JAJI KIONGOZI MHE. FERDINAND WAMBALI AKAGUA SHUGHULI ZA MAHAKAMA KANDA YA SONGEA

  Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mk...


 Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Ruvuma (Hawapo Pichani) wakati alipomtembelea Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe. Binilith Mahenge ofisini kwake akiwa katika ziara ya kukagua shughuli za Mahakama na Kusisitiza Utekelezaji wa Mpango Mkakatiwa Miaka Mitano wa Mahakama ya Tanzania katika Kanda ya Songea. 
 
 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe. Binilith Mahenge akizungumza.
 
 Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali akizungumza na Watumishi wa Mahakama Kuu kanda ya Songea (Hawapo Pichani) akiwa katika ziara ya kukagua shughuli za Mahakama na Kusisitiza Utekelezaji wa Mpango Mkakatiwa Miaka Mitano wa Mahakama ya Tanzania katika Kanda ya Songea. 
 
Mtendaji wa Mahakama, Samson Mashalla akifafanua masuala mbalimbali yanayohusu Utumishi kwa Watumishi wa Mahakama Kuu kanda ya Songea (hawapo pichani) wakati wa ziara ya Jaji Kiongozi kwenye kanda hiyo. 

Na Lydia Churi, Songea

Katika ziara hiyo Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mheshimiwa Ferdinand Wambali amesema Mahakama itashirikiana na wadau wake ili kuhakikisha kesi zinamalizika kwa haraka kwenye mahakama mbalimbali nchini. 

Amesema kupitia nguzo ya tatu ya Mpango Mkakati wa miaka mitano wa mahakama ya Tanzania ambayo inasisitiza kujenga imani ya wananchi kwa Mahakama na ushirikishwaji wa wadau katika shughuli za mahakama, Mahakama itatoa elimu kwa wananchi pamoja na viongozi wakiwemo wakuu wa wilaya juu ya masuala mbalimbali yanayohusu utoaji wa haki kwa wananchi. 

 Jaji Kiongozi amesema Mahakama imejiwekea mikakati ya kuhakikisha kesi zinamalizika kwa wakati na kwa haraka ukiwemo mkakati wa kesi kutokukaa kwa zaidi ya miaka 2 kwenye Mahakama Kuu, miezi 12 Mahakama za mikoa na Wilaya pamoja na miezi sita kwenye Mahakam za Mwanzo. Mikakati mingine ni ile ya kesi kusikilizwa kwa mfululizo na kuwekwa kwa maahirisho mafupi mafupi ya kesi kwenye Mahakama mbalimbali nchini na Majaji na Mahakimu kupangiwa idadi ya kesi watazosikiliza katika kipindi cha mwaka moja. 

Aidha, kila Jaji amepangiwa kusikiliza na kumaliza kesi 220 kwa mwaka ambapo Mahakimu wamepangiwa kumaliza kesi 250 kwa mwaka. 
Akizungumzia Maadili kwa watumishi wa Mahakama, Jaji Wambali amewataka watumishi hao kuwahudumia wananchi wanaofika mahakamani kwa bidii, uaminifu, na uadilifu ili kujenga imani ya wananchi kwa Mahakama. 
Amesema watumishi wa Mahakama hawana budi kufanya kazi kwa upendo na ushirikiano kwa kuwa kazi za mahakama zinategemeana ambapo kila kada ina umuhimu wake katika wananchi kufikia haki zao za msingi.
 Jaji Kiongozi yuko kwenye ziara katika kanda za Songea na Mtwara kwa ajili ya kukagua shughuli za kimahakama pamoja na kusisistiza utekelezaji wa Mpango Mkakati wa miaka mitano wa Mahakama ya Tanzania. Tayari ametembelea mahakama zilizoko Songea mjini na zile za wilaya za Mbinga, Nyasa, Namtumbo, na Tunduru.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: JAJI KIONGOZI MHE. FERDINAND WAMBALI AKAGUA SHUGHULI ZA MAHAKAMA KANDA YA SONGEA
JAJI KIONGOZI MHE. FERDINAND WAMBALI AKAGUA SHUGHULI ZA MAHAKAMA KANDA YA SONGEA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiMVQqv5mrSQowqfK6F6bqsjiaKPEhfsu2yPsiRixq4xPGacclsR9CxkE5Zd4LwkO6bJ0kC3lGDwoPu2EgUWieibvmbTB09n-RTN9E4LoPhk5xyOMnfeO3WZppfKAOkFqAogFRJjVceqoQ/s640/unnamed+%252825%2529.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiMVQqv5mrSQowqfK6F6bqsjiaKPEhfsu2yPsiRixq4xPGacclsR9CxkE5Zd4LwkO6bJ0kC3lGDwoPu2EgUWieibvmbTB09n-RTN9E4LoPhk5xyOMnfeO3WZppfKAOkFqAogFRJjVceqoQ/s72-c/unnamed+%252825%2529.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/jaji-kiongozi-mhe-ferdinand-wambali.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/jaji-kiongozi-mhe-ferdinand-wambali.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy