KAMANDA SIRO AZUNGUMZIA MIKAKATI YA OPERESHINI YA KUPAMBANA NA UHALIFU PAMOJA NA BODA BODA

Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii. JESHI la Polisi kanda Maalumu ya Dar es Salaam limekamata Marobota 10 ya vitenge na Katoni ...




Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
JESHI la Polisi kanda Maalumu ya Dar es Salaam limekamata Marobota 10 ya vitenge na Katoni 17 za Pampers  pamoja na Gari lililotumika kubebea hitu hivyo katika eneo ya Gezaulole lililopo pembezoni mwa ufukwe wa bahari ya Hindi.

Hayo yamesemwa na Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, amesema kuwa kukamatwa kwa gari lenye vitu hivyo ni mara baada ya kupewa taarifa na Raia wema kwa kuwa katika eneo hilo kunapitishiwa mali zisizotolewa ushuru.

Siro amesema kuwa Gari lililo kamatwa na Vitenge na Pampers ni aina ya Suzuki Carry lenye namba za usajili T490 CQB ambalo nalo linashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam.

Pia Sirro amesema kuwa mwananchi anaeona kuwa alitelekeza gari hilo lililo na vitu hivyo ajisalimishe Polisi ili apelekwe Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) akalipie ushuru wa vitu hivyo.

Katika Operesheni nyingine Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam lilifanikiwa kukamata gari moja la wizi aina ya Toyota Noah lenye namba za usajili T 314 DFH  ambapo kabla ya kuibwa lilikuwa na namba za usajili T 622 DDR  ikiwa gari hilo ni Mali ya Hellen Michael liliibwa maeneo ya Kitunda Kivule ambapo lililuwa limeegeshwa nyumbani kwake. Pia Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam limkamata watu wawili wakiwa na Pikipiki mbili zenye namba za usajili MC343 ASL aina ya Boxer na MC 606 ex aina ya Fercon ambazo ni za wizi na watuhumiwa hao kukuli kuwa wameziiba Pikipiki hizo.

Jeshi la Polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam kwa kipindi cha wiki moja limefanikiwa kukamata Pikipiki 519 katika Operesheni ya ukamataji wa Pikipiki kwa makosa mbalimbali operesheni hiyo ilifanywa katika mikoa ya Ilala piki[iki 183,Kinondoni pikipiki 139 na Temeke pikipiki 197.
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro  akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo kuhusina na Operesheni ya kukamata Pikipiki519 pamoja na gari lililokuwa na Vitenge marobota 10 na Pampers katoni17 katika eneo la Gezaulole pemeni mwa ufukwe wa bahari ya hindi ambapo eneo hilo linatumika kupitisha mali zisizolipiwa ushuru.

Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro akionyesha Baadhi ya Vitenge na Pempers zilizokamatwa katika operesheni ya Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro akionyesha gari lilokamatwa na vitenge na Pampers.
Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro akionesha pikipiki 519 ambazo zimekamatwa ja jeshi la Polisi kanda Maalum ya Dar es Salaam.
Kamanda Sirro akionesha mali zilizokamatwa katika Operesheni hiyo ya kupambana na Uhalifu,mbele ya Waandishi wa Habari,leo jijini Dar.


Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro akizungumza mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo jijini Dar,kuhusiana na suala zima la Operesheni ya kupambana na Uhalifu pamoja na Bodaboda.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: KAMANDA SIRO AZUNGUMZIA MIKAKATI YA OPERESHINI YA KUPAMBANA NA UHALIFU PAMOJA NA BODA BODA
KAMANDA SIRO AZUNGUMZIA MIKAKATI YA OPERESHINI YA KUPAMBANA NA UHALIFU PAMOJA NA BODA BODA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgPQuGeFu1K1LJNxaBkilXjyqBHYCIa6JIGnRSFqHyVtL3RsA8VlniMtKH1UrGI1Ib9ztvpjla5ooGbweQmqU7NBy_oSM6MPJ63YTWH-fiW_t9-5QzGl7M2P3sRuZ1E4tEddUDyT10XsCAB/s640/DSCF2219.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgPQuGeFu1K1LJNxaBkilXjyqBHYCIa6JIGnRSFqHyVtL3RsA8VlniMtKH1UrGI1Ib9ztvpjla5ooGbweQmqU7NBy_oSM6MPJ63YTWH-fiW_t9-5QzGl7M2P3sRuZ1E4tEddUDyT10XsCAB/s72-c/DSCF2219.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2016/04/kamanda-siro-azungumzia-mikakati-ya.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/04/kamanda-siro-azungumzia-mikakati-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy