WATEJA WA WOOLWORTHS WANUFAIKA NA NUSU BEI MPAKA PASAKA

Mteja wa muda mrefu wa  bidhaa zinazouzwa kwenye maduka ya Woolworths ambaye pia alikuwa Mgeni rasmi Manfred Ngantunga (kulia)  akifu...



Mteja wa muda mrefu wa  bidhaa zinazouzwa kwenye maduka ya Woolworths ambaye pia alikuwa Mgeni rasmi Manfred Ngantunga (kulia)  akifungua duka la Woolworths PPF tower baada ya kukata utepe alipozindua punguzo la bei la bidhaa kwa asilimia 50% zinazouzwa kwenye maduka ya hayo Tanzania.Uzinduzi huo ulifanyika Dar es Salaam jana. Pamoja naye ni Meneja Mkuu wa Woolworths, Joehans Mgimba, Afisa Fedha Mkuu, Samson Katemi (wa pili kushoto) na wateja mbalimbali wa duka hilo walioudhuria hafla hiyo. 

Mteja wa muda mrefu wa  bidhaa zinazouzwa kwenye maduka ya Woolworths ambaye pia alikuwa Mgeni rasmi Manfred Ngantunga (katikati)  akikabidhiwa zawadi na mfanyakazi wa duka hilo, baada ya kuzindua punguzo la bei la bidhaa kwa asilimia 50% zinazouzwa kwenye maduka ya hayo Tanzania. Kulia ni Meneja Mkuu wa Woolworths Joehans Bushiri. Hafla ya uzinduzi ilifanyika makao makuu ya woolworths  jijini Dar es Salaam.







Kulia ni Meneja Mkuu wa Woolworths Joehans Mgimba akiongea na wana habari wakati wa hafla ya uzinduzi huo.











Baadhi ya wateja waliohudhuria hafla hiyo

**********


Na Mwandishi Wetu         

Katika kipindi msimu huu wa sikukuu ya Pasaka Watanzania wanaweza kununua nguo zenye ubora kwa nusu bei kufuatia punguzo la asilimi 50 lililotangazwa jana na duka maarufu la nguo la Woolworths jijnini Dar Es Salaam.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa punguzo hilo, Meneja Mkuu Mkazi wa duka hilo Joehans Mgimba aliwaambia wateja waliofika dukani hapo kuwa punguzo hilo litadumu kwa muda wa wiki nne.

Alisema lengo kubwa la Woolworths ni kuwawezesha Watanzania wenye vipato  vya aina mbali mbali kufurahia sikukuu ya Pasaka kwa kupata nguo za kisasa zenye ubora kwa gharama nafuu.

Meneja huyo pia aliwaasa Watanzania kuachana na nguo za mtumba“Tunawasihi Watanzania kuepukana na matumizi ya nguo za mtumba kwani si salama kwa afya zao. Katika kipindi hiki cha sikukuu ya Pasaka duka la Woolworths linatoa punguzo kubwa ili kuwawezesha Watanzania kupata nguo mpya na zenye ubora.,” alisema.

Mgimba alisema duka hilo ambalo ni moja kati ya maduka makubwa ya nguo hapa nchini, litaendelea kuwahudumia wateja wake kwa kuwaletea nguo nzuri na zenye ubora kwa gharama nafuu na hivyo kuwasaidia kuepukana na nguo za mtumba.

“Mteja anayekuja kununua nguo dukani kwetu anakuwa amefanya uamuzi sahihi kwani atapa nguo zenye ubora kwa gharama nafuu na atakuwa amepata kitu ambacho kinaendana na thamani ya pesa yake,” alieleza

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa, duka hilo pia linatoa nafasi kwa wateja kununua nguo kwa kulipia kidogo kidogo hadi kwa muda wa miezi mitatu ili kuwawezesha wale wasio na fedha za kutosha kulipa mara moja kuweza kufurahia nguo zenye ubora.

Kuhakikisha wateja wetu wanapata vitu bora kabisa, vinavyoendana na wakati na kwa mda muafaka, Woolworths imeweza kubadilisha mfumo wa uletaji wa bidhaa nchini badala ya kutumia meli kama zamani sasa inatumia usafiri wa ndege. Kabla ya hapo tulikuwa tunnatumia muda wa mwezi mmoja hadi miwili kufikisha mizigo nchini wakati kwa sasa tunatumia mda wa wiki mbili hadi tatu.

Bwana Mgimba pia akasisitiza kwamba anapenda kuwahakikishia wateja wao kwamba Woolworths Tanzania ina bidhaa zote kama zinazopatikana South Africa na kwa bei zinazofaa kabisa. 

Kwa upande wake Manfred Ngatunga ambaye ni mmoja kati ya wateja wazuri wa duka hilo alitoa shukrani zake kwa uongozi wa duka hilo kwa kutoa punguzo kubwa haswa katika mismu huu wa sikukuu ya Pasaka.

Uamuzi wa punguzo la bei umekuja kipindi kizuri sana. Kipindi hiki na kipindi ambacho familia zinafanya manunuzi kwa ajili ya sikukuu ya Pasaka. Tunashukuru kwa kuwa tutapata nguo zenye ubora kwa nusu bei, kila mtu sasa anaweza kupendeza,” alieleza.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WATEJA WA WOOLWORTHS WANUFAIKA NA NUSU BEI MPAKA PASAKA
WATEJA WA WOOLWORTHS WANUFAIKA NA NUSU BEI MPAKA PASAKA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhk_4Tsm4wum4XpEPC2FjjxyyqcQ7qSDgUcCeRNK6U8_LiIJg3fftzOMx7MPdGoWiCrgayHTJN8PFSR-cjCAlXSjIM6oM-JDgOOd4S6C82uxbFqPacMn7rF9x3pKEPkXKHW8BVwW_gRqW7-/s1600/DSC_0609.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhk_4Tsm4wum4XpEPC2FjjxyyqcQ7qSDgUcCeRNK6U8_LiIJg3fftzOMx7MPdGoWiCrgayHTJN8PFSR-cjCAlXSjIM6oM-JDgOOd4S6C82uxbFqPacMn7rF9x3pKEPkXKHW8BVwW_gRqW7-/s72-c/DSC_0609.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2015/03/wateja-wa-woolworths-wanufaika-na-nusu.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2015/03/wateja-wa-woolworths-wanufaika-na-nusu.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy