Na Lilian Lundo – MAELEZO Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inatararajia kuanza upasuaji wa kupandikiza Moyo kwa wagonjwa...
Na Lilian Lundo – MAELEZO
Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inatararajia kuanza upasuaji wa
kupandikiza Moyo kwa wagonjwa wenye matatizo ya moyo nchini.
Mkurugenzi
wa Upasuaji na Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Moyo na Mishipa ya Damu
Dkt. Bashir Nyangasa ameyasema hayo leo Jijini, Dar es Salaam alipokuwa
akiongea na vyombo vya habari kuhusu malengo ya Taasisi hiyo.
“Tuko
katika maandalizi ya kuandaa mapendekezo kwa ajili ya kupeleka Bungeni
ili Bunge lilidhie na kupitisha sheria itakayoruhusu mtu kuandika wosia
wa viungo vyake kutumika mara baada ya kufariki, ikiwemo moyo, figo na
viungo vingine,” alifafanua Dkt. Nyangasa.
Aliendelea
kwa kusema kuwa, umefika wakati kwa watanzania kujiwekea utaratibu wa
kuacha wosia wa kutumika kwa viungo vyao mara baada ya kufariki kwa
ajili ya kuhifadhiwa katika benki za viungo ili viweze kutumika na watu
ambao wanauhitaji.
Aidha
Dkt. Nyangasa amesema hospitali ya Apolo Bangalole ya India na hospitali
nyingine za kimataifa za magonjwa ya moyo kwa sasa zimehamia JKCI
kutokana na huduma pamoja na vifaa vinavyopatikana katika hospitali hizo
vinapatikana katika Taasisi hiyo.
Kwa
upande wake Naibu Mkurugenzi Huduma za Tiba, Daktari Bingwa wa Wagonjwa
wa Moyo Dkt. Tulizo Shemu amesema kwa mwaka 2016 Taasisi imefanya
uchunguzi wa tiba kwa wagonjwa 973, kati ya wagonjwa hao 620 walipatiwa
matibabu ya moyo ya bila kufungua kifua kwa kupitia mishipa ya damu
(Catheterization) na wagonjwa 353 walifanyiwa upasuaji wa kufungua
kifua.
Vilevile
amesema kuwa kwa mwaka huu wa 2017 Taasisi hiyo imejipanga kufanya
upasuaji wa kupasua kifua kwa wagonjwa 700 na wagonjwa wengine 1000
watafanyiwa operesheni bila ya kufungua kifua kwa kutumia mtambo wa
‘Catheterization’.
Taasisi
hiyo inategemea kuwa na kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa
kushirikiana na Taasisi ya Open Heart International ya nchini Australia
kuanzia Machi 10, 2017 ambapo wagonjwa 25 wakiwemo watoto 15 na watu
wazima 10 watafanyiwa upasuaji.
Wananchi wameombwa kujitokeza kuchangia damu kutokana na uhitaji wa damu nyingi katika upasuaji huo.
COMMENTS