MSANII wa Filamu nchini Elizabeth Michael 'Lulu' ameonyesha kipaji chake kwa kuimba vyema wimbo wa YAHAYA wa Nguli wa muzik...
MSANII
wa Filamu nchini Elizabeth Michael 'Lulu' ameonyesha kipaji chake kwa
kuimba vyema wimbo wa YAHAYA wa Nguli wa muziki wa Kizaki kipya Lady Jay
Dee, na kutunzwa mijihela wakati akiimba wimbo huo na Jide kwenye
uzinduzi wa Video yake mpya na ya kwanza kusimama peke yake ya FOOLISH
AGE Agosti 30 2013.
Baada
ya move hiyo kali ya dakika 120 iliyoonyesha ukali wa staa huyo
kuoneshwa kwa dakika 20 tu na kubakisha zingine 100 kusubiri wateja
kuziona majumbani kwao alipanda jukwaani kujitambulisha na kutoa
shukrani kwa wapenzi na mashabiki wa tasnia ya filamu nchini Tanzania
kwa muitikio wao ambapo alipanda na kuimba wimbo huo wa Yahaya.
Lulu
alianza kwa kuimba kiitikio cha wimbo huo akiwa Back Stage, na
kuwashangaza watu pale alipomudu vyema wimbo huo kiasi cha mashabiki
‘Mapedeshee’ wakiongozwa na Pedeshee Rich Rich, kupanda jukwaani na
kumtunza fedha kibao ambazo hakika zilimpagawisha msanii huyo na mwisho
wa wimbo huo alitamka kuwa kweli muziki unalipa.
“Jamanieee
kumbe muziki unalipa ile mbaya yaani nimeimba ubeti mmoja tu hapa ona
mijihela kibao, kuanzia sasa na mimi nitaanza kuimba muziki”, alisema
Lulu, huku akishangiliwa na mashabiki wake.
Uzinduzi
wa filamu hiyo ya kiswahili ambayo ina sub title ya Kiingereza na
ambayo haipaswi kuangaliwa na watoto chini ya miaka 16, huku ikiwa
imechezwa na wasanii maarufu na wakongwe kama Elizabeth Michael
mwenyewe, Diana Kimaro, Hashim Kambi, Ombeni Phiri na Mzee Jengua
ulifanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Wasanii mbalimbali walihudhuria show hiyo usiku huu pale Mlimani City. (Picha kwa hisani ya Father Kidevu Blog)
Lulu Michael akizungumza machache mara baada ya Move yake kuoneshwa kwa
mashabiki na wapenzi wa filamu Tanzania ndani ya Ukumbi wa Mlimani City.
Wadau walifuatilia burudani...
Jide akikamua jukwaani...
Mama na mwanao ni kama chanda na Pete... huyo ni Natasha (kulia) na Bintiye Monalisa.
.... Walitunzana tu kivyao vyao...
noti alizo tuzwa Jide...
Rich Rich akimwaga noti
Wadau wakifuatilia uzinduzi huo wa Filamu.
Wakongwe wa Bongo Muvi wakifurahia jambo.
Mwogozaji wa Filamu za Kibongo, Leah Mwendamseke nae alikuwepo kuangalia kazi hiyo ya Lulu.
Waongoza Shughuli hiyo watangazaji wa Redio na TV Double G na mwana dada kutoka Times FM walikuwepo.
COMMENTS