MUSWADA WA SHERIA ZA HABARI UTAIPA TASNIA HESHIMA-MKURUGENZI MAELEZO
HomeJamii

MUSWADA WA SHERIA ZA HABARI UTAIPA TASNIA HESHIMA-MKURUGENZI MAELEZO

Na Jovina Bujulu-MAELEZO, Dar es Salaam WANATASNIA ya habari nchini wametakiwa kuukubali muswada wa sheria wa huduma...




Na Jovina Bujulu-MAELEZO, Dar es Salaam


WANATASNIA ya habari nchini wametakiwa kuukubali muswada wa sheria wa huduma ya habari unaotarajia kuwasilishwa hivi karibuni Bungeni kwa kuwa umekusudia kuifanya taaluma hiyo kuaminika kwa jamii.

Hayo yamasemwa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Hassan Abbas Jijini Dar es salaam wakati wa ziara yake ya kutembelea vyombo vya habari vilivyopo Jijini humo.

Alisema kwa muda mrefu wadau wa Habari na wanatasnia wenyewe wamekuwa na kiu ya kupata sheria mpya baada ya ile ya mwaka 1976, ambayo imepitwa na wakati.

“Kutokana na teknolojia kubadilika, ni wakati mwafaka wa kuanzishwa kwa taasisi inayosimamia maadili ya wanahabari, hivyo vyombo vya Habari waliona ni muhimu kuwa na sheria mpya itakayokidhi mabadiliko hayo” alisema Abbas.

Aidha, alisema kuwa sheria hiyo itahusu vyombo vya habari vya mfumo wa machapisho, ambavyo ni pamoja na magazeti na majarida na si mitandao ya kijamii kama wadau wanatafsiri.

Aliongeza kuwa miongoni mwa masuala yanayozungumziwa katika muswada huo ni pamoja na kuundwa kwa bodi ya ithibati kwa wanahabari, Baraza huru la habari, Ofisi ya mkurugenzi wa habari, na Mfuko wa mafunzo kwa wanahabari.

Abbas aliongeza Serikali imewashirikisha wadau muhimu wakati wa mchakato wa kuandaa muswada huo ikiwemo Baraza la Habari Tanzania (MCT), Chama cha wamiliki wa vyombo vya habari (MOAT), Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) na baadhi ya wadau wa haki za binadamu. 

Aidha alitoa wito kwa wadau wote kutoa maoni yao kwa lengo la kuboresha muswada huo sheria kupitia barua pepe ya ofisi ya Bunge can.bunge.go.tz ili kuyawasilisha mbele ya kamati ya kudumu ya bunge ya huduma za maendeleo ya jamii.
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MUSWADA WA SHERIA ZA HABARI UTAIPA TASNIA HESHIMA-MKURUGENZI MAELEZO
MUSWADA WA SHERIA ZA HABARI UTAIPA TASNIA HESHIMA-MKURUGENZI MAELEZO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiC8imSEd4ws3uUGY1RDfTmWiwe5j7k_YUVo7dGC-kBPbcSycU9C9jo6eEcDPxlMNxisJCLYfUPyAydqj3Id3-ZWZDX0c-37r4icdLcygtx6bKPwok2dQe98Ekd4eOn5DPMsk3lVX47BdG_/s320/OTH_0561.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiC8imSEd4ws3uUGY1RDfTmWiwe5j7k_YUVo7dGC-kBPbcSycU9C9jo6eEcDPxlMNxisJCLYfUPyAydqj3Id3-ZWZDX0c-37r4icdLcygtx6bKPwok2dQe98Ekd4eOn5DPMsk3lVX47BdG_/s72-c/OTH_0561.JPG
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/10/muswada-wa-sheria-za-habari-utaipa.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/10/muswada-wa-sheria-za-habari-utaipa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy