ISSA HAYATOU HATIMAYE ANG'OKA CAF, ZANZIBAR RASMI MWANACHAMA WA SHIRIKISHO HILO

K-VIS BLOG NA MASHIRIKA YA HABARI HATIMAYE Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF), aliyekaa madarakani kw...


K-VIS BLOG NA MASHIRIKA YA HABARI
HATIMAYE Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF), aliyekaa madarakani kwa muda mrefu, Mzee Issa Hayatou,(70), pichani juu, “ameng’oka” kwenye nafasi hiyo kufuatia ushindi mnono alioupata mpinzani wake, Rais wa chama cha soka cha Madagascar, Ahmad Ahmad, kufuatia uchaguzi mkuu wa Shirikisho hilo, uliofanyika mjini Addis Ababa Ethiopia leo Machi 16, 2017.
Katika uchaguzi huo, Ahmad Ahmad alijikusanyia jumla ya kura 30 ikiwa ni kura 10 zaidi ya Hayatou aliyeambulia 20.
Matokeo hayo yanahitimisha miaka 29 ya utawala wa Hayatou kama kiongozi wa juu wa soka barani Afrika.
Hayatou alikuwa rais wa CAF tangu mwaka 1988 wakati huo Lionel Messi akiwa na miezi tisa tu tangu azaliwe wakati mtawala huyo mzaliwa wa Cameroon alipotangazwa kusimamia soka la bara la Afrika.
Wakati huo huo, kilio cha Wazanzibara kimepata jibu baada ya mkutano mkuu wa 39 wa Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) unaoendelea mjini Addis-Ababa, Ethiopia, umepitisha ombi la chama cha soka Zanzibar (ZFA) kuwa mwanachama rasmi wa CAF.
Ni jambo la kihistoria kwa Zanzibar kwani safari hii ombi lao limepitishwa bila kupingwa na inakuwa nchi ya 55 mwanachama wa kujitemea wa CAF.
Awali Zanzibar ilikuwa inaunganishwa na Tanzania bara chini ya TFF na kupelekea kukosa haki za kushiriki kama nchi kwenye mashindano yanayoandaliwa na CAF pamoja na yale ya FIFA.
Pendekezo hilo lilipelekwa na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ndugu, Jamal Malinzi na lilipokelewa na wajumbe 54 wengine waliokuwepo.
Hii maana yake ni kuwa kwa sasa CAF ndio shirikisho mwanachama wa FIFA kwa upande wa mabara lenye wanachama wengi zaidi kuliko wote.
Vilabu vya Zanzibar vimekuwa vikishiriki mashindano mbalimbali ya CAF lakini kwa ngazi ya kitaifa hawakuwa na ruhusa na walicheza kwa kuungana na Tanzania bara na kushiriki kama Tanzania.
Kwa maana hiyo basi, chama cha soka cha Zanzibar kitapata uwezeshaji wa kifedha moja kwa moja kutoka CAF na FIFA kwa ajili ya timu ya taifa.


Rais mpya wa CAF, Ahmad Ahmad.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: ISSA HAYATOU HATIMAYE ANG'OKA CAF, ZANZIBAR RASMI MWANACHAMA WA SHIRIKISHO HILO
ISSA HAYATOU HATIMAYE ANG'OKA CAF, ZANZIBAR RASMI MWANACHAMA WA SHIRIKISHO HILO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgVo01QzL0usBju_loFLnMJBuFfJYzHGJXT9sKmlIPobP4vldXp6IRd-mF11MYSCaapkJsNpfnNjCrZGpuLbG8xSK8xBQ_Cq9dafMfFjdyzQ1rP7baYZqtIUYm81447K-FUmr02sHVCknM/s640/issahayatou.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgVo01QzL0usBju_loFLnMJBuFfJYzHGJXT9sKmlIPobP4vldXp6IRd-mF11MYSCaapkJsNpfnNjCrZGpuLbG8xSK8xBQ_Cq9dafMfFjdyzQ1rP7baYZqtIUYm81447K-FUmr02sHVCknM/s72-c/issahayatou.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2017/03/issa-hayatou-hatimaye-angoka-caf.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/issa-hayatou-hatimaye-angoka-caf.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy