TRUMP AIWEKA DEMOKRASIA YA MAREKANI NJIA PANDA, APATA KIGUGUMIZI KAMA ATAKUBALI KUSHINDWA UCHAGUZI WA NOVEMBA 8

MGOMBEA kiti cha Rais wa Marekani kupitia chama cha Republican, tajiri Donald Trump, amekataa kukubali endapo atakubali matokeo ...










MGOMBEA kiti cha Rais wa Marekani kupitia chama cha Republican, tajiri Donald Trump, amekataa kukubali endapo atakubali matokeo ya urais kwenye uchaguzi mkuu wan chi hiyo utakaofanyika Novemba 8, 2016.
Trump aliulizwa mara tatu na mwendesha mdahalo wa tatu na wa mwisho uliowakutanisha Trump na Mgombea wa nafasi hiyo kupitia chama cha Democrat, Hillary Clinton alfajiri ya leo Oktoba 20, 2016.
“Utayakubali matokeo ya Urais endapo utashindwa kwenye uchaguzi.” Aliuliza mtangazaji wa Shirika la Habari Fox News, Chris Wallace.
Akijibu swali hilo Trump alisema, “Nitaangalia swala hilo wakati uklifika.” Alijibu kwa kifupi hata alipoulizwa mara tatu na mtangazaji huyo, Trump alisisitiza jibu lake.
Vyombo vya habari vya nchi hiyo vimekuwa vikimnukuu Donald Trump, akiwaambia wafuasi wake kuwa mpinzani wake Bibi. Hillary Clinton ameandaa “mazingira” ya kuiba kura.
Trump amekuwa akishutubu kuwa mamilioni ya watu wameandikishwa kupiga kura ilihali hawakustahili kuandikishwa  akirejea taarifa za Pew report na sehemu nyingine.
Taarifa za Pew zimeonyesha kuwa zaidi ya marehemu milioni 1.8 wamo kwenye orodha ya  wapiga kura, hata hiovyo ripoti hiyo haikusema kuwa marehemu hao milioni 1.8 wameorodhesha kama wapiga kura, zaidi ya hapo taarifa ya Pew imefafanua kuwa ni ushahidi kuwa mfumo wa orodha ya wapiga kura kwenye jimbo hilo ni muhimu ukarekebishwa ili kuondoa hitilafu hiyo.
Na kwamba hakuna ushahidi wowote wa mtapakao wa kasoro hiyo au mpango mahsusi wa kuhujumu zoezi la upigaji kura.
Hata hivyo mtangazaji wa Fox News, aliendelea kumbana Trump kwa kumkumbusha kuwa “KKuna utamaduni wa miaka mingi nchini Marekani na hakika ni moja ya tunu za nchi hii ni kubadilishana uongozi kwa amani, haijalishi ugumu na mpambano mkali wakati wa kampeni na matokeo ya uchaguzi ndio mwisho wa kampuni ambapo aliyeshindwa hukubali matokeo na kumtambua mshindi.
“Kwa hivyo unasema hauko tayari kujiandaa kwa sasa kukubali juu ya misingi hiyo.” Wallace alimuuliza tena Trump.
Trump alijibu: “Nilichokwambia ndio hicho, nitakwambia wakati ukiwadia, nitakuacha ukidhania sawa.”
Ingawa mgombea mwenza wake, Gavana wa Indiana Mike Pence na bintiye Trump, Ivanka, muda mfupi kabla ya mdahalo huo, walisema watakubali matokeo lakini Trump mwenyewe hakutaka kujiingiza yeye mwenyewe kukubali kama ataridhia matokeo endapo atashindwa.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: TRUMP AIWEKA DEMOKRASIA YA MAREKANI NJIA PANDA, APATA KIGUGUMIZI KAMA ATAKUBALI KUSHINDWA UCHAGUZI WA NOVEMBA 8
TRUMP AIWEKA DEMOKRASIA YA MAREKANI NJIA PANDA, APATA KIGUGUMIZI KAMA ATAKUBALI KUSHINDWA UCHAGUZI WA NOVEMBA 8
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj90aeb5JBElesP52Ozy8JU0mWIFkdcevF2j9Nzc-ozYLhHdS2AtzSI4SXIEzWRVvDGX3rFXW7QtOunh5RlDhIOYNsbMAD-m8ZvA0uYuaIpmPNZaSlkQSboFYsLRGdLq1bDtwoHr3D_7YM/s640/e6022c682d0d6cb6c69b0aa859e6e889.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj90aeb5JBElesP52Ozy8JU0mWIFkdcevF2j9Nzc-ozYLhHdS2AtzSI4SXIEzWRVvDGX3rFXW7QtOunh5RlDhIOYNsbMAD-m8ZvA0uYuaIpmPNZaSlkQSboFYsLRGdLq1bDtwoHr3D_7YM/s72-c/e6022c682d0d6cb6c69b0aa859e6e889.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2016/10/trump-aiweka-demokrasia-ya-marekani.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/10/trump-aiweka-demokrasia-ya-marekani.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy