HUYU NDO MWANASHERIA MKUU WA ZANZIBAR, OTHMAN MASOUD ALIYEFUTWA KAZI JANA NA RAIS SHEIN

Mwanasheria Mkuu wa serikali ya mapinduzi Zanzibar, Othman Masoud Othman, a...



Mwanasheria Mkuu wa serikali ya mapinduzi Zanzibar, Othman Masoud Othman, amefutwa kazi na mteule wake, rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein.
Tayari Dkt. Shein amemteua aliyekuwa naibu mwanasheria mkuu, Said Hassan Said, kuchukua nafasi yake.
Kwa mujibu wa taarifa ya serikali,iliyopatikana Oktoba 7, 2014 kwa vyombo vya habari Masoud amefutwa kazi kwa mujibu wa vifungu namba 53 na 54 (1) na 55 (3) vya katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, na kifungu namba 12 (3) sheria ya utumishi wa umma ya Zanzibar ya mwaka 2011.
Itakumbukwa ya kwamba, Masoud, alijiondoa kwenye kamati ya uandishi ya bunge maalum la Katiba, bila ya kutoa sababu zozote huku akiwa mshauri mkluu wa sharia wa serikali hiyo na alionekana siku ya pili ya upigaji kura kuamua hatma ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayopendekezwa na bunge hilo.
Jambo lililowashtua wengi, katika kura yake ambayo ilikuwa ya wazi, alipiga kura ya hapana akikataa vifungu kadhaa vya katiba hiyo, hali iliyoamsha hamasa kutoka kwa baadhi ya wajumbe wa b unge hilo kutoka Zanzibar, na kupiga makelele ya kutaka aondolewe kwenye nafasi hiyo.
Hali hiyo iliwalazimu maafisa wa usalama wa bunge hilo, kumpatia ulinzi maal;um wakati akiondoka bungeni hapo ili kumuepiusha na kipigo kiutoka kwa wajumbe wa Bunge hilo.

Mwanasheria Mkuu mpya wa serikali ya mapinduzi, Zanzibar, Said Hassan Said.

Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein

Spika wa baraza la wawakilishi Zanzibar, Pandu Ameir Kificho, (kushoto), akiteta jambno na aliyekuwa mwanasheria mkuu wa serikali ya mapinduzi Zanzibar, Othman Masoud Othman, mwanzoni mwa vikao vya bunge maalum la katiba mjini Dodoma.

Askari wa bunge wakimsindikiza mwanasheria mkuu wa serikali ya mapinduzi Zanzibar, Othman Masoud Othman, (Wa pili kulia), wakatin akitolewa kwenye ukumbi wa bunge hilo kupitia mlango wa nyuman kumuepusha na kipigo toka kwa wajumbe kutoka Zanzibar. Kulia ni spika wa baraza la wawakilishi Pandu Ameir Kificho, ambaye alitumia gari lake kumtorosha kutoka viwanja vya bunge. (Imeandaliwa na K-VIS Blogs)

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: HUYU NDO MWANASHERIA MKUU WA ZANZIBAR, OTHMAN MASOUD ALIYEFUTWA KAZI JANA NA RAIS SHEIN
HUYU NDO MWANASHERIA MKUU WA ZANZIBAR, OTHMAN MASOUD ALIYEFUTWA KAZI JANA NA RAIS SHEIN
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj8t3Yjl8lWfvVkKrkd4-8wFNF_sFvrB3fDLzpTd15hCPTg2pdx6SMRWD4S-Q53h6nhQrYVbAk5e7kqvQ0LDjPY6ZcpCNlM3YzxvFlkkE0crGe-BzO39r-o7EowwNO-GsmhcMZIvqyLhaQ/s1600/Othman+Masoud+Othman8.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj8t3Yjl8lWfvVkKrkd4-8wFNF_sFvrB3fDLzpTd15hCPTg2pdx6SMRWD4S-Q53h6nhQrYVbAk5e7kqvQ0LDjPY6ZcpCNlM3YzxvFlkkE0crGe-BzO39r-o7EowwNO-GsmhcMZIvqyLhaQ/s72-c/Othman+Masoud+Othman8.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2014/10/huyu-ndo-mwanasheria-mkuu-wa-zanzibar.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2014/10/huyu-ndo-mwanasheria-mkuu-wa-zanzibar.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy