Mabondia Mada Maugo (kushoto) na Abdallah Pazi wakitunishiana misuli baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga siku ya sikuku...
Bondia Mada Maugo (kushoto) akipokea sehemu ya malipo ya awali kutoka kwa mratibu Rajabu Mhamila 'Super D' wa mpambano wake na Abdallaha Pazi. Utakaofanyika siku ya sikukuu ya Pasaka (Picha na SUPER D BOXING NEWS)
Na Mwandishi Wetu
Mabondia Mada Maugo na Abdalla Pazi 'Dulla Mbabe' wamesaini mkataba wa kuzipiga siku ya sikukuu ya pasaka katika uwanja wa ndani wa taifa mpambano wa raundi nane KG 76.
Akizungumza wakati wa kutiliana saini mikataba hiyo kocha wa mchezo wa masumbwi nchini ambaye ni mratibu wa mpambano huo amesema kuwa amewasainisha mabondia hawo ambao wanatamba katika tasnia ya masumbwi nchini ili wapenzi wa mchezo wa masubwi waburudike siku hiyo ya sikukuu ya pasaka
mbali na mpambano uho siku hiyo bondia chipkizi anaekuja kwa kasi zaidi katika mchezo wa masumbwi Vicent Mbilinyi anaetokea katika Super D Boxing Promotion atakae pambana na Mwinyi Mzengela mpambano wa KG 63 raundi nane mpambano mwingine utawakutanisha bondia Cosmas Cheka na Mohamed Matumla na Pius Kazaula atakumbana na Seba Temba
COMMENTS