Mwanasheria toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare Heche akionesha kwa waandishi wa habari moja ya po...
Mwanasheria
toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare
Heche akionesha kwa waandishi wa habari moja ya pombe kali aina ya Nguvu
zilizokamatwa wakati wa operesheni inayoendelea mapema leo hii jijini
Dar es Salaam wakati wa siku ya nne ya operesheni ya kusaka wasambazaji
wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.
Msimamizi
wa ghala la Love kira Enterprises lililopo Wazo Bi. Sia Mboya
(kushoto) akitoa maelekezo kwa Mwanasheria toka Baraza la Taifa la
Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare Heche (katikati) wakati wa
operesheni ya kuondoa pombe hiyo katika soko, kulia ni Afisa Afya toka
Manispaa ya Kinondoni Bw. John Kijumbe.
Gari lililokutwa limebeba pombe kali aina ya kiroba original likiwa
limeegeshwa nje ya duka kuuza vinywaji la Love Kira lililopo Wazo jijini
Dar es Salaam mapema hii leo.
COMMENTS