WANAFUNZI WANAWAKE CHUO CHA ELIMU YA BIASHARA DAR WAWEKA HISTORIA, WAANZISHA MFUKO WA KUWAKOMBOA KIELIMU.

WANAFUNZI WANAWAKE CHUO CHA ELIMU YA BIASHARA DAR WAWEKA HISTORIA, WAANZISHA MFUKO WA KUWAKOMBOA KIELIMU. Baadhi ya wanafunzi wa kike ...

WANAFUNZI WANAWAKE CHUO CHA ELIMU YA BIASHARA DAR WAWEKA HISTORIA, WAANZISHA MFUKO WA KUWAKOMBOA KIELIMU.



Baadhi ya wanafunzi wa kike wa chuo hicho wakifurahia  matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea wakati wa hafla ya uzinduzi wa  mchakato wa kuanzisha mfuko wa Jumuiya ya Wanafunzi wa kike chuoni hapo wenye lengo la kuwakomboa kielimu, kisiasa na kiutamaduni leo jijini Dar es Salaam.

Igizo la wanafunzi wakiwa kwenye majadiliano chuoni hapo bila kujali tofauti za jinsia .



Wanafunzi wa Kike wa chuo cha CBE wakiwa kwenye maandamano kuelekea eneo la tukio.

Moja ya kundi la Burudani la Waswahili Classic Group la chuo hicho likitoa buruduni wakati wa hafla ya uzinduzi wa mfuko huo.
Kikundi cha maagizo cha chuo hicho kikionyesha namna vitendo vya ukiukwaji wa maadili unavyodhibitiwa chuoni hapo na namna uongozi wa chuo hicho unavyowachukulia hatua za kinidhamu wanaokiuka maadili ya chuo hicho.

Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Mary Mwangisa (kulia) akizungumza  na wanafunzi wa Kike wa chuo cha CBE kampasi ya Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa  mchakato wa kuanzisha mfuko wa Jumuiya ya Wanafunzi wa kike chuoni hapo wenye lengo la kuwakomboa kielimu.

Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Mary Mwangisa (kulia) akizungumza jambo kabla ya kuanza kwa maandamano ya wanafunzi wa kike wa chuo cha CBE kampasi ya Dar es Salaam kuzindua  mchakato wa kuanzisha mfuko wa Jumuiya ya Wanafunzi wa kike chuoni hapo wenye lengo la kuwakomboa kielimu. Kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya Taaluma ya Chuo hicho Dkt. Ellen Otaru Okoedion.
Baadhi ya wanafunzi wa Kike wa Chuo cha CBE wakiwa wamebeba bango lenye ujumbe mahususi kutetea haki za wanawake na usawa wa kijinsia wakati wa uzinduzi wa mfuko maalum wa Jumuiya ya Wanafunzi wa kike wa chuo hicho.


Waziri wa Wanawake wa Chuo cha Elimu ya Biashara Dar es Salaam (CBE) Bi. Mwajuma Sangali akiwaongoza wananfunzi wa Kike wa chuo hicho wakati wa uzinduzi  wa mchakato wa kuanzisha mfuko wa Jumuiya ya Wanafunzi wa kike wenye lengo la kuwakomboa kielimu.
Wanafunzi wa Kike wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Mary Mwangisa (katikati). (Picha na Aron Msigwa – MAELEZO)

--------------------------------------------------------

Na. Aron Msigwa – MAELEZO.
22/3/2014. Dar es salaam.

Wanafunzi wanawake wa Chuo cha Elimu ya Biashara Dar es salaam (CBE) wamezindua mchakato wa kuanzisha mfuko wa Jumuiya ya wanafunzi wa kike wenye lengo la  kumkomboa na kumwezesha mwanafunzi wa kike kujitambua, kielimu, kisiasa na kiutamaduni.

Akizungumza na jumuiya ya wanafunzi wa kike wa chuo hicho wakati wa uzinduzi  wa mfuko huo  leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Mary Mwangisa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo amesema kuwa kuanzishwa kwa jumuiya hiyo  ni ishara ya umoja na mshikamano wa wanafunzi wa kike chuoni hapo.

Amesema kuanzishwa kwa mfuko huo kunatokana na kuongezeka kwa changamoto mbalimbali zinazowakabili wanawake pia  kukosekana kwa mifuko ya aina hiyo katika taasisi nyingi za elimu ya juu hapa nchini.

Ameeleza kuwa  malengo ya mfuko huo ni kumwezesha mwanafunzi wa kike wa CBE kujitambua kielimu, kisiasa na kiutamaduni na kuongeza kuwa yamekuja  wakati muafaka kufuatia  mabadiliko yaliyopo sasa ya kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiutamaduni.

 Amefafanua kuwa mfuko huo ulioanzishwa katika chuo hicho ni fursa pekee ya kuwawezesha wanafunzi wa kike kunufaika kwa kupata elimu bora bila vikwazo.

“Napenda kutumia fursa hii kuushukuru uongozi wa chuo hiki kwa kuonyesha njia ya kuwajali wanawake na pia katika kuweka taratibu nzuri za kulinda maadili, katika maisha yangu sijawahi kusikia chuo kikuu chochote kimezindua jukwaa la wanawake lenye malengo mazuri kama yenu” Amesema Dkt. Mwangisa.

Ameeleza kuwa kwa muda mrefu wanawake kote nchini wamekuwa na juhudi  mbalimbali za kujikomboa kiuchumi pamoja na kulitumikia taifa kwa kushika nyadhifa mbalimbali serikalini kwa ufanisi mkubwa na kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii pindi wanapokabidhiwa madaraka.

“Ninapowaangalia ninyi nafarijika maana naona viongozi wakuu wa serikali, naona marais na pia wakurugenzi wa biashara”

Akizungumza kuhusu kuanzishwa kwa mfuko huo na mafanikio yake  Dkt. Mwangisa amesema kuwa atatoa ushirikiano kwa wanafunzi hao ili kuhakikisha kuwa mfuko huo unajengewa uwezo wa  kusimama na kuwanufaisha wanawake wanaokumbwa na changamoto zinazokwamisha maendeleo yao ikiwemo ukosefu wa fedha.

Amesema kuwa kukamilika kwa taratibu za jumuiya hiyo ikiwemo maandalizi ya katiba ya jukwaa hilo kutaliwezesha jukwaa hilo kupanga, kuandaa na kutekeleza mikakati mbalimbali ya kujiendesha ili kuwawezesha wanafunzi hao kutatua changamoto zinazowakabili kwa kulinda heshima yao katika jamii.

Kwa upande wake mjumbe wa Bodi ya Taaluma ya Chuo hicho Dkt. Ellen Otaru Okoedion amesema kuwa wanafunzi wa kike wa chuo hicho wanahitaji msaada kupitia mfuko huo utakaowawezesha kupambana na wimbi la wanafunzi wa kike kushindwa kumaliza masomo yao kwa kushindwa kumudu gharama za masomo.

Amewataka wanafunzi wa kike wa chuo hicho kutumia ipasavyo taaluma wanayoipata  kusaidia mfuko huo kupata fedha  ili uwe endelevu kwa maendeleo ya wanawake na chuo hicho.

“Ninyi mnasoma elimu ya biashara na ndio watalaam wenyewe sitarajii mfuko wenu ukose uwezo, naamini mtatumia taaluma yenu mnayoipata hapa chuoni kutafuta fedha kwa kuwa mnao uwezo huo” Amesisitiza Dkt. Ellen.

Naye Waziri wa Wanawake wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Bi. Mwajuma Sangali ameeleza kuwa wanawake kote nchini wana jukumu la kuandaa kizazi cha watu wenye upendo, uzalendo, kupenda kazi na maendeleo.

Amesema kuanzishwa kwa chombo hicho kunalenga kuboresha maisha ya wanawake hasa katika masuala ya elimu,jamii,uchumi na siasa






















COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WANAFUNZI WANAWAKE CHUO CHA ELIMU YA BIASHARA DAR WAWEKA HISTORIA, WAANZISHA MFUKO WA KUWAKOMBOA KIELIMU.
WANAFUNZI WANAWAKE CHUO CHA ELIMU YA BIASHARA DAR WAWEKA HISTORIA, WAANZISHA MFUKO WA KUWAKOMBOA KIELIMU.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjvlUE5ALhKtx8Vs20-yoltjqhTHFGnmjyls3kGf8RRCbry8t3FeGP4CWXoXsiyU7uejWQlEtKna9nL2TzIJ1OesSB_WGh0m6vCZZpdHefZNL69R6SERTK24EKcPJqC-vitcX4wWxvt1uY/s1600/Picha+na+9.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjvlUE5ALhKtx8Vs20-yoltjqhTHFGnmjyls3kGf8RRCbry8t3FeGP4CWXoXsiyU7uejWQlEtKna9nL2TzIJ1OesSB_WGh0m6vCZZpdHefZNL69R6SERTK24EKcPJqC-vitcX4wWxvt1uY/s72-c/Picha+na+9.jpg
Okandablogs
https://robertokanda.blogspot.com/2014/03/wanafunzi-wanawake-chuo-cha-elimu-ya.html
https://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2014/03/wanafunzi-wanawake-chuo-cha-elimu-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy