RC MASENZA AZIPIGA JEKI SHULE TANO MKOANI IRINGA

  Mkuu wa mkoa Amina Masenza akiwa na viongozi mbalimbali wakikagua moja ya shule ya sekondari ambayo inajengwa kwa nguvu za wananc...





 Mkuu wa mkoa Amina Masenza akiwa na viongozi mbalimbali wakikagua moja ya shule ya sekondari ambayo inajengwa kwa nguvu za wananchi na serikali kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu mkoani Iringa

 Mkuu wa mkoa Amina Masenza akiwa na viongozi mbalimbali wakikagua moja ya shule ya sekondari na akiuliza kitu kuhusu ujenzi wa shule ya sekondari ya Nyanzwa

 Mkuu wa mkoa Amina Masenza akiwa na viongozi mbalimbali wakikagua moja ya shule ya sekondari akielekea kukagua vyoo vya shule ya sekondari ya Nyanzwa

 Mkuu wa mkoa Amina Masenza akiwa na viongozi mbalimbali wakikagua vyoo vya shule ya Nyanzwa

 Mkuu wa mkoa Amina Masenza akiwa na viongozi mbalimbali wakikagua vyoo katika sekondari ya Ibumu

 Na hili ni moja ya jengo ambalo linajengwa kwa ajili ya maabara za shule ya sekondari ya Ibumu

Na Fredy Mgunda,Kilolo



MKUU
wa mkoa wa Iringa Amina Masenza ametoa jumla ya shilingi milioni nne (4,000,000)
kwa ajili ya kuchochea manendeleo ya ujenzi
majengo kwenye shule nne za sekondari  ikiwa na lengo la kuhakikisha kuwa wanafunzi
wa shule hizo wanasoma bila kuwa na usumbufu wowote ule.

Akizungumza
wakati wa ziara ya kukagua ujenzi wa shule mpya za sekondari zilizopo tarafa ya
Mazombe mkuu wa mkoa Amina Masenza alisema kuwa serikali ya awamu ya tano chini
ya Rais Dr John Pombe Magufuli imejipanga kuhakikisha wanafunzi wanasoma bila
kulipia kitu mchango wowote ule utakaochangishwa na walimu.

“Mimi
nimetumwa na Rais kusisimamia ila ya chama cha mapinduzi kuhakikisha inatendewa
haki katika kuleta maendeleo hivyo ni lazima nihakikishe wanafunzi wanakwenda
shule na sio vinginevyo maana bila wanafunzi kwenda shule Rais hawezi kunielewa
nitakuwa sijatimiza malengo ya kutoa elimu bila malipo” alisema Masenza

Masenza
alisema kuwa atachangia shilingi milioni moja kwa kila shule za sekondari za
tarafa hiyo ambazo zipo kwenye ujenzi na shule hizo ni Ibumu na Nyanzwa ili
kuhakikisha wanafunzi wanasoma na kuwapunguzia umbali wa kutoka eneo moja
kwenda eneo jingine kuifuata shule.

“Naombeni
tuzikamilishe shule hizi kwa wakati ili kuwapunguzia umbali wa kusoma watoto
wetu haiwezekani wanafunzi hadi kuikuta shule moja ni umbali wa zaidi ya
kilometa kumi na tatu ,jamani hawa ni watoto zetu na maisha yao yanategemea
elimu hivyo ni lazima tuwekeze kwenye elimu” alisema Masenza

Masenza
aliwataka viongozi wa vijiji kuhakikisha kuwa wanafunzi wote waliofulu na
kuchaguliwa kuingia kidato cha kwanza wapelekwe shule kwa wakati na wazazi wote
ambao hawajawapeleke shule watoto wao wachukuliwe hatua kwa kuwa Rais hataki
kuskia kuwa mtoto hajaenda shule.

“Jamani
Rais ameagiza kuwa wanafunzi wote wanatakiwa kuwa shule hata kama hawana sare
za shule sasa huyo mzazi gani ambaye hatakiwa kuwa peleka shule naombeni kabla
sijawakulia hatua nyinyi viongozi basi hakikisheni wanafunzi wote waliofaulu
wanakwenda shule” alisema Masenza

Lakini
mkuu wa mkoa alifanya ziara kwenye shule ya sekondari Kihesa manispaa ya Iringa
na akatoa kiasi cha shilingi laki tano (500,000),shule ya sekondari  Ilambilole shilingi milioni moja(1,000,000)
na shule ya msingi Matembo nako alitoa kiasi cha shilingi laki tano (500,000)
pesa zote hizo ni kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa majengo ya shule.

Aidha Masenza alisema
kuwa sasa imefika mwisho kwa watoto wa mkoa wa Iringa kuwa soko la wafanyakazi
wa kazi za ndani wakati wanauwezo wa kuwa viongozi hapo baadae.

“Nasema tena
haiwezekani kila mfanyakazi ukifika daresalaam utasikia katoka Iringa sasa
sitaki kusika swala hilo na wazazi wanaofanya hivyo nitawachulia hatua za
kisheria serikali ya awamu ya tano inataka kuwa na wasomi wengi ili kuasaidia
maendeleo ya nchi”alisema Masenza

Sipia
Kinyowa ni kaimu mtendaji wa kata ya Nyanzwa, Amidu Kilamba diwani wa kata ya
Nyanzwa,Hemerd Wiliamu diwani wa kata ya Ibumu na Justine Mgina mtendaji wa
kata ya Ibumu ni baadhi ya viongozi waliompungeza mkuu wa mkoa kwa ziara
aliyoifanya ya kimaendeleo na kimkatikati kuhakikisha wanafunzi wote wanatakiwa
kufika shule na kusoma bila kubuguziwa na mtu yeyeto.

“Leo
tumefarijiaka sana kuona mkuu wetu kaja na mikakati hasa ya kusaidia kukuza
maendeleo kwenye sekta ya elimu hivyo hatuna budi kumuunda mkono kuhakikisha
kuwa mambo aliyoyaongea tunayafanyia kzi ili kuhikisha wanafunzi wanasoma”
walisema vingozi

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: RC MASENZA AZIPIGA JEKI SHULE TANO MKOANI IRINGA
RC MASENZA AZIPIGA JEKI SHULE TANO MKOANI IRINGA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgvx2g6IX7m0fbYMOx0byB_NkHcIwZEacTCVJgnqfW937R_Z-c8xyjChJteVzF0neJUhUXRHXHKhEv2vhOz8o__fO8mrEd1eHq8hJRAl6YIxUuPacYiwIF29Tv80vpLRA9_i24JELcJzd1O/s640/IMG_0123.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgvx2g6IX7m0fbYMOx0byB_NkHcIwZEacTCVJgnqfW937R_Z-c8xyjChJteVzF0neJUhUXRHXHKhEv2vhOz8o__fO8mrEd1eHq8hJRAl6YIxUuPacYiwIF29Tv80vpLRA9_i24JELcJzd1O/s72-c/IMG_0123.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2018/01/rc-masenza-azipiga-jeki-shule-tano.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2018/01/rc-masenza-azipiga-jeki-shule-tano.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy