Na Emmanuel Masaka,Globu ya jamii MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amepokea tani 120 za saruji ambazo ni sawa na mifuko 2,400 ya s...
Na Emmanuel Masaka,Globu ya jamii
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda
amepokea tani 120 za saruji ambazo ni sawa na mifuko 2,400 ya saruji kutoka kwa Vyama vya ushirika 27 vya Mkoa huo vilivyoguswa na kempeni ya ujenzi wa ofisi 402 za walimu Dar es Salaam.
Mifuko hiyo 2,400 ina uwezo wa kufyatua tofali 70,000 ambazo zitajenga ofisi 14 za kisasa kwa ajili ya Walimu.
Akizungumza baada ya kupokea mifuko hiyo Makonda amesema shughuli ya ujenzi wa ofisi za walimu inaendelea vizuri na amewashukuru wadau wote wanaoendelea kuchangia kampeni hiyo inayolenga kuboresha mazingira ya kazi kwa walimu ili waweze kutoa elimu bora kwa wanafunzi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jukwaa la Ushirika Dar es Salaam Tumaini Wilfred amesema wameguswa na jitiada zinazofanywa na Makonda katika kuboresha mazingira ya walimu.
Amesema ndio maana wameona umuhimu wa wao kama ushirika wasibaki nyuma katika kufanikisha jambo hilo ambalo ni jema na na la ukombozi wa fikra na kuongeza ushirika utaendelea kuunga mkono kwa kila hali juhudi zinazifanywa na Makonda.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda (kulia) akizungumza machache Machi 16 2018, jijini mara baada ya kupokea tani 120 za saruji ambazo ni sawa na mifuko 2,400 ya saruji jijini Dar es Salaam. (Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii).
COMMENTS