OFISI YA MPIGA CHAPA MKUU WA SERIKALI YAWATAKA WANANCHI KUHESHIMU TUNU ZA TAIFA

Na Frank Shija, MAELEZO Katika kuhakikisha heshima , hadhi na maadili miongoni mwa jamii ya Watanzania Serikali ya Awamu ya Tano c...




Na Frank Shija, MAELEZO
Katika kuhakikisha heshima , hadhi na maadili miongoni mwa jamii ya Watanzania Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi mahiri wa Rais John Pombe Magufuli imewakumbusha wananchi  kuheshimu na kuzingatia matumizi sahihi ya Vielelezo vya Taifa.
Haya yamebainishwa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali Cassian Chibogoyo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Kipindi chake cha ‘Tujikumbushe’’ Sehemu ya Pili kilichofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Chibogoyo amesema amesema kuwa wakati sasa umefika kwa jamii kuendeleza utamaduni uliokuwapo wa kuheshimu na kufuata desturi zilizowekwa katika kuendeleza umoja, amani na mshikamano.
‘Natoa wito kwa watanzania wote, katika kufanya maboresho ya kurejesha hadhi ya taifa tunapaswa kuheshimu sana Vielelezo vya Taifa letu, hapa na maanisha tuheshimu wimbo wa taifa na Nembo ya Taifa.’
Amesema kuwa katika kuhakikisha vielelezo hivyo vinaheshimiwa Ofisi yake imejipanga kufuatilia kwa karibu wale wote watakao kiuka matumizi sahihi ya Vielelezo vya Taifa ikiwemo Nembo, Bendera na Wimbo wa Taifa.
Aliongeza kuwa kuanzia sasa matumizi ya Bendera ya Taifa yatakwenda sambamba na matumizi ya Bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki hivyo amezitaka Ofisi zote za Serikali pamoja na Taasisi zake waanze utaratibu wa kupandisha pia bendera hiyo kwani Tanzania tunaamini katika ushirikiano huo.
Katika hatua nyingine uongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu (TUGHE) Tawi la Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali wamekanusha tuhuma zilizoandikwa na moja ya gazeti hapa nchini(Jina limehifadhiwa) zikimtuhumu Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kuwa na kusema kuwa tuhuma zilizoandikwa katika Gazeti hilo siyo zakweli na ata wao kama wafanyakazi wameshangazwa
Katibu wa TUGHE Tawi la Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali amesema kuwa ni vyema waandishi wakafanya kazi zao kwa weledi kuliko kuandika taarifa zizizosahihi kwani kufanya hivyo kuta waingiza matatizoni.
Nilitegemea kabla mwandishi hajachapisha habari ile angetafuta ukweli kutoka upande wa pili ikiwemo kuhusishwa kwa uongozi wa Chama cha Wafanyakazi kwani ndiyo wenye mamlaka yakutoa taarifa katika ngazi husika kwa tupo kwa ajili ya kuwawakilisha na kuwatetea wafanyakazi.
Kipindi cha Tujikumbushe kimekuwa kikionyeshwa na TBC1 ambapo lengo lake kuu ni kutoa elimu kwa jamiii juu ya matumizi sahihi na umuhimu wa kutunza nyaraka na tunu za Taifa, ambapo Sehemu ya Kwanza ya kipindi hicho kilihusu Nyaraka za Serikali. Kipindi kinachofuata kitahusu Historia ya kuwepo kwa Katiba na Katiba inayopendekezwa.

Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali, Kassian Chibogoyo (kusho) akionesha kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) rangi sahihi zinazotakiwa kutumika katika bendera ya Taifa wakati akielezea umuhimu wa wananchi kutumia vielelezo sahihi vya Taifa na kuachana na vile vya kughushi. Kulia ni Afisa Habari toka Idara ya Habari (Maelezo) Frank Shija.

Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali, Kassian Chibogoyo akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu umuhimu wa wananchi kutumia vielelezo sahihi vya Taifa na kuachana na vile vya kughushi. Kushoto ni Afisa Habari toka Ofisi ya Waziri Mkuu, Nyamagori Omari

Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali Bw. Kassian Chibogoyo (katikati) akionesha kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) baadhi ya vielelezo sahihi vya Taifa vinavyotakiwa kutumiwa na wananchi wakati alipokuwa akielezea umuhimu wa wananchi kutumia vielelezo sahihi vya Taifa na kuachana na vile vya kughushi mapema hii leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Habari toka Idara ya Habari (Maelezo) Frank Shija na Afisa Habari toka Ofisi ya Waziri Mkuu Nyamagori Omari. (Picha zote na Eliphace Marwa - Maelezo)







COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: OFISI YA MPIGA CHAPA MKUU WA SERIKALI YAWATAKA WANANCHI KUHESHIMU TUNU ZA TAIFA
OFISI YA MPIGA CHAPA MKUU WA SERIKALI YAWATAKA WANANCHI KUHESHIMU TUNU ZA TAIFA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhxy_eAEtiKaNC_AhVzS3nVM0KVh6rbTkyBYyWqsS4dQv9gWPbVPf0XbtELtoSaySzrfOlgyjm124XsPt4zWclrInh0Ajv2jttiTDtMwMTHs1gxHhciQ8NRrh-7E0FU-BLAb7Dh9I-Vwpo/s640/GP+01.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhxy_eAEtiKaNC_AhVzS3nVM0KVh6rbTkyBYyWqsS4dQv9gWPbVPf0XbtELtoSaySzrfOlgyjm124XsPt4zWclrInh0Ajv2jttiTDtMwMTHs1gxHhciQ8NRrh-7E0FU-BLAb7Dh9I-Vwpo/s72-c/GP+01.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2016/07/ofisi-ya-mpiga-chapa-mkuu-wa-serikali.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/07/ofisi-ya-mpiga-chapa-mkuu-wa-serikali.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy