SERIKALI YADHAMIRIA KUMALIZA MGOGORO WA NYAMONGO-MAJALIWA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kumaliza mgogoro ulipo kati ya wananchi wa Kata ya Nyamongo na muwekezaji wa mgodi...



WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kumaliza mgogoro ulipo kati ya wananchi wa Kata ya Nyamongo na muwekezaji wa mgodi wa North Mara.


Amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha wananchi pamoja na mwekezaji wa mgodi huo wanaishi na kuendesha shughuli zao za kimaendeleo kwa kufuata sheria za nchi.Ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Januari 18, 2018) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Kata ya Nyamongo, wilayani Tarime.


Waziri Mkuu amesema Serikali haiwezi kuvumilia kuona wananchi na wawekezaji wakigombana, inataka kumaliza mgogoro huo ili pande zote zifanye kazi zake kwa amani.Katika kuhakikisha mgogoro huo unakuwa historia Waziri Mkuu ameitisha kikao kitakachowakutanisha wawakilishi wa wananchi , viongozi wa mgodi na mbunge wa jimbo la Tarime Bw. John Heche.


Amesema katika hicho kitakachofanyika Januari 28, 2018 Ofisini kwa Waziri Mkuu mjini Dodoma, ambapo aliwakikishia wananchi hao kwamba Serikali italinda maslahi yao.Awali, Waziri Mkuu alitembelea kata ya Nyamwaga na kukagua kituo cha afya cha Nyamwaga, ambapo amesema kinatosha kupandishwa hadhi na kuwa hospitali ya wilaya.


Hivyo amemuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara, Dkt. Francis Mwanisi aanze mchakato wa kupeleka vifaa katika kituo hicho ili wananchi wa Halmashauri ya Tarime waanze kutibiwa.


Waziri Mkuu amesema Rais Dkt. John Magufuli ameongeza bajeti ya ununuzi wa dawa na kufikia sh. bilioni 269 ili kuhakikisha hakuna mgonjwa anayekwenda hospitali na kukosa dawa.


Amesema mbali na kuongeza bajeti katika ununuzi wa dawa, pia ameziagiza halmashauri zote kuhakikisha suala la utoaji wa vitambulisho kwa wazee ili watibiwe bure linatekelezwa

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SERIKALI YADHAMIRIA KUMALIZA MGOGORO WA NYAMONGO-MAJALIWA
SERIKALI YADHAMIRIA KUMALIZA MGOGORO WA NYAMONGO-MAJALIWA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgCDWrAJlAEbZ5QivPCJ_KN-22NAUY7QWe5dHnrpKdchc6KzCy9iL-PgJ-pjkZxfQP3_CMPJiI_-wUYA-yZuGKTE86MuJujc_fnsxnL0M2RkeSQUeJOcVobJqS3GaBbkTa4pj_ao5kOLD35/s400/index.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgCDWrAJlAEbZ5QivPCJ_KN-22NAUY7QWe5dHnrpKdchc6KzCy9iL-PgJ-pjkZxfQP3_CMPJiI_-wUYA-yZuGKTE86MuJujc_fnsxnL0M2RkeSQUeJOcVobJqS3GaBbkTa4pj_ao5kOLD35/s72-c/index.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2018/01/serikali-yadhamiria-kumaliza-mgogoro-wa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/01/serikali-yadhamiria-kumaliza-mgogoro-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy