe ili kusaidia kukabiliana na upungufu wa vyumba vya madarasa,
nyumba za walimu na vyoo mkoani humo.
Mkoa wa Songwe, ambao ni
miongoni mwa mikoa mipya, itatumia mabati hayo katika shughulli za ujenzi wa
vyumba vya madarasa kwa wilaya za Mbozi,
Mamba, Ileje, Songwe na Tunduma.
Akizungumza wakati wa
makabidhiano hayo, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Benki ya TIB Corporate, Bwana Frank
Nyabundege alisema msaada huo umelenga kuonyesha nia na jitihada za benki yake
katika kusaidia kukuza elimu na pia kuunga mkono serikali katika jitihada zake za kuboresha elimu nchini.
'Serikali pekee yake
haiwezi kukuza sekta ya elimu hivyo basi ni muhimu tuisaidie serikali katika kuboresha
sekta ya elimu kwa kuaanda mazingira mazuri kwa vijana wetu kujisomea’ alisema
Nyabundege.
Akitoa shukrani zake
kwa benki ya TIB Corporate, Mkuu wa mkoa wa Songwe Mheshimiwa Chiku Gallawa alisema
mchango huo ni muhimu katika kukuza na kuboresha sekta ya elimu ambayo ndio kichocheo cha ukuaji wa sekta ya
uchumi na kijamii kwa taifa la kesho.
‘Tunaishukuru benki ya
TIB Corporate kwa jitihada zake za kushirikiana
na serikali katika kukuza sekta ya elimu kwani hakuna taifa linaloweza kuendelea
bila kuwa na raia wasomi ' alisema Mheshimiwa Gallawa.
COMMENTS