WASHIRIKI KUTOKA RWANDA NA BURUNDI WAPIGANA NDANI YA KIJIJI CHA MAISHA PLUS

Katika hali isiyotarajiwa katika kijiji cha Maisha Plus, jana washiriki wawili, KAREKEZI Jean kutoka Rwanda na BASWARI Nib...












Katika hali isiyotarajiwa katika kijiji cha Maisha Plus, jana washiriki wawili, KAREKEZI Jean kutoka Rwanda na BASWARI Nibigira kutoka Burundi walipigana hadharani huku wakirekodiwa na camera zilizofungwa kijijini hapo. 


Ilikua hivi;

SOLANGE kawakuta KAREKEZI na PATRICK wamekaa wanapiga stori akawaambia kwamba BASWARI alikua anamsema KAREKEZI kwa watu. 

KAREKEZI hakuonyesha kufurahishwa na ile hali, akapata hasira, PATRICK akachochea, akamwambia asikubali kudharauliwa, lazima akapigane. 

"Muacheni, kwani nyie hamjui BASWARI anavyojifanya anajua kila kitu?" SOLANGE akahoji.

PATRICK akaendelea kushauri kwamba KAREKEZI asikubali kuliacha liishie hapo.. Akampige BASWARI. 


Baada ya kuona KAREKEZI anashawishika kwenda kupigana 

SOLANGE akamzuia asiende ili isijulikane kwamba yeye ndio ameleta hizo taarifa. 


KAREKEZI akiwa amekasirika akasema, "Mimi sipendi dharau... awe anawadharau nyie wanawake sio sisi wanaume." 


PATRICK akazidi kuchochea.. 'Nenda kampige asituchukulie hivyo... Kwanini atuseme vibaya?'


SOLANGE: "Usimdanganye mwenzio aende kupigana... Be gentle, men can't act like that... be gentle..''


Baada ya kuona mambo hayataishia pale, SOLANGE akaomba wasiseme kama yeye ndio ameleta hayo maneno.


KAREKEZI akamfuata BASWARI. Akamshika. BASWARI naye akamshika. Wakavutana. KAREKEZI akamwambia BASWARI, "Usiwe unaingilia maisha yangu, haunijui, wala sipendi unavyonisema kwa watu..." 


KAREKEZI akamtukana BASWARI kwa kifaransa. 


Ugomvi ukaendelea kwa muda.


SOLANGE akakasirika akatoka eneo la tukio akaona kama amesalitiwa... "Kwanini umenifanyia hivi, watu wakijua mimi ndio nimesema hayo maneno nitakua na bad image kwenye society.."


"Unaharibu reputation yetu kwa kugombana kijijni."


BABU hapendagi Ujinga. Kuna kikao cha kijiji asubuhi hii. Mjadala mkali unaendelea juu ya hatima ya hawa washiriki. Tukutane Azam Two saa 3.30 usiku kujua kitakachojiri. 



#VijanaNdioNgazi #HapaKaziTu

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WASHIRIKI KUTOKA RWANDA NA BURUNDI WAPIGANA NDANI YA KIJIJI CHA MAISHA PLUS
WASHIRIKI KUTOKA RWANDA NA BURUNDI WAPIGANA NDANI YA KIJIJI CHA MAISHA PLUS
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiWwDaeWLJVB-29wpSJe6gIDCBUtfLguDqiNWWc3CRhe3VQhR6NUz4qZZZET-mUKXuGtlcwzb81zXwhFjIQEold8DJMEuMv_gWk5PqC2tS2w2aoNv9RsUWL_7ttXKckoZ9nh0ovMwqXh5I/s640/WhatsApp+Image+2016-09-28+at+14.57.08+%25281%2529.jpeg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiWwDaeWLJVB-29wpSJe6gIDCBUtfLguDqiNWWc3CRhe3VQhR6NUz4qZZZET-mUKXuGtlcwzb81zXwhFjIQEold8DJMEuMv_gWk5PqC2tS2w2aoNv9RsUWL_7ttXKckoZ9nh0ovMwqXh5I/s72-c/WhatsApp+Image+2016-09-28+at+14.57.08+%25281%2529.jpeg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2016/09/washiriki-kutoka-rwanda-na-burundi.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/09/washiriki-kutoka-rwanda-na-burundi.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy