BOCCO, OKWI SASA NI SAWA NA "PISHA NJIA" SIMBA YAIRARUA MAJIMAJI 4-0

Combination ya Nahodha wa Simba, John Raphael Bocco, A.K.A Adebayo, na mshambualiaji wa Kimataifa kutoka Uganda, Emmanuel Anold...






Combination ya Nahodha wa Simba, John Raphael Bocco, A.K.A Adebayo, na mshambualiaji wa Kimataifa kutoka Uganda, Emmanuel Anold Okwi, inazidi kuimarika, baada ya Januari 28, 2018 kila mmoja akipachika mabao mawili wakati Simba ikiibuka na ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Majimaji ya Songea kwenye pambano la kufunga raundi ya kwanza ya ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
John Bocco ndiye alikuwa wakwanza kufunga bao baada ya kuunganisha kwa kichwa kona iliyopigwa na Shizah Kicvhuya kutoka Magharibi mwa uwanja wa Taifa goli la Kusini, kunako dakika ya 16 na dakika 10 baadaye yaani dakika ya 26 John Bocco tena alifunga bao la pili kwa kichwa baada ya kuunganisha krosi ya Said Ndemla, kutoka upande wa Mashariki, goli la kusini mwa uwanja wa Taifa. 
Timu zilienda mapumzikoni Simba ikiwa mbele kwa mabao 2-0.


Combination ya Bocco na Okwi, pia imeonekana kuleta manufaa, kwani wamekuwa wakielewana vilivyo uwanjani na hivyo kuwapa chaguo gumu walinzi wa timu pinzani wasijue ni yupi wamkabe sana.
Safari hii bao la tatu la Simba, lilifungwa na Emmanuel Okwi, kufuatia kazi kubwa iliyofanywa na John Bocco, ambaye alikokota mpira kutoka mita chache kwenye mduara wa uwanja, na kukipita "kijiji" cha walinzi wa Majimaji, kabla ya kumimina krosi ya chini chini na kumkuta Okwi upande wa Mashariki mwa uwanja wa Taifa ambapo kabla ya kupachika bao hilo "alimfinya: mlinzi wa Majimaji na kufumua shuti kwa kutumia mguu wake wa kushoto na kupachika bao.


Bao la nne la Simba lilifungwa tena na Okwi, kufuatia kona ya Shizah Kichuya, ambayo ilikuja chini chini wakati mlinzi wa Majimaji akijaribu kuokoa mpira ulipaa juu na kuja katikati ya goli ambapo Okwi alijitwisha kwa kichwa na kipa kuokoa lakini Okwi a,ifanikiwa tena kuunasa mpira huo na kuutumbukiza kimiani.
Simba sasa wamefikisha pointi 35 na magoli 35 wakiwa mbele ya Azam FC na Yanga. Msimamo wa VPL hadi sasa ambapo raundi ya kwanza imemalizika ni kama ulivyo hapo chini.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: BOCCO, OKWI SASA NI SAWA NA "PISHA NJIA" SIMBA YAIRARUA MAJIMAJI 4-0
BOCCO, OKWI SASA NI SAWA NA "PISHA NJIA" SIMBA YAIRARUA MAJIMAJI 4-0
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh41N1i92v5cxjVilBVoZuSIkKrVjftlm5Db7C3afbMBYxP4qasPdN9GsQxh0tTaHNnyUVykxJ_HKqu8FtJr877-K-0WIZ_FWZJ61IBFfWIA3IgysuwfC5kpDtRCyt8QoaXk-Wai2I05jIv/s640/IMG-20180128-WA0067.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh41N1i92v5cxjVilBVoZuSIkKrVjftlm5Db7C3afbMBYxP4qasPdN9GsQxh0tTaHNnyUVykxJ_HKqu8FtJr877-K-0WIZ_FWZJ61IBFfWIA3IgysuwfC5kpDtRCyt8QoaXk-Wai2I05jIv/s72-c/IMG-20180128-WA0067.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2018/01/bocco-okwi-sasa-ni-sawa-na-pisha-njia.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/01/bocco-okwi-sasa-ni-sawa-na-pisha-njia.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy