MAMA SALMA KIKWETE AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA HOSPITALI YA WATOTO, ZINGA-BAGAMOYO. Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya ...
MAMA SALMA KIKWETE AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA HOSPITALI YA WATOTO, ZINGA-BAGAMOYO.
Mke
wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Mama
Salma Kikwete akisalimiana na Rais wa Shirika la International Health
Partiners (IHP)-JEMA Tanzania, Mama Mary Ellen Kitundu mara baada ya
kuwasili katika kijiji cha Zinga huko Bagamoyo, mkoani Pwani. Mama Salma
alikwenda kijijini hapo kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi la hospitali
ya watoto inayojengwa na Shirika la IHP-JEMA Tanzania,Katikati ni
Mkurugenzi wa Mradi huo Dkt. Jesse Kitundu.
Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete akifuatana na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo
Ndugu Ahmed Kipozi wakitembelea eneo linalojengwa hospitali ya watoto
itakayo kuwa na uwezo wa kuwa na vitanda 500 katika kijiji cha Zinga
huko Bagamoyo
Baadhi
ya wananchi kutoka katika kijiji cha Zinga na wageni waalikwa kwenye
sherehe ya uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali ya watoto
wakifurahia jambo wakati mgeni rasmi Mama Salma Kikwete alipokuwa
akizungumza kabla ya kuweka jiwe la msingi la hospitali hiyo.
Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete akizungumza na wageni waalikwa na wananchi
wa Kijiji cha Zinga wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la
hospitali ya watoto itakayokuwa na uwezo wa vitanda 500
Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete akifungua kitambaa kuashiria uwekaji rasmi
wa jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali ya watoto katika Kijiji cha
Zinga huko wilayani Bagamoyo tarehe 10.6.2014. Kushoto kwa Mama Salma ni
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Ndugu Ahmed Kipozi.
Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete akipanda mti kwenye eneo linalojengwa
hospitali ya watoto katika kijiji cha Zinga wilayanI Bagamoyo mara baada
ya kuweka jiwe la msingi
COMMENTS