PROFESA MUHONGO AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA BACKBONE WA KV 400, UNAUNGANISHA MIKOA YA IRINGA, DODOMA, SINGIDA HADI SHINYANGA

Mhandisi Oscar Kanyama (kushoto) kutoka mradi wa BackBone akitoa maelezo kuhusu mradi huo wa usafirishaji umeme wa kV4...





Mhandisi Oscar Kanyama (kushoto) kutoka mradi wa BackBone akitoa maelezo kuhusu mradi huo wa usafirishaji umeme wa kV400 kwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati). Wakati wa ziara ya Waziri kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo, Julai 26, 2016 akiwa njiani kutoka Dodoma kwenda Singida Kulia ni Meneja Mradi wa BackBone, Mhandisi Khalid James.
 


WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amesema, mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa Kilovolti 400 kutoka mkoani Iringa hadi Shinyanga utakamilika Oktoba mwaka huu 2016
Profesa Muhongo ameyasema hayo wakati akiwa kwenye ziara ya kukagua maendeleao ya ujenzio wa mradi huo (BackBone Transmission line) wenye urefu wa Kilomita 670, kutoka mkoani Iringa hadi mkoa wa Shinyanga.
Profesa Muhongo ambaye kwa sasa yuko mkoani Singida, tayario amekwishakagua maendeleo ya ujenzi mkoani Dodoma.
“ Mradi utakapo kamilika utaboresha upatikanaji wa umeme kwenye mikoa ya kanda ya Ziwa na Kastazini mwa Tanzania,” alisema Profesa Muhongo.

Profesa Muhongo pia alsiema, mradi huo ambao gharama zake ni Dola za Kimarekani Milioni 450, utapita hadi kwenye mipaka ya nchi jirani za Kenya na Zambia ambako Tanzania inaweza kuuza umeme kwenye nchi hizo wakati ambapo Tanzania itakuwa na umeme wa kutosheleza mahitaji.
Akitoa taarifa fupi ya maendeleo ya ujenzi wa mradi huo mbele ya Waziri wa Nishati na Madini, Meneja Mradi, Mhandisi Khalid James, alisema, mradi huo umegawanyika katika awamu tatu, ambapo awamu ya kwanza Iringa-Dodoma, Dodoma-Singida, na Singida-Shinyanga.
Mhandisi James, amemwambia Waziri Profesa Muhongo kuwa, awamu ya kwanza ambayo ni ujenzi wa njia ya umeme kutoka Iringa-Dodoma, ambao mfadhili mkuu ni benki ya Dunia kwa thamani ya Dola za Kimarekani Milioni 150, yenye urefu wa Kilomita 225 mradi huo umekamilika kwa asilimia 100 na utazinduliwa Septemba mwaka huu 2016.
Aidha Mhandisi huyo alisema, kipande cha Dodoma-Singida, tayari asilimia 80 ya ujenzi wa mradi umekamilika. “Wafadhili wa mradi huu ni pamoja na Benki ya Maendeleo ya Afrika, AfDB, na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), ambao wafadhili hao wametoa jumla ya Dola za Kimarekani Milioni 169. alisema Meneja mradi na kuongeza kuwa uzinduzi wa mradi huo utafanyika Oktoba 2016.
Mhandisi James alisema, awamu ya tatu ya mradi huo ambayo ni Singida-Shinyanga yenye urefu wa Kilomita 228 na ambao umefadhiliwa na Jumuiya ya Ulaya EU kwa gharama ya Dola za Kimarekani Milioni 134, umekamilika kwa asilimia 99 na utazinduliwa Oktoba mwaka huu 2016.
“Mradi huu wa BackBone pia utahusika nauboreshaji wa vituo vya kupooza na kusambaza umeme katika Mikoa ya Iringa, Dodoma, Singida na Shinyanga ambapo upanuzi huo unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Korea kwa kiasi cha Dola za Marekani Milioni 36”.


Mafundi wa Kampuni ya Joyti Structures Ltd wakiunganisha moja ya nguzo za kusafirisha umeme zenye uwezo wa kV 400 kutoka Dodoma hadi Singida.


Baadhi ya nguzo zilizokwishakamilika ambazo zitasafarisha umemewa kV 400 kutoka Iringa hadi Shinyanga.

Mhandisi Joseph Mongi kutoka Kituo cha kupooza na kusambaza umeme cha Zuzu Mkoani Dodoma akitoa maelezo kwa Waziri wa Nishati na Madini, Prof. SospeterMuhongo

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: PROFESA MUHONGO AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA BACKBONE WA KV 400, UNAUNGANISHA MIKOA YA IRINGA, DODOMA, SINGIDA HADI SHINYANGA
PROFESA MUHONGO AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA BACKBONE WA KV 400, UNAUNGANISHA MIKOA YA IRINGA, DODOMA, SINGIDA HADI SHINYANGA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiOlEmZcvOKtBzSzdv9yJSE-xwvirzSViYTwWBjXxYsxEhyzBfJCbxDL7Yo28iay1Fzc5TpBJ044jqe56OHqliN30uy9l5pG19yzGfeQRaGPmLuraMA5iQenqYavd8BJ0UJWM3ylbDVu-M/s640/Muhongoz.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiOlEmZcvOKtBzSzdv9yJSE-xwvirzSViYTwWBjXxYsxEhyzBfJCbxDL7Yo28iay1Fzc5TpBJ044jqe56OHqliN30uy9l5pG19yzGfeQRaGPmLuraMA5iQenqYavd8BJ0UJWM3ylbDVu-M/s72-c/Muhongoz.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2016/07/profesa-muhongo-akagua-maendeleo-ya.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/07/profesa-muhongo-akagua-maendeleo-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy