JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA HABARI UTAMADUNI SANAA NA MICHEZO TAARIFA KWA UMMA Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Mic...
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA HABARI UTAMADUNI SANAA NA MICHEZO
TAARIFA KWA UMMA
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe anatoa pole kwa Kituo cha Utangazi cha EFM,familia, ndugu jamaa na marafiki pamoja na Watanzania kwa ujumla kufuatia kifo cha cha aliyekuwa Mtangazaji wa kituo hicho Bw. Seth Katende kilichotokea tarehe 09 /07/2017 katika hospitali ya Taifa Muhimbili.
Waziri Mwakyembe ametoa pole hizo kufuatia taarifa iliyotolewa na kituo cha Utangazaji cha EFM iliyoeleza kuwa Marehemu Seth awali alikuwa amelazwa katika Hospitali ya TMJ na baadae kuhamishiwa hospitali ya Taifa Muhimbili mpaka mauti ilipomfika.
Dkt Mwakyembe amesema kuwa kituo cha EFM kimepoteza mtangazaji muhimu aliyekuwa anafanya kazi yake kwa umahiri mkubwa hasa katika kipindi chake cha UBAONI.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.
Imetolewa na:
Zawadi Msalla
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo.
12/07/2017
COMMENTS