Na Mwandishi Wetu BONDIA Mohamed Matumla anatarajia kupanda tena ulingoni siku ya Idi pili katika ukumbi wa TASUBA u...
Na Mwandishi Wetu
BONDIA Mohamed Matumla anatarajia
kupanda tena ulingoni siku ya Idi pili katika ukumbi wa TASUBA uliopo
Bagamoyo Mkoa wa Pwani kupambana na Koba Nodat katika uzito wa KG 57
mpambano wa raundi sita. Matumla anapambana mpambano huo baada ya mpambano
wake wa mwisho kumtwanga Mchina kwa point. Mratibu na promota wa mpambano huo,
Muhsin Sharif amesema mbali na mpambano huo kutakuwa na
mapambano mengine ya utangulizi litawakutanisha bondia Iddi Pialali
kutoka Kiwangwa Bagamoyo na Meshack Mwankemwa kutoka Mbeya mpambano wa
raundi nane Kg 66 wakati bondia machachari katika tasnia ya mchezo wa
masumbwi nchini Vicent Mbilinyi atavaana na Khalidi Hongo mpambano wa
raundi nne wakati Twalibu Tuwa atavaana na Sudi Sudi
Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa
na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi kali pamoja na kutambua
sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile
COMMENTS